Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/09 uku. 1
  • Programu ya Kusanyiko la Pekee la Mwaka wa 2010

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Programu ya Kusanyiko la Pekee la Mwaka wa 2010
  • Huduma ya Ufalme—2009
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Mpango Mpya wa Kupitia Programu za Makusanyiko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Neno la Mungu Lina Nguvu
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2009
km 8/09 uku. 1

Programu ya Kusanyiko la Pekee la Mwaka wa 2010

1. (a) Ni habari gani za Biblia ambazo zimezungumziwa katika makusanyiko ya pekee katika miaka ya majuzi? (b) Je, kuna mambo yoyote yaliyozungumziwa katika makusanyiko ya pekee yaliyopita ambayo yamekusaidia katika huduma?

1 “Tuhakikishe Mambo Yaliyo ya Maana Zaidi,” “Kusimama Imara Tukiwa Kundi Moja,” “Fulizeni Kutoa Ushahidi Juu ya Kweli,” na “Sisi Ni Udongo—Yehova Ni Mfinyanzi Wetu.” (Flp. 1:9, 10, 27; Yoh. 18:37; Isa. 64:8) Vichwa hivyo ni baadhi tu ya vichwa vingi ambavyo vimezungumziwa katika makusanyiko ya pekee yaliyopita. Je, una hamu ya kuhudhuria kusanyiko la pekee la mwaka wa utumishi wa 2010? Mambo mbalimbali yanayohusu kichwa cha kusanyiko “Wakati Uliobaki Umepungua,” yatazungumziwa. Kichwa hicho kinategemea 1 Wakorintho 7:29.

2. Mnaweza kuchochea hamu ya kuhudhuria kusanyiko hili jinsi gani?

2 Mnaweza kuchochea hamu ya kuhudhuria kusanyiko hili kwa kuzungumzia programu kwa shauku mara tu baada ya tarehe ya kusanyiko lenu la pekee kutangazwa kutanikoni. Baadhi ya wazazi wanachochea hamu ya watoto wao ya kuhudhuria kusanyiko la pekee kwa kuweka alama katika kalenda nyumbani, kuandika orodha ya vitu ambavyo kila mtu anapaswa kubeba, na kisha kuhesabu siku zinazobaki mpaka kusanyiko litakapoanza. Katika jioni ya Ibada ya Familia mnaweza kupitia maandishi yenu ya mambo makuu ya makusanyiko ya pekee yaliyopita. Unaweza pia kutayarisha moyo wako kwa ajili ya kusanyiko hili kwa kupitia ukurasa wa 13-16 wa kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Sehemu hiyo ina mashauri kuhusu jinsi wewe na watu wa familia yenu mnavyoweza ‘kukazia uangalifu jinsi mnavyosikiliza.’—Luka 8:18.

3. Tunawezaje kunufaika kikamili na mambo yatakayozungumziwa?

3 Tenda Kupatana na Mambo Unayojifunza: Baada ya kuhudhuria kusanyiko wengi wanasema, “Programu ilikuwa nzuri ajabu!” Maneno hayo ni ya kweli kwa sababu makusanyiko yote ni maandalizi mazuri kutoka kwa Yehova. (Met. 10:22) Ili mambo unayojifunza yawe na manufaa, unahitaji kuyatafakari na kuyakumbuka. (Luka 8:15) Unaweza kuzungumzia programu pamoja na watu wa familia mnaposafiri kwenda nyumbani baada ya kusanyiko, au na wengine ambao unasafiri pamoja nao. Zungumzieni malengo ya mtu na mwenzake na mambo yanayoweza kuwasaidia katika huduma. Mkifanya hivyo, mtanufaika kwa muda mrefu na mambo mliyojifunza.—Yak. 1:25.

4. Kwa nini kusanyiko hili litatufaa kabisa?

4 Tunapopokea zawadi inayotufaa kabisa, tunajihisi kuwa wa maana. Tunatarajia kwa hamu mambo ambayo Yehova ametutayarishia katika kusanyiko lijalo la pekee. Hapana shaka kwamba yatatufaa kabisa. Tunaweza kutarajia kwamba Baba yetu wa mbinguni, Yehova, atatupa zawadi inayotufaa kabisa kwa kututia moyo na kutufundisha kufanya vizuri zaidi kazi ambayo ametugawia tuifanye.—2 Tim. 4:2; Yak. 1:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki