Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g98 4/22 kur. 3-5
  • Tatizo Laenea

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tatizo Laenea
  • Amkeni!—1998
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Pigo la Kuhuzunisha Sana
  • Je! Nijiunge na Genge?
    Amkeni!—1992
  • Mambo Tupaswayo Kujua Kuhusu Magenge
    Amkeni!—1998
  • Kuwalinda Watoto Wetu na Magenge
    Amkeni!—1998
  • Magenge ya Wanawake—Mwelekeo wa Kutisha
    Amkeni!—1996
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1998
g98 4/22 kur. 3-5

Tatizo Laenea

Robert mchanga alikuwa na umri wa miaka 11 tu, na bado alipatikana akiwa amelala kifudifudi chini ya daraja lililokuwa ukiwa. Kulikuwa na mashimo mawili ya risasi kisogoni mwake. Iliaminiwa, alikuwa ameuawa na washiriki wa genge lake la vijana.

Alex mwenye umri wa miaka 15 alikuwa anaelekea kuwa mshiriki wa genge na labda alielekeana na kifo cha mapema. Lakini aliona rafiki yake akifa, na alifikiria: ‘Singependa kupatwa na jambo kama hilo.’

MAGENGE ya mtaani yenye jeuri, ambayo wakati mmoja yalishirikishwa na magenge ya Los Angeles yenye kujulikana sana yaliyoitwa Bloods na Crips, yameenea ulimwenguni pote. Lakini popote yanapokuwa, kwa kustaajabisha magenge hufanana.

Genge la Uingereza “Teddy Boys” lilishtua ulimwengu katika miaka ya 1950. Gazeti The Times la London lilisema kwamba lilitumia mashoka, visu, minyororo ya baiskeli, na silaha nyinginezo ili “kusababisha majeraha mabaya sana” kwa watu wasiokuwa na hatia. ‘Mapigano ya visu yalizuka, mikahawa iliharibiwa, na majengo ya kuuzia kahawa yalibomolewa.’ Watu walisumbuliwa, wakapokonywa, wakapigwa, na nyakati nyingine wakauawa.

Gazeti la habari Die Welt la Hamburg, Ujerumani, liliripoti kwamba hivi karibuni vijana “wakiwa njiani kuelekea kwenye disko au wakiwa njiani kurudi nyumbani mwao” wameshambuliwa na magenge yenye kutumia “magongo ya besiboli, visu, na bunduki.” Gazeti la habari la Munich Süddeutsche Zeitung lilisema kwamba magenge yenye nywele fupi sana katika Berlin hushambulia mtu yeyote “ambaye huonekana kuwa dhaifu—wasiokuwa na makao, walemavu, wanawake waliostaafu.”

Mleta-habari wa Amkeni! katika Hispania aliripoti kwamba tatizo la magenge ya matineja huko ni la karibuni lakini linakua. Gazeti la habari katika Madrid, ABC, lilikuwa na kichwa cha habari “Magenge Yenye Nywele Fupi Sana—Ogofyo Jipya la Mitaani.” Mshiriki mmoja wa genge lenye nywele fupi sana wa awali wa kutoka Hispania alisema kwamba wangegundua “kuku mgeni, makahaba, na wagoni-jinsia-moja.” Aliongezea: “Usiku usiokuwa na jeuri [haukufaa] kitu.”

Katika Afrika Kusini Cape Times lilisema kwamba mwingi wa uhalifu huko ni “zaotuka la utamaduni wa genge wenye makosa.” Kitabu kilichochapishwa katika Cape Town husema kwamba magenge ya Afrika Kusini yalikuwa “vimelea” katika vitongoji vilivyo maskini zaidi na kwamba “yaliibia na kuwabaka washiriki wa jumuiya zao wenyewe na kujiingiza katika mapigano ya magenge juu ya maeneo, bidhaa zinazohitajiwa, na wanawake.”

