Waliokuwa Wapinzani Wanakubali Kweli ya Biblia
WATU wanaopinga vikali kazi ya mashahidi wa Kikristo wa Yehova mara nyingi wanafanya hivyo kwa kutokujua. Moyoni wengi hawako vile maneno yao makali yanavyoonyesha. Kati ya wale wanaojifunza Biblia sasa na mashahidi wa Yehova au kushiriki pamoja nao katika kuhubiri habari njema walikuwa wapinzani. Ni jambo gani lililowafanya wengine wa watu hawa kugeuka?
● Mtu mmoja Mkanada aliyekuwa amewafukuza mashahidi wa Yehova walipomtembelea aligeuza nia yake nyuma ya kusoma nakala moja tu ya Awake!
Alipokuwa akifanya ununuzi katika mji karibu na nyumba yake, mtu huyu aliona gazeti la Awake! chini barabarani. Likiwa limechanika na chafu, lilikuwa na kichwa, “Je! Makanisa Yanakaribia Mwisho Wao?” Huyo mtu aliliokota gazeti hilo na kulipeleka nyumbani. Yeye na jamaa yake walilisoma na kurudia kulisoma. Walikuwa karibu kuyasema yaliyomo kwa moyo.
Walipokuwa wakitembelea nyumba tena katika eneo hilo, mashahidi wa Yehova walisita kumtembelea yule mtu mpinzani. Lakini Shahidi mmoja alifanya hivyo. Fikiria mshangao wake aliposalimiwa kwa furaha na uchangamfu! Huyu mtu alikuwa amekuwa akiwangoja mashahidi wa Yehova wamtembelee. Jamaa yote kwa bidii ilikubali kuwa na funzo la Biblia nyumbani mwao. Mbele ya funzo la kwanza kuongozwa walisafiri maili 40 kumtembelea Shahidi. Mazungumzo ya saa tano na nusu yakafuata. Kulingana na ripoti ya mwisho, jamaa hiyo inafanya maendeleo mema katika funzo la Maandiko.
● Mara nyingi, si habari iliyosemwa au iliyoandikwa, bali ni mwenendo wa mashahidi wa Yehova unaoshinda maoni mabaya yasiyo na msingi.
Shahidi Mnigeria aliokota kifuko chenye pauni moja (shilingi 20.00) mahali anapofanya kazi. Kifuko hiki kilikuwa mali ya kiongozi wa idara, mtu aliyewachukia mashahidi wa Yehova. Bila ya Shahidi kujua, mmoja wa wafanya kazi wenzi wa yule mtu akamwambia kwamba ‘hangepata fedha yake tena isipokuwa “mtu wa Yehova” amekipata kifuko.’ Ikatukia kwamba, Shahidi alikiokota na mara moja akakipeleka kwa kiongozi wa idara yake. Mtu yule alishangaa. Sasa aliona kwamba kulikuwa na tofauti kati ya mashahidi wa Yehova na watu wengine. Nyumaye, Shahidi alimpa msaada wa kujifunza Biblia Kweli Iongozayo kwenye Uzima wa Milele. Halafu funzo la Biblia lilianzwa na huyu aliyekuwa mpinzani.
● Katika kijiji cha Nigeria palikuwa na mtu aliyewachukia mashahidi wa Yehova. Aliabudu “juju” (uchawi) na kuzoea dawa za kienyeji. Siku moja, alipopanda mtende shambani lake kutoa utomvu wa mtende, kamba yake ilikatika. Alianguka chini, akavunjika miguu. Akapiga yowe kwa uchungu, lakini majirani zake na marafiki, labda kwa sababu ya woga wa ushirikina, wakamwacha. Mashahidi fulani wakasikia juu ya kisa hicho na kukimbilia pale. Mtu aliyeumia alikuwa amezimia. Kwa haraka Mashahidi wakampeleka hospitali na kufanya mipango ya kumtunza. Aliporudiwa na fahamu, mtu huyu aligundua kwamba wale aliokuwa amechukia walimtunza, na hali marafiki zake walimwacha. Nyuma ya hapo alikubali kuwa na funzo la nyumbani la Biblia na mashahidi wa Yehova. Leo ni Shahidi aliyebatizwa na, kupitia kwa juhudi yake, wanne wengine katika jamaa yake walikubali kweli ya Biblia kama ilivyotangazwa na mashahidi wa Yehova.
● Katika New Zealand mwanamke mmoja alikuwa hataki matembezi ya mashahidi wa Yehova hivyo kwamba alimwuliza mumewe aweke kibao nje mlangoni kikiwakataza kuingia. Mbele ya kibao hicho kuwekwa, Shahidi alimtembelea mwanamke huyu, kukaribishwa tu kwa ukali. Akiona kwamba mwanamke huyu alikuwa na ugumu kufikia keki iliyokuwa juu, Shahidi huyu wa kike alijitoa kumsaidia. Onyesho hili la kirafiki lilimtuliza mwanamke huyo mpinzani na kumwongoza kukubali funzo la Biblia.
Halafu kidogo huyu aliyekuwa mpinzani alianza kuhudhuria mikutano ya mashahidi wa Yehova. Kwanza alikuwa mwenye kisirani na alimeza dawa za kukituliza. Lakini, kwa kutumia shauri la Biblia juu ya mwenendo, hakutaka tena dawa. Vile vile aliacha na tabia ya kuvuta tumbako. Leo yeye, kama Shahidi aliyebatizwa, anawaambia wengine juu ya Maandiko.
Haimpasi mtu awahukumu watu kulingana na walivyo kwa nje. Ni mapenzi ya Mungu kwamba “watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli.” (1 Tim. 2:4) Hivyo mashahidi wa Kikristo wa Yehova wanajaribu kuendelea kuwatembelea watu wote, kutia ndani na wapinzani, na “habari njema” juu ya ufalme wa Mungu.