HAZINA ZA NENO LA MUNGU | 2 WAKORINTHO 4-6
“Hatufi Moyo”
Fikiria familia mbili zinazoishi kwenye jengo moja la zamani na bovu. Washiriki wa familia moja wanaonekana wamevunjika moyo. Jambo la kushangaza ni kwamba familia ile nyingine ina furaha. Kwa nini? Kwa sababu, hivi karibuni washiriki wa familia hiyo ya pili watahamia kwenye nyumba nzuri na mpya.
Ingawa “uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja mpaka sasa,” watumishi wa Mungu wana tumaini linalowaimarisha. (Ro 8:22) Tunajua kwamba matatizo tunayokabili sasa, hata yale yanayoendelea kutusumbua kwa miaka mingi, ni “ya muda mfupi na ni [mepesi]” tunapoyalinganisha na uzima wa milele katika ulimwengu mpya wa Mungu. Kukazia fikira baraka za wakati ujao za Ufalme kutatusaidia tuwe na furaha na tusife moyo.