Gazeti la habari la Brazili O Estado de S. Paulo, lilisema kwamba huko magenge yalikuwa “yakiongezeka kwa kiwango chenye kuogopesha.” Lilitaarifu kwamba yangeshambulia magenge ya upinzani, vijana walio na hali bora, watu wa jamii nyingine, na wafanyakazi-wahamaji walio maskini. Pia lilisema kwamba siku moja magenge kadhaa yalifanyiza wavu, “yakawaibia watu waliokuwa katika ufuo . . . , yakapigana miongoni mwao wenyewe,” na kugeuza barabara moja ya Rio de Janeiro “kuwa ukanda wa vita.” Ripoti nyingine kutoka Brazili ilisema kwamba idadi ya magenge inaongezeka katika majiji makubwa kama vile São Paulo na Rio de Janeiro na katika miji midogo.

Gazeti la Kanada Maclean’s lilisema kwamba katika mwaka wa 1995 kulingana na makadirio ya polisi, kulikuwa na angalau magenge ya mtaani manane yenye kutenda katika Winnipeg, Kanada. Na magazeti ya habari katika Marekani yamechapisha picha za washiriki wa magenge ambao wameingiza nguo za magenge na michoro ya ukutani hadi kwenye maeneo yaliyotengwa ya Wahindi wa Amerika ya Kusini-Magharibi.

Katika New York City, ujeuri uliohusishwa na genge uliotokea mara nyingi na kwa muda mfupi uliibuka mwaka jana. Washiriki wa Bloods na Crips, magenge ambayo hapo awali yalikuwa mashuhuri katika Los Angeles, walisemekana kuwa walihusika. Kulingana na meya wa New York, kati ya Julai na Septemba, polisi waliwashika watu 702 katika visa vilivyohusiana moja kwa moja na magenge ya mtaani.

Tatizo hili haliko tu katika majiji makubwa tena. Gazeti la habari Quad-City Times, linalochapishwa katika sehemu ya kati ya Marekani, lilisema juu ya “jeuri iliyoongezeka miongoni mwa matineja, matumizi yenye kuenea ya madawa ya kulevya na hisi inayokua ya kujiona kutofaa kitu.”

Pigo la Kuhuzunisha Sana

Genge moja lasemekana kuwa lilianza likiwa kikundi cha marafiki. Lakini sifa ya kiongozi wake ilipokua, ndivyo ilivyokuwa na jeuri. Kiongozi wa genge hilo aliishi katika nyumba ya nyanya yake, ambayo ilipigwa risasi mara kadhaa, hata wakati nyanya yake alipokuwa ndani. Gazeti moja la habari liliripoti kwamba kuliwako zaidi ya mashimo 50 ya risasi katika nyumba hiyo. Yaelekea risasi hizo zilirushwa kwa kulipiza kisasi kwa ajili ya matendo ambayo, genge la mjukuu huyo lilifanya. Kwa kuongezea, kaka ya kiongozi wa genge hilo alikuwa gerezani likiwa tokeo la utendaji uliohusiana na genge, na vilevile binamu yake, ambaye alikuwa amehama ili kuepa jeuri na aliyekuwa amerudi nyumbani kuzuru, alikuwa amepigwa risasi na mtu fulani aliyekuwa ndani ya gari la mizigo lililokuwa linapita.

Katika Los Angeles, washiriki wa genge walipiga gari risasi na kumwua mtoto mchanga mwenye umri wa miaka mitatu asiyekuwa na hatia ambaye mama yake na rafiki wa kiume wa mama yake walikuwa wamepitia katika barabara fulani kwa makosa. Risasi ilivunja shule na kumpiga mwalimu aliyekuwa akijaribu kuwasaidia wanafunzi wajifunze namna ya kuboresha maisha zao. Wengine wengi wameuawa pia ambao hawakuhusika kabisa na magenge lakini ambao wamekuwa wahasiriwa wake. Mama mmoja wa Brooklyn, New York, alijulikana katika ujirani wake kwa sababu ya hali yake iliyohuzunisha sana na ya kipekee—kuwapoteza wana wake wachanga watatu kwa sababu ya jeuri ya genge.

Ni nini kimesababisha tatizo hili la ulimwenguni pote la jeuri inayofanywa na vijana, na twaweza kuwalindaje watoto wetu wapendwa na jeuri? Kwanza magenge huanzaje, na kwa nini vijana wengi sana wanajiunga nayo? Maswali haya yanazungumziwa katika makala zinazofuata.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 3]

Scott Olson/Sipa Press

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki