Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba
Juma Linaloanza Septemba 7
Dak. 15: Matangazo ya kwenu na matangazo yanayofaa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Zungumzia makala “Je! Kupendezwa Kwaweza Kuamshwa Tena?” na utoe onyesho fupi la jinsi ziara hiyo yaweza kufanywa.
Dak. 15: “Msifu Mungu wa Uumbaji.” Pitio la makala kwa maswali na majibu. Panga kimbele vijana walio mfano mzuri wasimulie mambo yaliyoonwa kutoka vichapo vilivyotajwa katika fungu 4, na mhubiri mwingine aweza kusimulia mambo yaliyoonwa yaliyotajwa katika fungu 5.
Dak. 15: “Utoaji Mbalimbali Unaochochea Kupendezwa.” Zungumza pamoja na wasikilizaji jinsi ya kutekeleza madokezo hayo katika eneo la kwenu. Pangia kuwe maonyesho mawili au matatu yaliyo halisi, na yaliyotayarishwa vizuri. Mahali ambapo kitabu Kuishi Milele kitatolewa hudumani, toa maonyesho ya madokezo yanayopatikana katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Agosti 1992, chini ya kichwa “Matangulizi ya Kuchochea Kupendezwa.”
Wimbo 96 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 14
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia ndani ripoti ya hesabu na shukrani kwa ajili ya upaji. Lipongeze kundi kwa utegemezaji wa ukarimu kwa mahitaji ya kwenu pamoja na kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote. Kadiri wakati uruhusuvyo, kuwe na mambo yaliyoonwa yaliyotayarishwa yanayohusiana na kutoa kitabu Creation.
Dak. 20: “Kulinda Salama Watoto Wenu na Matumizi Mabaya ya Damu.” Mzee atoe hotuba kuhusu mafungu 1-11. Elewesha wazi sababu ya mkataa kwamba wazazi wanaokubali tabibu amtibu mtoto wao chini ya hali zinazoelezwa katika mafungu 5-7 hawahitaji kuonwa kuwa wanaridhiana.
Dak. 15: “Hakikisha Kwamba Unarudi.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Toa wonyesho uliotayarishwa vizuri unaohusu habari iliyo katika fungu 6. Kazia uhitaji wa kuwazuru tena watu waliopendezwa uliowapata mapema mwezi huu.
Wimbo 10 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 21
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Simulia kifupi jambo la kwenu lililoonwa shambani au taja mambo ya kuzungumzia ambayo yanaweza kutumiwa juma hili katika utumishi wa shambani.
Dak. 15: “Kulinda Salama Watoto Wenu na Matumizi Mabaya ya Damu.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya mafungu 12-28. Kazia jibu la swali lililo katika fungu 20. Kazia kwamba matayarisho ya mapema ya wazazi katika kupata matibabu kwa ajili ya mtoto wao mara nyingi ndio ufunguo wa kufanikiwa ili kuepuka kutiwa damu mishipani.
Dak. 15: “Utasema Nini Unaporudi?” Zungumza pamoja na wasikilizaji na uwe na wahubiri waliojitayarisha kutoa maonyesho ya madokezo katika mafungu kadiri yanavyopitiwa. Maonyesho hayo mafupi yapaswa yatayarishwe kimbele.
Dak. 10: Kupitia Utendaji wa Kundi. Kwa kutumia tarakimu katika upande wa mbele wa Ripoti ya Mchanganuo wa Kundi (S-10-SW) iliyopelekwa kwa Sosaiti mapema mwezi huu, mwangalizi msimamizi na mwangalizi wa utumishi wazungumzia mambo makuu ya utendaji wa kundi kwa mwaka uliopita. Wapongeze wahubiri na mapainia kwa uchangamfu kwa ajili ya jitihada zao za kujinyima katika utumishi na uaminifu wao katika kuhudhuria mikutano. Taja hasa sehemu ambazo wamefanya vizuri sana. Ulinganisho waweza kufanywa na utendaji wa miaka iliyopita ikiwa ripoti hizo zimo katika faili. Pia, taja sehemu ambazo maendeleo yanaweza kufanywa wakati wa mwaka wa utumishi wa 1993.
Wimbo 43 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 28
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Tangaza ni magazeti gani yanayopatikana ya kutumiwa katika utumishi wa shambani, na udokeze jambo moja au mawili ya kuzungumzia yanayopaswa kuwavutia wenyeji. Toa wonyesho wa jinsi magazeti ya sasa yanavyoweza kutolewa.
Dak. 15: “Ubatizo,” kitabu Kutoa Sababu, kurasa 321-5. Hotuba ya utangulizi ikitegemea “Fasili.” Toa wonyesho wa jinsi mzee anavyoweza kuzungumza na mtu ambaye anajizuia asibatizwe. Kazia habari katika ukurasa 321. Kazia umaana wa kujiweka wakfu na kuufananisha kwa ubatizo wa maji. Msemaji amalizia kwa kupitia kifupi habari juu ya ubatizo kwa roho takatifu, ubatizo wa wafu, na ubatizo kwa moto.
Dak. 15: Toa Magazeti Wakati wa Oktoba. Hotuba fupi ikikazia thamani ya Amkeni! na Mnara wa Mlinzi. Wahubiri wapaswa kusoma matoleo mapya bila kuchelewa ili wazungumze kwa shauku wanapoyatoa kwa wengine. Toa wonyesho wa jinsi mhubiri anaweza kutoa gazeti na apange kurudi na toleo linalofuata, hivyo akianzisha kwanza njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida.
Wimbo 48 na sala ya kumalizia.