Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb88 kur. 253-255
  • ‘Sisi Tunamtumikia Yehova!’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Sisi Tunamtumikia Yehova!’
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ule “Mkutano Mkubwa” Waendelea Kukua
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Mashahidi wa Yehova—Ripoti ya Kitabu-Mwaka 1994
    1994 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Ushindi Mkubwa Kupitia Kwa Imani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Kitabu-mwaka cha Mashahidi wa Yehova 1990
    1990 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb88 kur. 253-255

‘Sisi Tunamtumikia Yehova!’

“Chagueni kwa ajili yenu wenyewe leo ambaye ninyi mtamtumikia” ndilo takwa ambalo Yoshua aliweka mbele ya Waisraeli karne 34 zilizopita. Itikio la Yoshua kwa maneno yake mwenyewe yenye kuchunguza moyo lilisikika wazi: “Kwa habari yangu mimi na nyumba yangu, sisi tutamtumikia Yehova.” (Yos. 24:15, NW) Kama Yoshua wa kale, Mashahidi wa Yehova wa leo ‘watamtumikia Yehova.’ Hilo ndilo lililokuwa andiko letu kwa mwaka uliopita. Nayo ripoti ya mwaka wa utumishi wa 1987 inatoa ushuhuda ulio wazi sana kwamba Mashahidi wa Yehova katika nchi 210 wanamtumikia Yehova kwa moyo mzima wote!

Je! wewe hukushangilia katika kujifunza juu ya kilele kipya cha wahubiri—3,395,612? Namna gani hesabu ya waliobatizwa—230,843? Maongezeko yote mawili ni ushuhuda wenye kuonekana wa baraka ya Yehova juu ya kazi ya kueneza evanjeli ulimwenguni pote mwaka huo wa utumishi uliopita. Ebu wazia! Yale maongezeko ambayo tumesoma juu yayo katika Kitabu cha Mwaka chetu yameonwa pia kutoka mbinguni na malaika watakatifu pamoja na Yehova na Kristo Yesu. Lo, ni shangwe iliyoje ambayo lazima kazi hiyo iwe iliwaletea!—Linganisha Luka 15:6, 7.

Hata marufuku za kiserikali haziwezi kuzuia Kristo Yesu asiwaongoze wanafunzi wake kwa njia yenye utendaji wajisukume mbele katika kazi ya kueneza evanjeli. Hesabu iliyorekodiwa ya wahubiri 267,296 wenye shughuli katika maeneo ambako uhuru wa kuhubiri umepunguzwa ni ithibati iliyo hai ya uhakika huo! Lo, ni mifano myema kama nini ya ushikamanifu ambayo akina ndugu hawa wameweka—hata kukiwa na hatari ya kufungwa gerezani au kupoteza uhai!

Ndugu zetu wameteseka sana sana mahali pengi. Katika nchi moja ya Kiafrika, kuanzia Januari kufika Aprili 1987 wimbi baya sana la mateso liliwapata ndugu zetu. Miongo kadhaa yao walitiwa mbaroni kwa sababu tu wao walikuwa Mashahidi wa Yehova. Lakini utendaji wa kitheokrasi umepangwa upya kitengenezo, nayo kazi ya kufanya wanafunzi inaendelea. Tawi linaloangalia nchi hiyo linaripoti hivi: “Bila kuepukika pamoja na mateso hayo kumekuwako usafishaji wa kuondolea nje wale wanaokosa imani. Hata hivyo, walio wengi wao wanabaki wakiwa imara, na kazi inaendelea kusonga mbele, kukiwako na wengi wapya wanaobatizwa.”

Katika nchi fulani ambako utendaji wetu wa kutoa ushuhuda umekuwa chini ya vizuizi, ndugu zetu wameruhusiwa uhuru zaidi wahubiri na kukutana waziwazi. Sisi tunashukuru kwamba katika sehemu hizi watawala wenye akili zenye kutaka haki wamesukumwa waondoe vizuizi hivi na kwamba sala kwa ajili ya ndugu zetu zimejibiwa. (1 Tim. 2:1, 2) Mabadiliko ya haraka ya kutokeza watawala wapya katika nchi nyingine yameleta mateso yenye jeuri. Hali hizi zilizobadilika hazitangazwi sikuzote katika Kitabu cha Mwaka. Hivyo, acheni hiki kiwe kikumbusha kwamba haitupasi sisi kuwa wazembe katika ibada yetu na kukata kauli kwamba upinzani wenye jeuri hutukia katika sehemu za mbali zaidi tu. Tumieni mambo yaliyoonwa katika ripoti hii yawe chanzo cha kitia-moyo na kama msaada wa kuwatieni nguvu pia kwa ajili ya yo yote yale yanayoweza kuletwa na wakati ujao. Jinsi yanavyotia moyo maneno ya mtume Paulo! Yeye aliandika: “Ikiwa Mungu yu kwa ajili yetu, ni nani ambaye atakuwa dhidi ya sisi?”—Rum. 8:31, NW.

