Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kupendezwa na Watu Kibinafsi
Kwa Nini Ni Muhimu: Yesu alipendezwa na watu kibinafsi. Kwa mfano, pindi moja huenda Yesu alitambua kwamba kiziwi fulani ana wasiwasi, hivyo alimponya faraghani mbali na umati wa watu. (Marko 7:31-35) Aliwaonyesha ufikirio wanafunzi wake kwa kutambua mipaka yao na hivyo hakuwaambia mambo mengi kupita kiasi. (Yoh. 16:12) Hata akiwa mbinguni, Yesu anapendezwa na watu kibinafsi. (2 Tim. 4:17) Tukiwa wafuasi wa Kristo, tunapenda kumwiga. (1 Pet. 2:21; 1 Yoh. 3:16, 18) Zaidi ya hilo, tutakuwa na matokeo zaidi katika huduma ikiwa tutamwonyesha mwenye nyumba ufikirio na kuzingatia hali, mapendezi, na mahangaiko yake. Huenda atakuwa tayari kusikiliza, akitambua kwamba kusudi letu si tu kusambaza ujumbe au kugawa machapisho, bali tunapendezwa naye kibinafsi.
Jaribu Dokezo Hili kwa Mwezi Mzima:
Fanyeni mazoezi wakati wa ibada ya familia, au labda mnapokuwa katika utumishi, kuhusu jinsi mhubiri anavyoweza kubadili mazungumzo ili azungumzie jambo linalomhangaisha mwenye nyumba.
Katika baadhi ya mikutano ya utumishi wa shambani, ndugu anayeongoza anaweza kuzungumzia au kupanga kuwe na onyesho la jinsi ya kupendezwa na watu kibinafsi.