Bei ya Njaa
Watu wasiopungua milioni 30 ulimwenguni pote wanakufa njaa kila mwaka, kulingana na gazeti Guardian la Manchester, Uingereza. Na ili kununua chakula kinachotosha kuwaokoa, jumla ya dola 12,000,000,000 zinahitajiwa. Ingawa mataifa yanatatizwa sana kuweza kupata jumla ya pesa hizo ili kuokoa wenye njaa, “jumla iyo hiyo ya pesa inatumiwa kutengeneza silaha za vita katika muda wa siku 10,” linasema gazeti Guardian. Kweli hizi “siku za mwisho” ni zenye “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.”—2 Timotheo 3:1, NW.