Ule “Mkutano Mkubwa” Waendelea Kukua

Sisi tunafurahi kushuhudia kukusanywa kwa ule “mkutano mkubwa” kulikotabiriwa, hata ingawa hilo lataka jitihada iliyoongezeka upande wa kila mmoja wetu. (Ufu. 7:9) Majumba ya Ufalme na Majumba ya makusanyiko zaidi lazima yajengwe, na vifaa vya tawi zaidi lazima vipanuliwe. Sisi twathamini kweli kweli ile michango ya ukarimu ya kazi ngumu na fedha kutoka kwa waabudu wenzetu ili kutusaidia katika kazi hii kubwa ya upanuzi. Ule ubinafsi wa ulimwengu hakika haujaambukia ndugu zetu.—2 Tim. 3:1, 2.

Baadhi ya akina ndugu wanaweza kuwa sehemu ya programu ya Wafanya Kazi ya Ujenzi wa Kujitolea wa Kimataifa na kusaidia ujenzi wa matawi nje ya nchi ya kwao. Mfanya-kazi wa kujitolea mmoja alituandikia hivi: “Sharti niseme asanteni kwa pendeleo zuri sana! Ni vigumu kutia katika maneno ile nguvu na upendo ambao mimi nilipata katika kufanya kazi pamoja na ndugu zangu. Unyenyekevu wao, upendo wao kwa Biblia na Yehova, na kushikamana kwao imara na tumaini la ulimwengu mpya liliacha mimi nikiwa na mengi ya kutafakari mwishoni mwa kila siku.”

Ni kweli, lile ongezeko zuri ajabu la hesabu ya wasifaji wa Yehova huleta baraka nyingi kwa watu wake wote, lakini pia linakazia uhitaji mkubwa wa kutolegeza mkono. Kuhubiriwa kwa habari njema za Ufalme lazima kuendelee mpaka mwisho. (Marko 13:10) Na kama inavyoonekana wazi kutokana na hadhirina ya ukumbusho ya mwaka uliopita ya 8,965,221 kuna wengi zaidi ambao huenda wakawa bado washiriki wenzetu katika kazi ya kueneza evanjeli. Kwa hiyo sasa ndio wakati wa ‘kujitahidi wenyewe’ katika “kazi ya Bwana.” (Luka 13:24; 1 Kor. 15:58) Je! kile kielelezo cha ndugu zetu, kama kilivyosimuliwa katika ripoti hii, hakifanyizi ndani yetu tamaa yenye kuwaka ya kufanya lo lote liwezekanalo tuwasaidie wapya wajiunge nasi katika ibada ya kweli? Wengi wanaingia katika utumishi wa wakati wote. Wewe, pia, waweza kujiunga na hesabu ya mapainia wa kawaida ambao walifikia kilele kipya cha 665,327 wakati wa 1987. Ikiwa hili haliwezekani kwa sababu ya hali ambazo huwezi kuzuia, usife moyo. Fanya yote yote uwezayo katika utumishi wa Yehova, naye atakubariki wewe.—Luka 21:1-4.

Ni jambo gani tunaloweza kufanya sisi sote tusaidie na kutia moyo wale vijana wengi wanaoshirikiana nasi kwenye mikutano yetu, pamoja na wapya waliobatizwa? Sisi tunahitaji kuonyesha ufahamu na subira. Iweni wenye fadhili na kuhurumia, na mwatie moyo wafanye maendeleo, mkiwaalika washiriki pamoja nasi utendaji wa Ufalme.

Kwa kuwa sisi tunaishi katika wakati wa mtihani, pigeni moyo konde, kama Yoshua, kumtumikia Yehova! Mambo yaliyoonwa yaliyoandikwa katika hiki Kitabu cha Mwaka na yatusaidie kuthamini uhakikisho wa Yehova kwamba hatuhitaji kuogopa. (Isa. 41:10) Huku mikazo ya ulimwengu ikiendelea kupanda, sisi sote na tutii shauri lenye hekima la andiko la mwaka wa utumishi wa 1988: “Tumaini katika Yehova na kushika njia yake.”—Zab. 37:34, NW.

Sisi kwenye makao makuu ya ulimwengu tunawajali ninyi na kuwahangaikia sana sana. Sisi tunasali kwamba ninyi ‘mtaendelea kukua katika fadhili zisizostahiliwa na maarifa ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo’ na ya Mungu wake na Mungu wetu, Yehova.—2 Pet. 3:18, NW.

Ndugu Zenu,

BARAZA LINALOONGOZA LA MASHAHIDI WA YEHOVA

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki