Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/10 uku. 2
  • Wahudumu Wakristo Wanahitaji Kusali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wahudumu Wakristo Wanahitaji Kusali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Tuombeane
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Yesu Anatufundisha Kusali
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Kumkaribia Mungu Katika Sala
    Mungu Anataka Tufanye Nini?
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 5/10 uku. 2

Wahudumu Wakristo Wanahitaji Kusali

1. Tunahitaji kufanya nini ili tutimize huduma yetu?

1 Hatuwezi kutimiza huduma kwa nguvu zetu wenyewe. Yehova ndiye anayetupa nguvu za kufanya kazi ya kuhubiri. (Flp. 4:13) Yeye anatumia malaika wake kutusaidia kupata watu walio kama kondoo. (Ufu. 14:6, 7) Ni Yehova ambaye anakuza mbegu za ukweli ambazo tunapanda na kuzitilia maji. (1 Kor. 3:6, 9) Ni muhimu sana kwa wahudumu Wakristo kumtegemea Baba yetu wa mbinguni katika sala!

2. Tunaweza kusali kuhusu nini?

2 Kusali Kuhusu Mahitaji Yetu Wenyewe: Tunapaswa kusali pindi zote tunapohubiri. (Efe. 6:18) Tunaweza kusali kuhusu nini? Tunaweza kumwomba Yehova atusaidie kuwa na mtazamo unaofaa kuhusu eneo letu na vilevile kuwa na ujasiri tunapohubiri. (Mdo. 4:29) Tunaweza kumwomba Yehova atuelekeze kwa watu wenye mioyo minyofu ili tujifunze Biblia pamoja nao. Mwenye nyumba anapouliza swali, tunaweza kutoa sala fupi kimya-kimya na kumwomba Yehova atusaidie kumpa mwenye nyumba huyo jibu linalofaa. (Neh. 2:4) Tunaweza pia kusali tupate hekima ya kutanguliza huduma maishani. (Yak. 1:5) Vilevile, Yehova anafurahi tunapomshukuru kwa pendeleo la kuwa wahudumu wake.—Kol. 3:15.

3. Kusali kwa ajili ya wengine kunafanikisha kazi ya kuhubiri katika njia zipi?

3 Kusali kwa Ajili ya Wengine: Biblia inawatia Wakristo moyo ‘wasali kwa ajili ya mtu na mwenzake.’ Hivyo, inapofaa, tunaweza kutaja majina ya wahudumu wenzetu katika sala. (Yak. 5:16; Mdo. 12:5) Je, matatizo ya afya yanakuzuia usitimize mengi katika kazi ya kuhubiri? Basi, sali kwa ajili ya wahudumu wenzako walio na afya nzuri. Sala zako kwa ajili yao zinaweza kuwa na nguvu nyingi sana! Pia, inafaa kusali kwa ajili ya wenye mamlaka za nchi ili wawe na mwelekeo unaofaa kuelekea kazi yetu ya kuhubiri. Huenda jambo hili likawawezesha ndugu zetu ‘waendelee kuishi maisha shwari na matulivu.’—1 Tim. 2:1, 2.

4. Kwa nini tunapaswa kudumu katika sala?

4 Tuna kazi kubwa sana ya kutangaza habari njema katika dunia yote inayokaliwa. Tutatimiza kazi hii kwa msaada wa Yehova ikiwa ‘tutadumu katika sala.’—Rom. 12:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki