Mikutano Ya Utumishi Kwa Oktoba
ANGALIA: Huduma ya Ufalme Yetu itaratibu Mkutano wa Utumishi kwa kila juma wakati wa pindi ya mkusanyiko. Makutaniko yaweza kufanya marekebisho kama inavyohitajiwa ili kuruhusu wakati wa kuhudhuria “Ufundishaji wa Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya halafu kuwe na pitio la dakika 30 kuhusu mambo makuu ya programu kwenye Mkutano wa Utumishi juma linalofuata. Pitio la siku baada ya siku la programu ya mkusanyiko wa wilaya lapasa kugawiwa mapema ndugu wawili au watatu wanaostahili ambao wataweza kukazia mambo ya kutokeza. Pitio hilo lililotayarishwa vizuri litasaidia kutaniko likumbuke mambo ya msingi ili wayatumie kibinafsi na shambani. Maelezo kutoka kwa wasikilizaji na mambo yaliyoonwa yanayosimuliwa yapaswa kuwa mafupi na kutokeza wazo kuu.
Juma Linaloanza Oktoba 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Dokeza njia ambazo magazeti ya karibuni yaweza kutumiwa katika eneo lenu. Kazia umaana wa kurudia wote ulioangushia magazeti kwa kusudi la kuanzisha njia za kupelekea watu magazeti. Wenye nyumba wanapothibitika kuwa wenye kupendezwa kikweli, maandikisho yaweza kutolewa.
Dak. 15: “Je! Wewe Hustahi Mahali Pako pa Ibada?” Hotuba ikitolewa na mzee inayotegemea makala katika Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 1993. Tumia habari ifae hali za kwenu. Ikiwa kuna tatizo hususa la kuzungumziwa, toa kwa busara shauri linalofaa.
Dak. 20: Ongeza Huduma Yako ya Nyumba kwa Nyumba Wakati wa Oktoba. Mwangalizi wa utumishi au ndugu mwingine anayestahili azungumza na wasikilizaji juu ya umaana wa huduma ya nyumba kwa nyumba. Toleo la fasihi lenye utumizi mwingi la Oktoba laruhusu kuwe na unamna-namna mwingi wa utoaji. Onyesha: (1) Mhubiri aanzisha mazungumzo yatakayoongoza kwenye makala katika Amkeni! au Mnara wa Mlinzi. Ikitegemea kupendezwa kunakoonyeshwa na mwenye nyumba, mhubiri aweza kutoa magazeti ya karibuni zaidi au ampe mtu trakti. (2) Mhubiri aanzisha mazungumzo akiwa na wazo la kuelekeza kwenye kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kumtafuta Mungu. Kulingana na hali, mhubiri aweza kutoa kitabu au aamue kutoa magazeti mawili. (3) Mhubiri atumia trakti ili kuanzisha mazungumzo ya kivivi-hivi halafu atoa magazeti ya karibuni kwa mtu huyo aliyependezwa. (4) Mhubiri akimzuru mtu anayepelekea magazeti kwa ukawaida aamua kutoa uandikisho. Njia hizo mbalimbali zapasa ziwatie moyo wahubiri wote waongeze huduma yao ya nyumba kwa nyumba wakati wa Oktoba. Bila shaka baadhi ya wale walio kutanikoni watakuwa wakitumikia wakiwa mapainia wasaidizi mwezi huu. Huenda isiwe kuchelewa mno kwa wale wanaoweza kufanya hivyo kuweza kujiandikisha.
Wimbo 42 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Soma shukrani kwa ajili ya michango, na upongeze kutaniko kwa kutegemeza kwa ukarimu kazi ya ulimwenguni pote kutia na kutunza mahitaji ya kimwili ya kutaniko lenu. Pitia kifupi mipango ya utumishi wa shambani kwa ajili ya juma, na utoe shukrani kwa utegemezo wa bidii wa wahubiri.
