Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 9/15 kur. 430-431
  • Fika Kwenye “Utumishi Mtakatifu” Kusanyiko!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fika Kwenye “Utumishi Mtakatifu” Kusanyiko!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAHALI PA KUSANYIKO
  • “Kweli ya Ufalme” Makusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • “Amani ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1986
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • “Ongezeko la Ufalme” Makusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Njooni Kwenye Mkusanyiko wa Wilaya wa “Hofu ya Kimungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 9/15 kur. 430-431

Fika Kwenye “Utumishi Mtakatifu” Kusanyiko!

WAABUDU wote mlio wakf na Wakristo wa Yehova Mungu, sikieni! Vilevile sikieni ninyi nyote mnaopendezwa na kujua mengi zaidi juu ya Mungu na Biblia! Nyote mnakaribishwa mhudhurie “Utumishi Mtakatifu” Kusanyiko la Wilaya litakalofanywa ulimwenguni pote mwaka huu wa 1976. Mwaka jana, kulingana na sehemu sehemu za ripoti zilizopokewa kutoka nchi 36, watu wasiopungua 2,375,681 walihudhuria. Ni wangapi watakaohudhuria mwaka huu? Je! wewe utakuwa mmoja wao? Utapata baraka nyingi sana ukiwa mmoja!

Kusanyiko hili litatoa chakula cha kiroho kinachokufaa hasa. Kila siku itaelekea upande mmoja wa utumishi mtakatifu wa Mkristo. Kichwa cha siku ya kwanza ni “Utumishi Mtakatifu kama Jamaa.” Programu hii itazungumza matatizo ya jamaa na itaonyesha yanayotakiwa kwa waume na wake wa Kikristo. Hasa vijana wote watafaidika na hotuba “Vijana Wataka Nini Maishani?”

“Utumishi Wake Mtakatifu Kundini” ndicho kichwa cha siku ya pili. Kuhitaji kwetu tengenezo la Yehova kutakaziwa. Pia, itakaziwa vile wazee wanavyoweza kushirikiana pamoja na vile wote wanaweza kupata faida zaidi kutokana na ziara ya mwangalizi wa mzunguko. Kama kawaida, ubatizo utakuwako siku hii, na hotuba yake yasema “Ubatizo Wafungua Mlango wa Utumishi Mtakatifu.”

Kichwa cha siku ya tatu kitakuwa “Utumishi Mtakatifu Shambani.” Tutatiwa moyo tufanye mahubiri yetu shambani yawe ya Kibiblia zaidi. Itazungumzwa pia vile tunavyoweza kutumia nafasi zetu kwa ukamili, na vilevile namna ya kuwa na matokeo zaidi tunapofanya wanafunzi na pendeleo letu kutumia wakati zaidi tukitoa ushuhuda.

“Kuvumilia Katika Utumishi Mtakatifu” ndicho kichwa cha siku ya nne ambayo ndiyo mwisho wa kusanyiko. Uhitaji wa kuendeleza nia ya akili inayofaa juu ya wakati utakaziwa. Pia, itakaziwa vile tunavyoweza kusimama imara katika imani na vile sala inavyoweza kutusaidia. Hotuba ya watu wote “Je! Kumtumikia Yehova Kutatatua Matatizo Yako?” itasaidia sana watu wa nje na hasa wale walioanza kupendezwa karibuni. Kusanyiko litamalizika na hotuba mbili zinazopaswa kutufanya tuthamini zaidi mambo mema yote tuliyosikia na kutusisimua tuchukue hatua juu ya mambo ambayo tumejifunza.

Sehemu mpya ya kusanyiko hili itakuwa ile ya kuanzia siku ya pili na kuendelea, maana programu itaanza kwa kurudia kujikumbusha mambo makuu ya siku iliyotangulia. Kila siku kutakuwa na mchezo wa kuigiza, na miwili itakuwa juu ya matukio ya Kibiblia na miwili itakuwa na vikao vya kisasa. Kabla ya kusanyiko, inapendekezwa msome Wafalme wa Pili sura 22 na 23, na Danieli sura 1 na 3.

Je! wewe wauona uhitaji wako wa kiroho? (Mt. 5:3) Basi jitahidi kabisa, uhudhurie “Utumishi Mtakatifu Kusanyiko.”

MAHALI PA KUSANYIKO

Kusanyiko litafanyiwa Nairobi. Wanaotaka mahali pa kulala wakati wa kusanyiko wanaweza kuomba fomu ya Mahali pa Kulala na anwani ya idara ya mahali pa kulala katika kundi la kwao la Mashahidi wa Yehova, au kutoka afisi ya tawi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki