Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/96 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Julai

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Julai
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Julai 1
  • Juma Linaloanza Julai 8
  • Juma Linaloanza Julai 15
  • Juma Linaloanza Julai 22
  • Juma Linaloanza Julai 29
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 7/96 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Julai

Juma Linaloanza Julai 1

Wimbo 90

Dak 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Toa maelezo juu ya ripoti ya utumishi ya Aprili ya kutaniko la kwenu.

Dak 15: “Kutimiza Nadhiri Yetu Siku kwa Siku.” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo kutoka Insight, Buku la 2, ukurasa 1162, mafungu 6-7, kuonyesha jinsi nadhiri ilivyo wajibu mzito.

Dak 18: “Mwige Yehova kwa Kujali Wengine Kikweli.” (Mafungu 1-3) Tumia fungu la kwanza kusitawisha kichwa cha makala hiyo. Chunguza ni broshua gani zilizopo akibani katika kutaniko wakati huu zinazoweza kuamsha kupendezwa katika eneo lenu. Kisha pitia mafungu 2-3 pekee, na uonyeshe jinsi ziara ya kwanza na ya kurudia iwezavyo kushughulikiwa kwa kutumia broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? Onyesha jinsi watangazaji wanavyoweza kufanya utoaji wao wenyewe wa broshua nyingine itakayofaa eneo la kwenu.

Wimbo 112 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 8

Wimbo 43

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak 15: “Mwige Yehova kwa Kujali Wengine Kikweli.” (Mafungu 4-5) Zungumzia mafungu 4-5 tu na mambo makuu kadhaa ya broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Kisha utoe wonyesho wa utoaji mbalimbali uliodokezwa kwa ziara ya kwanza na ya kurudia.

Dak 20: “Je, Umejaribu Kutoa Ushahidi Katika Maeneo Yasiyogawiwa Mtu?” Hotuba kukiwa na ushiriki wa wasikilizaji. Tia ndani mambo yaliyoonwa yaonyeshayo matokeo chanya kutokana na kutoa ushahidi katika maeneo yasiyogawiwa mtu. Eleza ratiba ya kwenu ya kuhubiri maeneo ya mbali.

Wimbo 16 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 15

Wimbo 162

Dak 10: Matangazo ya kwenu.

Dak 20: “Ndugu Zaidi Wanahitajiwa Katika Utumishi wa Painia.” Maswali na majibu. Wakati ukiruhusu, pitia madokezo ya jinsi ya kushughulika na mahitaji ya fedha, kama ilivyozungumziwa katika Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 1993, kurasa 28-31.

Dak 15: “Mwige Yehova kwa Kujali Wengine Kikweli.” (Mafungu 6-8) Tumia fungu la mwisho la makala hiyo kutia wote moyo wafanye ziara za kurudia haraka kwa wale ambao waliangushiwa broshua. Ukitumia mafungu 6-7, toa wonyesho wa jinsi ya kutoa broshua Kusudi La Uhai kwenye ziara ya kwanza na jinsi ya kuanzisha funzo katika sura ya kwanza ya kitabu Ujuzi kwenye ziara ya kurudia. Kumbusha watangazaji kwamba wanaweza kufanyiza utoaji mbalimbali wao wenyewe wa broshua hizo, wakifuata kigezo cha utoaji mbalimbali uliodokezwa katika Huduma ya Ufalme Yetu.

Wimbo 64 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 22

Wimbo 108

Dak 10: Matangazo ya kwenu.

Dak 15: Fuatia Mradi wa Utumishi wa Wakati Wote. Mazungumzo kati ya mzee na tineja mmoja au wawili, yakitegemea Mnara wa Mlinzi, Desemba 15, 1988, kurasa 25-27. Vijana wanajaribu kuamua ni miradi gani watakayofuatia baada ya kumaliza shule ya sekondari. Wanaonyesha kupendezwa katika mambo ya kimwili yanayotolewa na kazi-maisha za kilimwengu. Mzee aonyesha sababu nzuri kwa nini ingefaa kuweka mradi kufikia utumishi wa painia. Matineja wakubali lakini wanatia shaka kama wanaweza kupainia na kujiandalia kimwili. Mzee ashiriki mambo yaliyoonwa kutoka makala ya Mnara wa Mlinzi, kuonyesha kwamba utumishi wa painia ni mradi ufaao, uwezao kufikiwa ambao huletea wengine shangwe. Mazungumzo yamalizika matineja hao wakionyesha uthamini kwa maelezo ya mzee na nia yao ya kufikiria kwa uzito kufuatia mradi wa kuwa na ushiriki kamili katika utumishi wa Ufalme.

Dak 20: “Jinsi ya Kufanya Wanafunzi Ukitumia Kitabu Ujuzi.” Hotuba inayoshughulikia mafungu 12-16 ya nyongeza ya Juni 1996. Tia ndani maonyesho mawili ya funzo la Biblia linaloongozwa. La kwanza laonyesha jinsi ya kuzoeza mwanafuzi kutayarisha somo kwa kutia alama au kupiga mstari maneno na semi za maana ambazo hujibu moja kwa moja maswali yaliyochapishwa. La pili laonyesha unaloweza kusema ili kumtia moyo mwanafunzi huyo wa Biblia ahudhurie Mkutano wa Watu Wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi.

Wimbo 116 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 29

Wimbo 212

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Pitia kifupi matoleo ya karibuni ya magazeti, ukionyesha mambo makuu yenye kupendeza ambayo huenda yakatumiwa kuyatoa mlangoni.

Dak 20: Ni Nini Kiwezacho Kumsaidia Mtu Kupata Funzo la Biblia? Mzee aongoza mazungumzo kati ya watu wawili au watatu ambao wamepata mafanikio katika kazi ya funzo la Biblia, wakipitia njia za kuwa wenye mafanikio zaidi katika kuanzisha mafunzo: (1) Sali ili kupata msaada wa Yehova. (2) Shiriki kwa ukawaida katika sehemu mbalimbali za huduma ili kutafuta watu wenye kupendezwa. (3) Andika majina ya watu wote wenye kupendezwa, na ufanye ziara za kurudia mara moja. (4) Sikuzote toa funzo kupendezwa kuonyeshwapo. (Ona kichwa kidogo “Kuanzisha Mafunzo ya Biblia,” kwenye ukurasa 20 wa Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1996.) (5) Uwe na uhakika katika uwezo wako wa kufundisha kwa kutumia madokezo manne yaliyoorodheshwa kwenye kurasa 16-21 za Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1985.

Dak 15: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee. Zungumzia sababu zinazotusukuma kuwa wakarimu, kama ionyeshwavyo katika Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1992, kurasa 16-17.

Wimbo 165 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki