Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 5/15 uku. 3
  • Vijana Waigeukia Dini—kwa Sababu Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vijana Waigeukia Dini—kwa Sababu Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Habari Zinazolingana
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vijana Hupendezwa na Dini Kadiri Gani?
    Amkeni!—1998
  • Je! Dini Yoyote Ni Nzuri vya Kutosha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kuzoea Dini Safi Kwa Ajili Ya Kuokolewa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 5/15 uku. 3

Vijana Waigeukia Dini​—kwa Sababu Gani?

‘‘TUKIO geni sana,” ndivyo watu wengine wanasema. Wanasema juu ya vijana wanaozidi kuongezeka ambao karibuni wameigeukia dini duniani pote. Katika nchi za Magharibi (za Wazungu), maelfu ya vijana wanahusika na kinachoitwa “mapindunzi ya Yesu.” “Maguru kadha wa kadha na madhehebu yamepata waamini kutoka watu wa kila namna. Katika nchi za Mashariki (za Asia) ni jambo la kawaida sana kuona vijana wamebeba Biblia zao wakienda kanisani Jumapili badala ya kwenda matembezi. Katika Hong Kong, vikundi vingi tofauti tofauti vya vijana vimefanywa ili vipate kuwa na shirika pamoja, na kuwa na mazungumzo ya Biblia na labda kugawa trakiti zilizochapwa na mashirika ya Biblia.

Ni kitu gani kimetokeza juhudi hii ya kidini? Haziwezi kuwa shule za kidini, kwa kuwa kama inavyoripotiwa, mafunzo ya dini kwa kawaida ni yenye kuchosha na hayana maana. Tofauti yake, inaonekana ni kwa sababu ya uhakika wa kwamba, ulimwenguni pote, vijana wanaona kwamba kupenda mali za kimwili, serikali za kibinadamu na mipango yao imetokeza pupa, choyo, vita, huzuni na utupu wa namna zote. Wengi wamejaribu dawa za kulevya, uasherati na vileo, walakini hawakupata suluhisho. Basi wanageukia dini wakiwa na tumaini, lakini mara nyingi si dini ya jamaa zao.

Huku kugeukia dini kwa ghafula na badiliko la njia ya maisha mara nyingi kunahangaisha sana wazazi au washiriki wengine wa jamaa. Mara nyingine wana sababu nzuri ya kufanya hivyo, kwa kuwa vikundi vingine vya kidini huongoza waamini vijana waache jamaa na rafiki zao zote, watoe fedha zao zote kwa vikundi hivyo, kisha wajitenge kwa kuishi pamoja mbali na ulimwengu. Katika nchi za Mashariki (za Asia), wazazi wanapendelea zaidi kuona watoto wao wakifuatia kitu fulani chenye faida za kimwili, kama vile masomo zaidi na kazi za kulipwa fedha nyingi.

Ikiwa wewe ni kijana, ungeonaje na ungefanyaje ikiwa washiriki wengine wa jamaa wangepinga kwa ghafula imani yako ya kidini? Je! tofauti katika dini au hata upinzani unamaanisha kwamba lazima kuwe kutopatana katika uhusiano (ushirikiano) wa jamaa? Hapana. Lakini ili kujibu maulizo hayo vizuri, kwanza ni lazima uwe na dini ya kweli, na uwe na mambo ya hakika ya kuhakikisha hilo. Sababu ni kwamba dini ya kweli peke yake, dini ya Biblia, ndiyo inayofanyiza watoto bora na kuonyesha mtu namna ya kupata uhusiano (urafiki) wa karibu zaidi pamoja na wazazi na washiriki wengine wa jamaa. Katika Biblia, mwanzishi wa jamaa, Muumba wa wanadamu, Yehova, anatoa mafundisho mengi juu ya namna ya kupata jamaa zenye umoja na furaha kweli kweli.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki