Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Je, unakubaliana na maneno haya? [Soma Yakobo 3:2.] Makala hii inatoa mapendekezo yanayofaa kutoka kwa Biblia ya kutusaidia tuepuke kuwaumiza washiriki wa familia kwa maneno yetu.” Zungumzia makala inayoanza kwenye ukurasa wa 10.
Amkeni! Jan.
“Kila ndoa ina matatizo yake. Unafikiri wenzi wa ndoa wanaweza kupata wapi mashauri yanayotegemeka? [Mruhusu ajibu.] Ona mwongozo huu unaofaa. [Soma Waefeso 5:22, 25.] Makala hii inaeleza jinsi mke anavyopaswa kujitiisha kwa mume wake.” Zungumzia makala inayoanza kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
“Kukiwa na matatizo mengi sana leo, je, unafikiri inawezekana kuwa na amani ya kweli ya akilini? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi wamefaidika kwa kufikiria tumaini la Biblia la ajili ya wakati ujao. [Soma moja kati ya maandiko yaliyonukuliwa au kutajwa katika makala unayozungumzia.] Gazeti hili linazungumzia kile ambacho Biblia inasema kuhusu mahali tulikotoka, kusudi la uhai, na kile ambacho tunatarajia wakati ujao.”
Amkeni! Feb.
“Kwa sababu ya kuongezeka kwa uhalifu, watu wengi hawajihisi wakiwa salama. Je, unafikiri hali zitawahi kuwa bora zaidi? [Mruhusu ajibu.] Ona unabii huu wa Biblia unaopendeza. [Soma Zaburi 37:10.] Gazeti hili linazungumzia chanzo cha uhalifu na suluhisho la Biblia la tatizo hilo.”