Habari Za Kitheokrasi
Liberia: Ofisi ya tawi katika Monrovia ilifunguliwa tena katika Septemba 1, baada ya kufungwa kwa miezi 15 kwa sababu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe. Waliripoti kilele kipya cha wakati wote cha wahubiri 1,977 katika Septemba.
Msumbiji: Kilele kipya cha wahubiri 28,005 kilifikiwa katika Septemba. Kilele cha zamani kilikuwa 25,790 katika Mei 1975, kwa hiyo hii ni hatua kubwa katika historia ya kitheokrasi ya Msumbiji.
Nepali: Kilele kipya cha wahubiri 306 kilifikiwa katika Septemba. Mafunzo ya Biblia yapatayo 500 yanaongozwa kwa sasa.
St. Helena: Watu katika kila nyumba kwenye kisiwa hiki walipewa nakala ya trakti Habari za Ufalme Na. 35.
Nchi kadhaa zilianza mwaka wa utumishi kwa vilele vipya vya wahubiri kufikia maongezeko ya asilimia 5 kuliko wastani wa mwaka uliopita: Hong Kong, 4,230; Madagaska, 8,749 (kutia ndani kilele cha mapainia wa kawaida 912); Taiwan, 3,497.