Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/02 uku. 4
  • Shangwe za Utumishi wa Wakati Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shangwe za Utumishi wa Wakati Wote
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Utumishi wa Painia—Je, Wakufaa Wewe?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Umewawekea Watoto Wako Miradi Gani?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Ndugu Zaidi Wanahitajiwa Katika Utumishi wa Painia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kutembea kwa Nafsi Yote katika Njia ya Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 4/02 uku. 4

Shangwe za Utumishi wa Wakati Wote

1 Ukiwa kijana, bila shaka umefikiria kuhusu wakati wako ujao. Mithali 21:5 hutuambia kwamba “mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu.” Itakufaidi ukichunguza kwa uzito miradi yako maishani. Unapofanya mipango yako ya wakati ujao, fikiria kuhusu utumishi wa wakati wote. Kwa nini?

2 Uliza watu wazima ambao walifanya upainia walipokuwa vijana wakuambie maoni yao, na mara nyingi watasema sababu ileile: “Hiyo ndiyo iliyokuwa miaka bora zaidi maishani mwangu!” Ndugu mmoja ambaye alipata shangwe za utumishi wa wakati wote tangu ujana wake alisema hivi baadaye: “Inaridhisha kufikiria siku za ujanani na kuweza kusema kwamba nimetii shauri lenye hekima: ‘Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako.’” (Mhu. 12:1) Wewe na wazazi wako mwahitaji kufanya mipango mizuri sasa, ili ufurahie jambo hili ujanani.

3 Wazazi, Wachocheeni Wafanye Utumishi wa Wakati Wote: Yehova ni Baba mwenye kujali, naye hukuonyesha hasa njia unayopaswa kufuata. (Isa. 30:21) Kwa kutoa mwongozo huo wenye upendo, yeye huwawekea nyinyi wazazi Wakristo kielelezo bora. Badala ya kuwaachia watoto wenu wenyewe wachague njia inayowapendeza, wazoezeni kwa hekima njia watakayofuata ili wapate baraka za Yehova. Kisha watakapokuwa wakubwa, mazoezi yenu yatawasaidia “kutofautisha lililo sahihi na lililo kosa pia.” (Ebr. 5:14) Kutokana na mambo ambayo wamejionea, watu wazima wanajua kwamba hawawezi kuyategemea maoni yao wenyewe na ni lazima wamtegemee Yehova ili wanyoshe njia zao. (Mit. 3:5, 6) Jambo hilo lafaa zaidi hasa kwa vijana kwa kuwa hawana ujuzi mwingi maishani.

4 Enyi wazazi, watoto wenu wanapokaribia kuwa matineja, au hata kabla ya hapo, ongeeni nao kuhusu miradi yao ya kazi wanayotaka kufanya maishani. Washauri wa shule, walimu, na wanadarasa wenzao watajaribu kuwashawishi wachague kufuatia vitu vya kimwili vya ulimwengu. Saidieni watoto wenu wachague masomo ya shule yatakayowapa mazoezi yanayofaa, yakiwatayarisha kutunza mahitaji yao ya kimwili bila kupuuza masilahi ya Ufalme. (1 Tim. 6:6-11) Mara nyingi, elimu ya sekondari pamoja na mafunzo ya kazi huenda ndiyo yanayohitajiwa tu ili kutunza mahitaji yake ya lazima huku akianza huduma ya painia wa kawaida.

5 Tia moyo vijana wafuatie zawadi ya useja. Baadaye wakiamua kufunga ndoa, watakuwa tayari kutimiza madaraka mazito ya ndoa. (Ona fungu la 19 katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2001, “Je Waweza Kujitolea?”) Kwa kuongea vizuri kuhusu upainia, kutumikia mahali palipo na uhitaji mkubwa zaidi, utumishi wa Betheli, na utumishi wa mishonari, sitawisha ndani ya mioyo ya vijana tamaa ya kutumia maisha yao kwa njia inayompendeza Yehova, wakinufaisha wengine, na kujipatia shangwe.

6 Vijana, Wekeni Utumishi wa Wakati Wote Kwanza: Vijana, hamhitaji kujiuliza kazi ya upainia ikoje. Mnaweza kuijaribu kwa muda kwa kufanya upainia msaidizi ikiwezekana mkiwa shuleni na wakati wa likizo. Ndipo mtakapojua jinsi utumishi wa painia unavyoridhisha! Je, mwaweza kupangia kufanya upainia msaidizi kati ya wakati huu na mwisho wa mwaka huu wa utumishi?

7 Ikiwa wewe ni ndugu kijana katika tengenezo la Mungu, pia fikiria kwa uzito kufikia kustahili kuwa mtumishi wa huduma. (1 Tim. 3:8-10, 12) Kwa kuongezea, amua kama unataka kujiandikisha kwa ajili ya utumishi wa Betheli au kuhudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma unapofikia umri unaotakikana. Uzoefu wako katika huduma ya painia utakufundisha masomo yafaayo sana, kama vile jinsi ya kuishi kulingana na ratiba, jinsi ya kupanga mambo vizuri, jinsi ya kupatana na wengine, na jinsi ya kuchukua madaraka kwa uzito. Yote hayo yatakutayarisha kwa ajili ya mapendeleo makubwa zaidi ya utumishi baadaye.

8 Jambo la maana ili kufanikiwa katika utumishi wa wakati wote ni kuwa na roho ya bidii kwenye utumishi wa Mungu. Mtume Paulo alichochea mtazamo huo, na alionyesha baraka zinazotokana nao: “Lolote mnalofanya, lifanyeni kwa nafsi yote kama kwa Yehova, . . . kwa maana mwajua kwamba ni kutoka kwa Yehova nyinyi mtapokea thawabu ipasayo ya urithi.” (Kol. 3:23, 24) Yehova na akubariki kwa shangwe nyingi katika utumishi wa wakati wote!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki