Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/95 kur. 3-4
  • Kujitolea Wenyewe kwa Hiari kwa Kila Kazi Njema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujitolea Wenyewe kwa Hiari kwa Kila Kazi Njema
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Kujitoa kwa Hiari
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • “Kutafuta Kwanza Ufalme”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Njia za Kupanua Huduma Yako
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Ile Roho Ambayo Yehova Hubariki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 8/95 kur. 3-4

Kujitolea Wenyewe kwa Hiari kwa Kila Kazi Njema

1 Kichapo cha kilimwengu kilitoa taarifa hii kuhusu Mashahidi wa Yehova, ikisema: “Ingekuwa vigumu kupata washiriki wa kikundi chochote kile ambao hufanya kazi kwa bidii kwenye dini yao kama wafanyavyo Mashahidi.” Kwa nini Mashahidi wa Yehova hufanya kazi kwa bidii sana wakiwa na roho ya hiari hivyo?

2 Sababu moja ni kuwa wao huchochewa na roho ya uharaka. Yesu alitambua kwamba alikuwa na wakati mchache wa kumaliza kazi yake duniani. (Yn. 9:4) Wakati Mwana wa Mungu aliyetukuzwa anaendelea kutiisha katikati ya adui zake leo, watu wa Yehova wanatambua kwamba wana wakati mchache wa kufanya kazi yao. Kwa hiyo, wanaendelea kujitoa wenyewe kwa hiari kwa ajili ya utumishi mtakatifu. (Zab. 110:1-3) Kukiwa na wafanyakazi wengi wanaohitajiwa kuleta mavuno, hawawezi kuacha jitihada zao. (Mt. 9:37, 38) Hivyo, wanajitahidi kumwiga Yesu, aliyeweka kielelezo kikamilifu cha hiari na bidii katika kazi yake.—Yn. 5:17.

3 Sababu nyingine ambayo Mashahidi wa Yehova hufanya kazi kwa nafsi yote kana kwamba kwa Yehova ni kwamba tengenezo lao la ulimwenguni pote ni tofauti na vikundi vinginevyo vyote. Mashirika ya kilimwengu ya kidini kwa kawaida hutaka wakati na jitihada ndogo tu kutoka kwa wafuasi wayo. Wanayoamini yana matokeo machache au hayana matokeo katika maisha yao ya kila siku, kushughulika kwao wao kwa wao, au ufuatiaji wao maishani. Wakikosa nguvu yenye kuchochea ya imani ya kweli, wamesisitiza kwamba wachungaji wao ‘wawaambie maneno laini,’ wakiwahakikishia kwamba jitihada yao yatosha. (Isa. 30:10) Makasisi wao wamewafanyia mema kwa ‘kutekenya masikio yao,’ wakiingiza roho ya ubaridi na uvivu wa kiroho.—2 Tim. 4:3, NW.

4 Kuna tofauti kama nini miongoni mwa watu wa Yehova! Kila kitu katika ibada yetu hutia ndani jitihada, kujikakamua, na kazi. Kila siku katika kila kitu tufanyacho, sisi hufanya yale tunayoamini. Kweli inapotuletea shangwe nyingi, hiyo huhusisha “kuishindania sana” ili tutimize inalohitaji. (Linganisha 1 Wathesalonike 2:2.) Kuangalia madaraka ya kila siku tu kunatosha kufanya watu walio wengi kuwa wenye shughuli. Hata hivyo, haturuhusu mahangaikio haya yatuzuie kuweka masilahi za Ufalme kwanza.—Mt. 6:33.

5 Tunayopewa kufanya katika utumishi wa Yehova ni yenye manufaa na ya uharaka hivi kwamba twachochewa ‘kukomboa’ wakati kutoka ufuatiaji mwingine na kuutumia kwa faida zaidi kwa mambo ya kiroho. (Efe. 5:16) Kujua kwamba ujitoaji wetu na roho yetu ya hiari humpendeza Yehova, tuna kichocheo kikubwa zaidi cha kuendelea na kazi yetu ngumu. Tukiwa na baraka tele tunazopokea sasa na matazamio ya uhai ulio mbele, azimio letu ni kuendelea ‘kujitaabisha na kujitahidi’ kwa ajili ya masilahi za Ufalme.—1 Tim. 4:10.

6 Ujitoaji na Roho ya Kujidhabihu: Watu wengi leo huyapa nafasi ya kwanza mahitaji na masilahi za kimwili kuliko chochote kile. Wao huhisi wakiwa wametosheka kabisa wakitoa uangalifu kwa yale watakayokula, kunywa, au kuvaa. (Mt. 6:31) Wakiwa hawatosheki na mambo ya lazima, wanachochewa na mradi wa kufurahia kuishi kuzuri vya kutosha sasa na ‘wakiwa na vitu vyema vingi walivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; basi wanaweza kupumzika, kula, kunywa, na kufurahi.’ (Luka 12:19) Mwenda-kanisani wa kawaida huhisi kwamba jitihada yoyote ya kibinafsi inayohitajiwa upande wake na dini yake inavuka mipaka ya haki zake. Wazo la kuacha au hata kupunguza ufuatiaji wa kimwili kadhaa au kuacha upendezi wenye kuvutia ni jambo lenye kuchukiza. Akiwa na kufikiri kwake kwenye ubinafsi, kusitawisha roho ya kujidhabihu si jambo halisi, halifai.

7 Sisi huona jambo hili kwa njia tofauti. Neno la Mungu limechochea kufikiri kwetu hivi kwamba twafikiri mawazo ya Mungu badala ya yale ya wanadamu. (Isa. 55:8, 9) Tuna miradi maishani inayopita ufuatiaji wa kimwili. Kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova na kutakaswa kwa jina lake ni masuala muhimu zaidi katika ulimwengu mzima. Umuhimu wa masuala haya ni mkubwa hivi kwamba, kwa kulinganishwa, mataifa yote “huwa kama si kitu mbele zake.” (Isa. 40:17) Jaribio lolote la kuishi maisha zetu katika njia inayopuuza mapenzi ya Mungu lazima lionwe kuwa upumbavu.—1 Kor. 3:19.

8 Kwa hiyo ijapokuwa vitu vingine vya kimwili vyahitajiwa na vingine vyafaa katika kutimiza utendaji wetu wa Ufalme, twatambua kwamba hivi kwa kweli si ‘vitu vya maana zaidi.’ (Flp. 1:10, NW) Twashikamana na roho ya 1 Timotheo 6:8 kwa kuwekea mipaka ufuatiaji wetu wa mambo ya kimwili na kujitahidi kwa hekima kuendeleza mioyo yetu ikiwa imekazia ‘visivyoonekana ambavyo ni vya milele.’—2 Kor. 4:18.

9 Kadiri tufikirivyo mawazo ya Mungu, ndivyo tulivyo na mahangaikio machache kuhusu vitu vya kimwili. Tunapotafakari yale Yehova ametufanyia tayari na baraka za ajabu ambazo ameahidi kwa wakati ujao, tuko tayari kufanya dhabihu zozote anazotutaka. (Mk. 10:29, 30) Twadaiwa kuishi kwetu na yeye. Kama si kwa sababu ya huruma zake na upendo wake, hatungefurahia maisha sasa na wakati ujao wowote. Twahisi tukiwa na wajibu wa kujitoa wenyewe, kwa kuwa kila kitu tufanyacho katika utumishi wake ni ‘yale tu yanayotupasa kuwa tukifanya.’ (Luka 17:10) Chochote tunachoombwa tumrudishie Yehova, twatoa kwa uchangamfu, tukijua kwamba ‘tutavuna kwa ukarimu.’—2 Kor. 9:6, 7.

10 Wafanyakazi wa Hiari Wahitajiwa Sasa: Kuanzia mwanzo walo, kutaniko la Kikristo liliingia katika kipindi cha utendaji mwingi. Ushahidi kamili ulihitaji kutolewa kabla ya kupinduliwa kwa Yerusalemu mwaka wa 70 W.K. Wakati huo wanafunzi wa Yesu walikuwa ‘wamesongwa sana na lile neno.’ (Mdo. 18:5) Upanuzi wa haraka ulifanya iwe lazima kuzoeza waeneza-evanjeli zaidi na wachungaji wenye ustadi na kutumia msaada wao. Wanaume walio na maarifa ya kushughulika na mamlaka za kilimwengu na vilevile wenye ustahili wanaoweza kusimamia ukusanyaji na ugawaji wa vitu vya kimwili walihitajiwa. (Mdo. 6:1-6; Efe. 4:11) Ijapokuwa wachache walitumikia wakitokeza sana, wengine wao walibaki bila kutokeza sana. Lakini wote ‘walijitahidi,’ wakifanya kazi pamoja kwa moyo wote ili watimize kazi.—Luka 13:24.

11 Ingawa kulikuwa na uhitaji mdogo wa kujitahidi zaidi kwa kulinganisha kuhusu kiwango cha ulimwengu wote wakati wa karne nyingi zilizofuata, kuhuishwa kwa kiwango kikubwa kwa utendaji wa Ufalme kulianza Yesu alipotwaa mamlaka katika Ufalme wake mwaka wa 1914. Mwanzoni, wachache walitambua uhitaji wa wafanyakazi kwa niaba ya masilahi za Ufalme ungekuwa mkubwa zaidi, ukihitaji msaada wa mamilioni ya watu wenye hiari katika nchi kuzunguka tufe lote.

12 Leo tengenezo limejiingiza kindani katika miradi mbalimbali inayotaka zaidi raslimali zetu hadi kilele chazo. Utendaji wa Ufalme unasonga mbele kwa kasi sana. Uharaka wa nyakati zetu watuchochea tujitahidi kwelikweli na kutumia kila upande tulio nao ili tutimize kazi inayohitaji kufanywa. Mwisho wa mfumo wote mbovu wa mambo ukaribiapo zaidi, twatazamia hata zaidi utendaji mwingi katika siku za usoni. Kila mtumishi wa Yehova aliyejiweka wakfu anaombwa ajitolee mwenyewe kwa hiari katika kazi ya kukusanya yenye uharaka.

13 Ni Nini Linalohitaji Kufanywa? Twaweza kusema kikweli kwamba kuna ‘mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.’ (1 Kor. 15:58, NW) Katika maeneo mengi mavuno yameiva, bali wafanyakazi ni wachache. Twaalikwa kufanya sehemu yetu si kwa kutenda kikamili tu kupitia eneo letu wenyewe bali pia kukabiliana na ugumu wa kutumikia palipo na uhitaji mkubwa zaidi.

14 Ni jambo lenye kupongezwa kuona jinsi Mashahidi katika sehemu zote za ulimwengu wanajitolea wenyewe kwa hiari kwa utendaji mwingineo. Huenda ni kuanzia kujitolea katika ujenzi wa mahali pa ibada, kutumikia kwenye mikusanyiko, na kusaidia katika jitihada za kupunguza shida wakati wa msiba hadi kusafisha Jumba la Ufalme la mahali penu kwa ukawaida. Kuhusiana na utendaji huo wa mwisho, kuna jambo la kuhakikisha sikuzote kwamba Jumba la Ufalme laachwa likiwa safi na katika hali yenye utaratibu baada ya kila mkutano. Kutimiza kazi zinazoweza kuonekana kuwa za hali ya chini kwaonyesha uelewevu unaofaa wa maneno ya Yesu kwenye Luka 16:10: “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.”

■ Kuunga Mkono Utendaji wa Kutaniko: Ijapokuwa kila kutaniko hutenda likiwa sehemu ya tengenezo lote na hupokea mwelekezo kutoka “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” limefanyizwa kwa wahubiri wa Ufalme mmoja-mmoja. (Mt. 24:45) Matimizo yalo hutegemea zaidi jinsi kila Shahidi alivyo tayari na awezayo kufanya. Kutaniko hukazia kuhubiriwa kwa habari njema katika eneo lalo, kufanya wanafunzi wapya, kisha kuwaimarisha kiroho. Kila mmoja wetu aweza kushiriki kazi hii. Pia twaweza kujiwekea miradi wenyewe katika funzo la kibinafsi, ushiriki wenye maana katika mikutano, na kusaidia wengine walio na uhitaji katika kutaniko. Utendaji huu hutoa fursa nyingi nzuri kwetu ili kuonyesha hiari yetu.

■ Kuchukua Uongozi kwa Upande wa Wale Walio na Wadhifa wa Uangalizi: Yehova amekabidhi usimamizi wa kila kutaniko kwa wazee walioteuliwa. (Mdo. 20:28) Hawa ni wanaume ambao wamestahili ili kupata pendeleo hili. (1 Tim. 3:1) Karibu kila ndugu katika kutaniko ana uwezekano wa kustahili madaraka mazito. Ndugu wengi wanasitawi kiroho na wanahitaji kuendelea kukua wakiwa chini ya mwongozo na msaada wenye upendo wa wazee wa kutaniko. Wanaume hawa wapaswa kuwa wanafunzi wenye bidii wa Biblia na vichapo vyetu. Wanaweza kuonyesha hiari yao kwa kuwa watiifu kwa wazee walioteuliwa kwa roho, wakiiga imani yao, na kusitawisha sifa zinazoangaliwa kwa waangalizi.—Ebr. 13:7, 17.