Dak. 15: “Kutumia Magazeti Yetu Nyumba kwa Nyumba.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Tuna sababu nzuri ya kuwa wenye idili katika kutoa magazeti hayo kwa watu tunaokuta katika utumishi wa shambani na wale tunaotolea ushahidi kivivi-hivi. Ingawa magazeti yana tarehe na matoleo ya karibuni zaidi yapasa kutolewa siku ya magazeti, hatuhitaji kusita kutoa magazeti ya zamani zaidi wakati pindi inaporuhusu. Hakikisha tu kwamba magazeti hayo unayotoa ni safi na hayajaharibika. Mhubiri anayestahili atoe wonyesho wa utoaji ulioonyeshwa katika fungu la 4.
Dak. 20: “Nufaika Kabisa kwa ‘Ufundishaji wa Kimungu’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1993.”—Sehemu ya 1. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji wa mafungu 1-16. Wahubiri wapaswa wazungumze mambo yanayofaa pamoja na wanafunzi wao wa Biblia watakaohudhuria mkusanyiko.
Wimbo 44 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 18
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 10: “Kuonyesha Hali ya Kutopendelea Katika Huduma Yetu.” Maswali na majibu. Kazia mambo katika habari hii ambayo hasa yahangaisha katika eneo la kwenu.
Dak. 15: “Toa Uangalifu kwa Kupendezwa Kunakopatikana.” Hotuba, maswali fulani yakielekezwa kwa wasikilizaji. Onyesha jinsi wahubiri wamesitawisha kupendezwa katika eneo la kwenu, au mhubiri asimulie ono la hivi karibuni linaloonyesha thamani ya kurudia wale waliokubali nakala moja-moja za Amkeni! na Mnara wa Mlinzi.
Dak. 15: “Nufaika Kabisa kwa ‘Ufundishaji wa Kimungu’ Mkusanyiko wa Wilaya”—Sehemu ya 2. Zungumza pamoja na wasikilizaji mafungu 17-19 na mpitie kwa uangalifu “Vikumbusha vya Mkusanyiko wa Wilaya.” Tia ndani vikumbusha vinavyofaa vinavyotegemea habari katika Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 1989, kurasa 10-20, au tia moyo vikundi vya familia vipitie habari katika makala hizo kabla ya kuhudhuria mkusanyiko.
Wimbo 60 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia ndani mipango ya utumishi wa shambani ya juma, na uelekeze fikira kwenye mambo katika magazeti ya karibuni ambayo wahubiri waweza kutumia katika utumishi wa shambani katika siku zilizo mbele. Ikiwa wakati waruhusu, onyesha kifupi onyesho moja au mawili ambayo yangefaa eneo la kwenu. Toa vikumbusha juu ya uhitaji wa kurudia wote ambao wameonyesha kupendezwa.
Dak. 15: Uwe Tayari Kuwafariji Wale Wanaoomboleza (ikitegemea kurasa 104-6 za kitabu Kutoa Sababu). (Dak. 3) Ndugu anayeshughulikia sehemu hii aonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova hawakatai desturi zote zinazohusiana na kifo. (Dak. 5) Onyesha jinsi Shahidi angeweza kumweleza mfanyakazi mwenzake sababu inayofanya Mashahidi wa Yehova waepuke desturi fulani za kimapokeo za kuwaomboleza wafu, ukitegemeza mazungumzo kwenye rs-SW kurasa 104-5. (Dak. 7) Zungumza na wasikilizaji sehemu chini ya “Mtu Akisema—” kwenye kurasa 105-6.
Dak. 20: “Kuongoza Funzo la Biblia Nyumbani.” Pitio la makala kwa maswali na majibu. Toa wonyesho uliotayarishwa vizuri wa mhubiri akisaidia mwanafunzi kuelewa jinsi andiko lililoonyeshwa linavyounga mkono habari katika fungu linalozungumziwa. Katika onyesho hilohilo mhubiri atumia maswali ya ziada ili kusaidia mwanafunzi afanye kweli iwe yake mwenyewe. Tumia sehemu iliyoteuliwa ya kitabu Wenye Umoja Katika Ibada au Kuishi Milele.
Wimbo 78 na sala ya kumalizia.