Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/97 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Agosti 4
  • Juma Linaloanza Agosti 11
  • Juma Linaloanza Agosti 18
  • Juma Linaloanza Agosti 25
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 8/97 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti

Juma Linaloanza Agosti 4

Wimbo 16

Dak. 7: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Toa maelezo kuhusu ripoti ya utumishi wa shambani ya Aprili ya nchi na ya kutaniko la kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 13: “Mikutano Huchochea Kwenye Kazi Zilizo Bora.” Maswali na majibu. Onyesha manufaa za mazungumzo yenye kujenga kabla na baada ya mikutano.—Ona kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 82, fungu la 17-18.

Dak. 25: “Mtegemee Yehova Akuze Vitu.” Hotuba na maonyesho. Kazia uhitaji wa kufanya ziara za kurudia mahali ambapo broshua ziliangushwa. Panga kuwe na maonyesho mawili yaliyotayarishwa vizuri kuonyesha jinsi ya kuanzisha mafunzo. Tia ndani madokezo kutoka nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Machi 1997, fungu la 7-11.

Wimbo 78 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 11

Wimbo 20

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: “Mlio Wazee-Wazee Hubirini Bila Kuacha.” Maswali na majibu. Tia ndani jambo lililoonwa kuhusu nyanya mzee-mzee ambaye alifanya upainia-msaidizi, katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 1988, ukurasa wa 13.

Dak. 20: “Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Katika Afrika Mashariki.” Maswali na majibu.

Wimbo 71 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 18

Wimbo 14

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.”

Dak. 10: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 25: Fanya Ziara za Kurudia, Ukitumia Broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Onyesha jinsi ya kutokeza swali na kurejezea jibu kwenye broshua hiyo. Kwa mfano, broshua hiyo hujibu maswali yafuatayo: Je, kuna tumaini lolote kwa wafu? (Ukurasa wa 5-6) Je, kuna ubaya wowote kuhuzunika? (Ukurasa wa 8-9) Mtu anaweza kukabilianaje na huzuni? (Ukurasa wa 18) Wengine wanaweza kusaidiaje? (Ukurasa wa 20-23) Watoto wanaweza kusaidiwaje waelewe kifo? (Ukurasa wa 25) Biblia hutoa faraja gani? (Ukurasa wa 27) Kisha, zungumza kifupi na wahubiri wawili wenye uwezo jinsi ambavyo wametumia broshua hii kwenye ziara za kurudia, ili kujibu maswali yanayoulizwa mara nyingi kuhusu kifo. Toa wonyesho wa jinsi ya kutumia broshua hiyo unapofanya ziara ya kurudia.

Wimbo 94 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 25

Wimbo 23

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote walete ripoti za utumishi wa shambani. Tangaza mipango ya utumishi ya mwisho-juma.

Dak. 15: Hotuba itolewe na mzee yenye kutegemea Mnara wa Mlinzi la Machi 15, 1997 ukurasa wa 18-22 ikitia moyo akina ndugu kuonyesha ufahamu katika mambo ya kibiashara. Kazia kwamba mambo ya kibiashara yasizungumziwe kwenye Jumba la Ufalme au mahali pengine pa mikutano. Kumbusha akina ndugu hekima ya kuandika mambo.

Dak. 20: Hubiri Ukiwa na Kusudi. Mzee na mtumishi wa huduma mmoja au wawili wapitia kitabu Huduma Yetu, kwenye ukurasa wa 8-12. Kazia fikira sababu zenye kushurutisha zinazotufanya tudumishe mtazamo unaofaa, mtazamo wenye maendeleo kuelekea huduma yetu na sikuzote tushirikiane kwa ukaribu na tengenezo.

Wimbo 100 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki