Kutoka kwa Wasomaji Wetu
Kimbunga Andrew Makala nzuri ajabu! (“Mambo Ambayo Kimbunga Andrew Hakingeweza Kuharibu,” Januari 8, 1993) Kwa vile nilikuwa na pendeleo la kusaidia katika kazi ya kutoa msaada, hasa nilifurahia manukuu kutoka kwa wakazi wenyeji. Siku saba nilizokaa huko ziliimarisha tumaini langu kwa Yehova na kunitia moyo nipende ndugu na dada zangu Wakristo zaidi na zaidi.
M. J., United States
Mnyanyaso wa Nazi Asanteni kwa makala “Kushika Ukamilifu-Maadili Katika Ujerumani ya Nazi.” (Februari 8, 1993) Ndugu na dada zetu Wakristo wamepitia majaribu mengi sana, lakini wanabaki wakiwa waaminifu! Iwapo nimepatwa na jaribu kali sana, natumaini nitakuwa na nguvu na uvumilivu wa Josef Rehwald na familia yake.
D. J. United States
Leo nilisoma masimulizi ya maisha ya Josef Rehwald. Nilitokwa machozi nilipofikiria jinsi Yehova anavyotegemeza watumishi wake katika nyakati za taabu. Nililazimika Kumshukuru!
V. M., Italia
Vitumbuizo Zile makala za “Vitumbuizo Vinaathirije Maisha Yako?” (Novemba 8, 1992, Kiingereza) zilikuja kwa wakati unaofaa kabisa. Hasa nilithamini habari zilizotolewa juu ya sinema. Ninafanya kazi katika duka la kukopesha vidio, na sinema Basic Instinct mliyotaja katika makala yenu ilikuwa ndiyo vidio iliyopendwa zaidi. Siwezi kuamini jinsi sinema mbovu zinavyonunuliwa sana!
D. M., United States
Usanii wa Kisasa Mtu akisoma makala “Usanii wa Kisasa Washindwa” (“Kuutazama Ulimwengu,” Novemba 8, 1992, Kiingereza), anaweza kupata wazo la kwamba rangi za akriliki hazifai sana. Lakini sivyo. Kwa kweli, zina mafaa makubwa mengi kuliko rangi za aina nyingine. Kwa mfano, hazichanganyiki na oksijeni. Kwa kuongezea, vyandarua vya kibiashara vya uchoraji hutumia akriliki ikiwa rangi ya msingi. Hatari za kumomonyoka hutokea wakati rangi ya akriliki inapopakwa vibaya, labda kwenye sehemu yenye uchafu au yenye mafuta-mafuta. Huenda ilikuwa hivyo na msanii aliyetajwa.
J. W., Uswisi
Tunathamini jinsi umeweka jambo hilo wazi.—Mhariri.
Ndugu Wanaopotea Asanteni kwa makala yenye kichwa “Vijana Wanauliza . . . Je! Nitakuwa Kama Ndugu Yangu?” (Desemba 22, 1992, Kiingereza) Niliithamini sana. Dada yangu alikuwa painia [mweneza-evanjeli wa wakati wote], na tulikuwa na uhusiano wa karibu. Nilikuwa na mradi wa kupainia pamoja na yeye, lakini upesi baadaye mradi wangu ukafifia. Miezi minne baada ya mimi kubatizwa nikiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, alitengwa na ushirika wa kutaniko. Hilo lilikuwa jambo gumu kwangu, hasa wakati marafiki wangeniuliza juu yake. Sikuweza kujivunia juu yake tena. Makala hiyo ilinisaidia nijue kwamba ninaweza kuwa (na nitakuwa) tofauti!
L. S., United States
Nilikuwa na wakati mgumu ndugu yangu alipotengwa na ushirika. Hata hivyo, sikuwa kama yeye. Sasa nimehitimu shule ya sekondari na ninaweza kupainia. Pia ninasaidia katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova. Ningependa niweke bidii na kudumu katika kufanya yaliyo mema.
K. M., Japani
Nina ndugu wawili waliotengwa na ushirika. Nyakati fulani nilikuwa mwoga kubatizwa kwa sababu nilifikiri ningekuwa kama wao. Yehova alijibu sala zangu kupitia makala hiyo. Katika Januari, nilibatizwa. Hivyo niliweza kuonyesha wazi kwamba nilikuwa nimejiweka wakfu kwa Yehova, na nitakuwa mwangalifu nisifanye makosa yale waliyofanya ndugu zangu.
R. C., Italia