Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • sj kur. 4-5
  • Kusudi Letu Katika Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kusudi Letu Katika Maisha
  • Shule na Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wanavyoiona Biblia
  • Elimu Yenye Kusudi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Sababu Gani Ujifunze Shuleni?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Pata Manufaa Zote za Shule
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kutotukuza Elimu Mno
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Shule na Mashahidi wa Yehova
sj kur. 4-5

Kusudi Letu Katika Maisha

Kwanza, itafaa tueleze kwa ufupi juu ya Mashahidi wa Yehova na kusudi letu katika maisha. Sisi ni jamii ya mataifa yote ya Wakristo wanaoweza kupatikana katika nchi zaidi ya 200 ulimwenguni pote. Njia yetu ya kuabudia Mungu inatia ndani maoni yetu yote na namna yetu yote ya maisha.

Kwa kuwa tunasadiki kwamba kuna Mungu kweli kweli, tunaona ni muhimu tuendeleze uhusiano wa karibu sana na wa kibinafsi pamoja naye, Baba yetu. (Mathayo 6:9) Kati ya mambo mengine, hiyo inatia ndani kumjua yeye kwa jina lake. Biblia inasema hivi katika Zaburi 83:18: “Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.”

Sisi tukiwa Wakristo, tunajaribu pia kufuatisha maisha zetu kwa mfano wa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu. Hekima ya mafundisho yake inaonyesha kwamba yeye alikuwa mtu mashuhuri mwenye elimu sana. Lakini Yesu alitumia maarifa yake kwa faida ya wengine. Hakuyatumia ili ajipatie cheo cha kumletea fedha wala cheo kikubwa. Kumtumikia Mungu kulikuwa ndilo jambo kuu zaidi katika maisha yake. Yesu alisema: “Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.”—Yohana 4:34.

Maoni yetu ni kama hayo. Kwa kusudi hilo, Mashahidi ulimwenguni pote wanaona ubora wa elimu nzuri. Sisi tunawatia moyo watoto wetu wapanue maoni yao—wapate maarifa na ufahamu wa mazingira yao na maana ya maisha. Kwa kusudi hilo wanasoma, na mara nyingi wanatumia gazeti letu Amkeni! katika masomo yao ya shule. Gazeti hilo linazungumza karibu sehemu zote za maarifa ya kibinadamu. Walimu fulani pia wanatumia gazeti hilo wakitayarisha mitaala yao ya shule.

Mazoezi ya elimu ambayo watoto wetu wanapokea yamesaidia wengi wao wasitawishe uwezo wao wa kubuni vitu. Kichapo kinachoitwa Journal of Personality kilisema hivi kilipotoa ripoti juu ya uchunguzi wa Australia juu ya “akili ya kubuni vitu” ya watoto wenye umri wa miaka 12. Wachunguzi wa habari walisema: “Hasa, idadi kubwa isiyokadirika ya watoto wenye akili nyingi za kubuni vitu walikuwa Mashahidi wa Yehova.” Sababu hiyo inaweza kuwa ni kwa vile dini ya Mashahidi inatia moyo watu watumie uwezo wao wa kufikiri.

Hata vijana-Mashahidi wajapopendezwa na elimu nzuri, hawafuatii masomo ya shule wakiwa na nia ya kujipatia sifa au cheo kikubwa. Mradi wao mkubwa katika maisha ni kutumikia vya kufaa wakiwa wahudumu wa Mungu, na wanathamini masomo ya shule kuwa msaada wa kutimiza mradi huo. Basi kwa ujumla wanachagua mitaala inayofaa ili wajipatie riziki katika ulimwengu wa kisasa. Hivyo, huenda wengi wakajifunza mitaala ya kikazi au wakahudhuria shule zinazotoa mafundisho ya kazi. Wanapomaliza shule wanatamani kutafuta kazi itakayowaruhusu wakaze fikira zao juu ya kazi yao kuu, yaani, huduma ya Kikristo.

Wanavyoiona Biblia

Kama unavyoweza kufahamu kutokana na yaliyotangulia, Mashahidi wa Yehova wanaiona Biblia kuwa kiongozi cha kila siku kwa uzito zaidi ya watu wengi. Wanaamini kweli kweli kwamba “kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu.”—2 Timotheo 3:16, Zaïre Swahili Bible.

Kupatana na maneno hayo, sisi tunaamini kwamba kila jambo lililoandikwa katika Biblia ni sahihi na limepasa kuwa mwongozo wa Mkristo katika maisha. Kwa sababu hiyo, huenda ikawa kwamba maoni ya kijana Shahidi juu ya shughuli fulani za shule yatakuwa tofauti sana na yale ya mwanafunzi asiyeichukua Biblia kwa uzito sana. Broshua hii itazungumza shughuli zinazohusika na itajaribu kukusaidia ufahamu ni kwa nini Mashahidi wa Yehova wanachukua msimamo huo juu ya shughuli hizo.

Kwa kuwa, kama unavyojua kwa kutokeza Biblia ni kitabu cha unabii, tungependa ufikirie kinachofanya Mashahidi hao wawe na mwelekeo fulani juu ya shule, kwa sababu ya kuamini unabii wa Biblia.

[Blabu katika ukurasa wa 4]

Mashahidi ulimwenguni pote wanaona ubora wa elimu nzuri

[Picha na blabu katika ukurasa wa 5]

Inatumiwa kuwa mwongozo wa kila siku

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki