Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Septemba 8
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Watie moyo wote warudie maandishi ya kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi uliopita wanapojitayarishia Mkutano wa Utumishi wa juma lijalo. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6, panga kuwe na maonyesho mawili halisi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 15 na Amkeni! la Agosti 22. Katika onyesho moja, mwanafunzi au mzazi amtolea mwalimu ushahidi.
Dak. 10: Barua Kutoka kwa Ofisi ya Tawi. Mazungumzo kati ya mhubiri wa muda mrefu, ikiwezekana mzee, na mhubiri kijana. Kijana amuuliza mhubiri huyo wa muda mrefu kama ameona barua kutoka kwa ofisi ya tawi katika Huduma Yetu ya Ufalme. Mhubiri huyo mwenye uzoefu anamwambia kwamba barua kutoka kwa ofisi ya tawi ilikuwa ikichapishwa kwa ukawaida katika Huduma Yetu ya Ufalme katika miaka ya 1960 na 1970. Kisha wanazungumzia na kukazia mambo makuu ya barua iliyo katika ukurasa wa kwanza.
Dak. 25: “Vijana—Wekeni Msingi Mzuri kwa Ajili ya Wakati Ujao.”a Ishughulikiwe na mzee, akitumia maswali yaliyo kwenye makala. Unapozungumzia fungu la 5, kazia shangwe na baraka za utumishi wa wakati wote.
Wimbo 170 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 10: “Kujifunza Kitabu Mwabudu Mungu.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa funzo la kitabu. Onyesha ratiba ya kujifunza. Unapozungumzia fungu la nne, tia ndani maelezo yaliyo katika kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 28, fungu la 1, na ukurasa wa 70.
Dak. 25: “Mtumaini Yehova Ukatende Mema.” (Zab. 37:3) Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea maswali yafuatayo yanayokazia mambo makuu ya programu ya kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi uliopita. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wametumia mambo hayo makuu maishani mwao au katika familia. Zungumzia sehemu hizi za programu: (1)“Kuonyesha Tunamtumaini Yehova.” Kwa nini ni muhimu kumtumaini Yehova katika shughuli zetu zote maishani? (it-2 uku. 521) Kitabu Watch Tower Publications Index kinaweza kutusaidiaje? (2) “Jihadharini na Mambo ya Ubatili.” (Mhu. 2:4-8, 11) Tunapaswa kujihadhari na mambo gani ya ubatili, na twawezaje kufanya hivyo? (3) “Epukeni Mabaya, Tendeni Mema.” Kwa nini ni muhimu kufuata kanuni za Yehova? (Isa. 5:20) Tunapaswa kujishughulisha na kazi zipi bora? (4) “Kudumisha Tumaini Letu Katika Yehova.” Ni nini kitakachotusaidia kusimama imara tunapokabili majaribu na vishawishi? Kwa nini tunahitaji kumwachia Yehova mambo fulani? (5) “Je, Utahesabiwa Kuwa Unastahili Ufalme wa Mungu?” (Kol. 1:10) Ni mifano gani katika Biblia inayotuchochea tuendelee kutembea kwa kumstahili Yehova? (6) “Tumaini Ahadi za Yehova.” Maisha yetu yatakuwaje tukifanya hivyo?
Wimbo 58 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6, panga kuwe na maonyesho mawili ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1 na Amkeni! la Septemba 8. Katika maonyesho hayo, mzee na mhubiri mgonjwa au mhubiri mwingine asiyeweza kutimiza mengi wahubiri barabarani.
Dak. 15: Tulitimiza Nini Mwaka Uliopita? Mwangalizi wa utumishi ataja mambo makuu ya ripoti ya kutaniko ya mwaka wa utumishi wa 2003. Pongeza kutaniko kwa mambo mazuri waliyotimiza. Zungumzia pia mambo yafaayo ya ripoti ya mwisho ya mwangalizi wa mzunguko. Taja mradi mmoja au miwili inayoweza kutimizwa mwaka ujao.
Dak. 20: Je, Dini Zote Zinakubalika kwa Mungu? Mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea kitabu Kutoa Sababu. Zungumzieni jinsi ya kumsadikisha mtu kuhusu jambo hilo. (rs uku. 67-68) Kazia njia kadhaa za kutambulisha dini ya kweli. (rs uku. 73-75) Huduma yetu huwasaidia wengine kuchagua ibada inayompendeza Mungu.—Kol. 1:9, 10.
Wimbo 39 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 29
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Septemba. Taja toleo la vichapo la Oktoba.
Dak. 22: “Iweni na Bidii Katika ‘Kutoa Ushahidi Kamili.’”b Tumia maswali yaliyo kwenye makala. Baada ya kuzungumzia fungu la 5 na 6, kuwe na onyesho fupi la kumhubiria isivyo rasmi mwenye duka na kumtolea trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? Mafungu ya 7 na 8 yasomwe kabla hamjayazungumzia. Malizia kwa kusoma na kuzungumzia sanduku “Usiwasahau!”
Dak. 18: “Jivikeni Unyenyekevu.”c Waombe wasikilizaji waeleze matumizi ya maandiko.
Wimbo 224 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Mwezi huu tunafanya jitihada ya pekee ya kuanzisha mafunzo ya Biblia. Zungumzia kifupi Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 2002, ukurasa wa 1, fungu la 1. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Hakikisha Unatanguliza Mambo Yanayopasa Kutangulizwa!” Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea makala ya Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, 1998, ukurasa wa 19-21. Taja tarehe za programu za kiroho za miezi kadhaa ijayo, na uwatie moyo wote waweke alama tarehe hizo kwenye kalenda zao. Waombe wasikilizaji waeleze wanayofanya ili wasikose maandalizi ya kiroho.
Dak. 20: Kushinda Uvutano wa Marika. Mhoji mzee au mtumishi wa huduma aliyelelewa na wazazi Wakristo. Zungumzia mambo makuu ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la Februari 15, 2003. Ndugu huyo alikabili uvutano gani shuleni? (uku. 24 fu. 3; uku. 25 fu. 4-5) Je, alikabili uvutano mbaya wa wengine? (uku. 26 fu. 4-6) Je, bado anakabili uvutano akiwa mtu mzima? Ni nini kimemsaidia kushinda uvutano huo? Malizia kwa hotuba fupi inayotegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 1, 1999, ukurasa wa 24-25 na ukazie faida za kuwa na marafiki wazuri.
Wimbo 26 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.