■ Kuchukua Utumishi wa Wakati Wote: Kutaniko hutenda hasa kwa kuhubiri habari njema. (Mt. 24:14) Loo! ni baraka kama nini wenye bidii wanapozidisha jitihada zao kwa kujiandikisha wawe mapainia! Hili kwa kawaida huhusisha kufanya marekebisho katika maisha yao binafsi. Marekebisho ya ziada huenda yakahitajiwa ili waendelee katika upande huu wa pekee wa utumishi. Lakini wale ambao hushikilia pendeleo hili badala ya kuacha baada ya mwaka mmoja hivi kwa sababu ya kivunja-moyo cha muda tu wanahakikishiwa kupata baraka tele za Yehova. Wazee wenye upendo na wengine walio wakomavu wanaweza kuongezea mafanikio ya mapainia, kuwatia moyo kwa neno na tendo. Ni roho nzuri wee, kama nini inayoonyeshwa na vijana wanaoelekea moja kwa moja katika kazi ya upainia baada ya kumaliza shule! Jambo hilo ni sawa kwa watu wazima wanaojiandikisha kuwa mapainia wa kawaida mara baada ya kazi zao za kimwili kupunguka. Inaridhisha kama nini kwa Mkristo aliyejiweka wakfu anaposhiriki kuhimiza kwa Yehova kazi ya ukusanyaji!—Isa. 60:22.

■ Kushiriki Katika Ujenzi na Utunzi wa Mahali pa Kukutania: Kwa kweli mamia ya Majumba ya Ufalme ya kisasa vilevile na Majumba ya Mkusanyiko yamejengwa. Kwa kushangaza, karibu kazi yote imefanywa na ndugu na dada zetu ambao wametoa kwa hiari wakati wao na stadi zao. (1 Nya. 28:21) Maelfu ya wafanyakazi wenye hiari wanaendeleza majengo haya katika hali nzuri kwa kufanya kazi zozote ambazo huenda zikahitajiwa. (2 Nya. 34:8) Kwa kuwa kazi hii ni upande mmoja wa utumishi mtakatifu, wale wanaosaidia wanajitoa wenyewe kwa hiari, bila kuomba malipo ya utumishi wao kuhusu jambo hili, kama vile tu wasivyoomba walipwe kuhubiri nyumba kwa nyumba, kutoa hotuba za watu wote katika kutaniko, au kusaidia katika kazi ya mkusanyiko au kusanyiko. Wajitoleaji hawa hutoa huduma zao bila malipo kwa kutayarisha na kujenga mahali pa ibada kwa sifa ya Yehova. Wao wanasaidia kwa hamu mambo kama vile kushughulikia hati za kisheria, kuweka rekodi za hesabu, kushughulikia mahusiano ya ununuzi, na kuhesabu kiwango cha vyombo vinavyohitajiwa. Watumishi hawa waaminifu washikamanifu wa Yehova hawaongezi gharama za kibiashara au kwa njia yoyote ile kutafuta kufaidika kimwili kwa njia ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja kutokana na huduma wanazotoa, kwa kuwa vipawa vyao vyote na raslimali vimewekwa wakfu kwa Yehova. Utendaji huu wahitaji wafanyakazi wenye bidii wanaofanya utumishi wao ‘kwa [“nafsi yote,” NW] kama kwa Yehova.’—Kol. 3:23.

15 Ni nini basi, hufanya hiari ya watu wa Yehova kuwa isiyo na kifani? Ni ile roho ya kutoa. Kutoa kwao kwa ukarimu hutia ndani mengi kuliko fedha au vitu vya kimwili—‘wanajitoa wenyewe kwa hiari.’ (Zab. 110:3) Hiki ndicho kiini cha ujitoaji wetu kwa Yehova. Twathawabishwa kwa njia ya pekee. Twaona ‘furaha nyingi sana’ na “kuvuna kwa ukarimu” kwa sababu tunayofanya yanathaminiwa na wengine, ambao wanatupatia pia. (Mdo 20:35; 2 Kor. 9:6; Luka 6:38) Mfadhili wetu mkubwa zaidi ni Baba yetu wa kimbingu, Yehova, ambaye “humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.” (2 Kor. 9:7) Yeye atatulipa mara mia, pamoja na baraka zitakazodumu milele. (Mal. 3:10; Rum. 6:23) Kwa hiyo unapopewa mapendeleo ya utumishi wa Yehova, je, utajitolea kwa hiari na kujibu kama alivyojibu Isaya: “Mimi hapa, nitume mimi.”?—Isa. 6:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki