Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 4/15 kur. 4-7
  • Biblia na Adili ya Utineja

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia na Adili ya Utineja
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwapa Vijana Mwongozo wa Kiadili
  • Kusaidia Vijana Wawe na Hofu kwa Yehova
  • Maoni Yenye Usawaziko Juu ya Ngono na Ndoa
  • Kufanya Vijana “Wawe Wenye Hekima kwa Ajili ya Wokovu”
  • Wazazi Walindeni Salama Watoto Wenu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Ngono—Ni Shauri Gani Hasa Lihalofaa?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Kuukabili Huo Ugumu
    Amkeni!—1997
  • Je! Ni Busara Kutofanya Ngono Kabla ya Kufunga Ndoa?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 4/15 kur. 4-7

Biblia na Adili ya Utineja

“Inaonekana kama kwamba vijana-matineja ndio wamerithi ulimwengu ulio mbaya zaidi kati ya maulimwengu yote yawezekanayo kuhusiana na kuachiwa wazi ujumbe mbalimbali unaohusu ngono: Sinema, muziki, redio na TV zinawaambia kwamba ngono ni mahaba yenye kusisimua, yenye kufurahisha, yenye kunyegeresha . . . Na bado, wakati ule ule, vijana wanapashwa habari kwamba wasichana wema wanapaswa kukataa.”​—Taasisi ya Alan Guttmacher.

VIJANA wa leo wamekua wakiwa katika muda wa mashaka-mashaka ya kutojua la kufanya na adili. Ingawa hivyo, Biblia inatoa mwelekezo wa wazi, usio wa mashaka-mashaka juu ya adili ya ngono. Ingawa programu za elimu ya ngono zinaelekea kukaza fikira juu ya kuepuka mimba, Biblia inaonyesha kwamba kitu chenyewe kilicho cha kuepukwa ni ngono kabla ya ndoa. “Mnaweza kuwa na uhakika kabisa kwamba hakuna mtu ambaye anajiingiza hasa katika uasherati [ambao unatia ndani ngono kabla ya ndoa] au ukosefu wa utakato au ngono za ovyo-ovyo . . . anaweza kurithi cho chote cha ufalme wa Mungu,” inasema Biblia. (Waefeso 5:5, The Jerusalem Bible) Kwa uwazi, uhusiano wa kingono unapasa kuzuiliwa uwe ndani ya ndoa tu.

Hivyo, jibu kwa tatizo la mimba za utineja si kufundisha vijana njia za kuzuia mimba, bali ni kuwapa mwongozo wa kiadili na kiroho. Biblia inaelewesha wazi ni daraka la nani kutoa mwongozo huo: “Akina baba, msiwe mkiwaudhi watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova.”​—Waefeso 6:4, NW.

Ingawa hivyo, katika uchunguzi mmoja vijana waliombwa ‘wakadirie ubora wa wazazi wao kuanzia kiwango cha kuwa wasioridhisha mpaka kiwango cha kuwa wenye kuridhisha sana wakiwa vyanzo vya utoaji habari za ngono. Vijana-wabalehe walikadiria mama zao sana-sana kuwa wenye kuridhisha kidogo. Akina baba walikadiriwa kuwa wenye kukosa sana kuridhisha.” Basi, je! inafaa kutazamia wazazi wawape watoto wao mwelekezo juu ya mambo ya ngono?

Kuwapa Vijana Mwongozo wa Kiadili

Katika Mithali 4:1-4 (NW), Mfalme Sulemani anahimiza vijana hivi: “Sikilizeni, O wana, nidhamu ya baba . . . Kwa maana mimi nilithibitika kuwa mwana halisi kwa baba yangu, mwororo na aliye mmoja tu mbele ya mama yangu. Na yeye [baba] alikuwa akiniagiza mimi na kuniambia: ‘Moyo wako na upate kushika maneno yangu kwa uthabiti.’ “Ni wazi kwamba Sulemani aliweza kuzungumzia hata mambo ya usiri pamoja na baba yake; Sulemani mwenyewe anaendelea kuzungumzia ukosefu wa adili katika ngono kwa kutoboa mambo wazi sana.​—Mithali 5:1-19.

Miongoni mwa Mashahidi wa Yehova, jamaa nyingi zinadumisha mazungumziano ya wazi hivyo pamoja na watoto wao—tena mafanikio ni makubwa! Wao hawafanyi tu kuambia watoto wao “Hapana!” kuhusu uhusiano wa kingono. Biblia inawasaidia wawape watoto wao sababu zinazofaa za kuepuka ngono za ovyo-ovyo. Fikiria, tena, maneno ya Sulemani. Kwenye Mithali 5:3, 4, yeye anawatia moyo wanaume vijana waepuke kufanya ngono pamoja na malaya. “Midomo ya malaya hudondoza asali, na kinywa chake ni laini kuliko mafuta.” Ndiyo, huenda tazamio la ukosefu wa adili likaonekana kuwa la kushawishi sana. Hata hivyo, Sulemani anaonya hivi: “Mwisho wake ni mchungu kuliko pakanga; ni mkali kama upanga wa makali kuwili.”

Kama Sulemani, wazazi wanaweza kusababiana pamoja na watoto wao juu ya matokeo ya uhusiano wa kingono. Dhamiri yenye masumbufu, mimba zisizotakwa, magonjwa yenye kuambukizwa kupitia ngono kama vile UKIMWI—hayo ni malipo machungu ya dakika chache za raha yenye kushawishi. Sulemani anazidi kuhimiza sana vijana ‘wasiwape wengine fahari yao.’ (Mithali 5:9, NW) Je! haionyeshi ukosefu wa kujiheshimu kijana akijipa mwenyewe, awe ni wa kiume au wa kike, kwa mtu fulani asiyependezwa na ndoa? Je! hainyenyekezi mtu kutumikia akiwa njia tu ya kutosheleza harara za ubinafsi zake mwenyewe au za mtu mwingine? Wazazi wanaweza kusaidia watoto wao wathamini mambo haya ya hakika.

Sulemani alitoa mashauri zaidi juu ya kushughulika na mtu aliye mkosefu wa adili: “Pita mbali kabisa usiwe kando ya [mwanamke] huyo, na usiwe karibu na mwingilio wa nyumba yake.” (Mithali 5:8, NW) Vivyo hivyo, wazazi wanaweza kuwapa vijana mashauri yenye mafaa katika kuepuka mazingira yenye kuwaachisha msimamo unaofaa. Wanaweza kuwahimiza wasifanye matembezi ya kirafiki pamoja na watu wasiofuata kanuni. Na wakati watakapofikia hatua ya kustahili kufuatia uchumba, wanaweza kutiwa moyo kuchukua hatua zenye mafaa kuepuka mwenendo wenye dhambi. Mathalani, wale wawili wenye kuchumbiana wangeweza kupanga mtu fulani aandamane nao sikuzote katika matembezi yao ya kirafiki. Je! hayo ni mambo ya kizamani? Labda. Lakini ni afadhali kuchukua hatua za nadhari inayofaa kuliko ‘kulazimika kupiga kite katika wakati ujao wako ambapo mnofu wako na oganizimu yako vinakuja kwenye mwisho. Na wewe utalazimika kusema: ‘Mimi nimechukia nidhamu kama nini . . . Nami nimekuwa sikusikiliza sauti ya waagizaji wangu.’”​—Mithali 5:11-13, NW.

Kusaidia Vijana Wawe na Hofu kwa Yehova

Kulingana na makadirio fulani, kuna vijana zaidi ya milioni 12 wenye kufanya ngono katika United States tu. Hata lile ambukizo kubwa la UKIMWI halijazuia sana wimbi hilo la ukosefu wa adili. Hata hivyo, Mashahidi wa Yehova wanajaribu kukaza kikiki katika watoto wao jambo lenye uvutano mwingi kuliko hofu ya UKIMWI au ya kupata mimba: hofu yenye afya juu ya Yehova Mungu. Sulemani anakumbusha vijana kwenye Mithali 5:21 (NW) hivi: “Kwa maana njia za mwanadamu ziko mbele ya macho ya Yehova, na yeye anafikiria sana mapito yake yote.” John, mmoja wa Mashahidi wa Yehova na baba wa watoto wanne, anatoa shauri hili: ‘Kinachosaidia ni watoto kuwa na hofu yenye upendo kwa Yehova. Usiogope kuacha mtoto wako ajue kwamba Yehova anaweza kusikitishwa na vitendo vyetu vya ubinafsi.’ —Linganisha Mithali 27:11.

Bila shaka, ili hofu kwa Mungu iwe kizuizi chenye matokeo cha ukosefu wa adili, lazima Mungu awe halisi sana kwa kijana. (Linganisha Waebrania 11:27.) Wazazi wanaweza kusaidia watoto wao wasitawishe uhusiano wa kikweli pamoja na Mungu kupitia funzo la ukawaida la Biblia, sala ya kila siku, na kujionea wenyewe mambo ya maisha. Wakati kijana anapokuja kuthamini kwamba Mungu anamjali, atasukumwa kuepuka mwenendo ambao ungeweza kumchukiza Yeye. — 1 Petro 5:7, NW.

Jambo la kupendeza ni kwamba, uhusiano wa kijana pamoja na Mungu unaweza pia kusaidia kujazia mahitaji fulani yasiyotimizwa katika vijana wengine wengi. Mathalani, wastadi wanadai kwamba ngono za ovyo-ovyo kwa kawaida ni njia ya vijana ya kupambana na hisia za kujiona hoi au za ukosefu wa kujiheshimu Ingawa hivyo, hisia hizo hazihitaji kupata mtu aliye na urafiki pamoja na Yehova! Kijana kama huyo anaweza kusema: “Mungu ni msaidiaji wangu; Yehova yumo miongoni mwa wale wanaotegemeza nafsi yangu.”​—Zaburi 54:4, NW.

Maoni Yenye Usawaziko Juu ya Ngono na Ndoa

Bila shaka, wazazi hawataki watoto wao wasitawishe maoni ya ubaridi mwingi mno au ya mwelekeo hasi kuhusu mahusiano ya kingono. Ingawa Biblia inashutumu uasherati, pia inaonyesha kwamba mambo ya usiri wa ngono yanaweza kufurahisha sana—yaani, ndani ya ule muundo wa ndoa. Akitumia lugha ya kishairi, Sulemani anaongezea hivi: “Acha chanzo cha maji yako kithibitike kuwa kibarikiwa, na ushangilie pamoja na mke wa ujana wako . .. Acha matiti yake mwenyewe yakurushe akili nyakati zote. Kwa upendo wake wewe na upate kuwa katika mzumbao daima.”​—Mithali 5:18, 19, NW.

Kwa kufikiria maoni haya yaliyotukuka kuhusu ngono katika ndoa, hakuna sababu kwa wazazi kuhisi kwamba kuzungumzia mambo ya usiri si jambo la uelekevu. Anasema hivi John (aliyerejezelewa hapo mapema): “Sikuzote sisi tunaongea nao kwa kusema wazi, kwa hiyo habari ya ngono si siri. Sisi tunakazia kwamba hiyo ni zawadi kutoka kwa Muumba, Yehova, ya kufurahiwa na mume na mke wakati unaofaa.” Anasema hivi baba mwingine wa wavulana wawili matineja: “Kuanzia miaka yao ya mapema, sisi tumezungumzia ngono pamoja nao kwa kutoboa mambo wazi. Tumejaribu kuwafundisha maoni yenye staha, yenye hadhi kuhusu upendo na ngono. Sisi tunadumisha mazungumziano yenye kuendelea.” Kwa kufaa, watoto Wao wamebaki wakiwa safi kiadili.

Kufanya Vijana “Wawe Wenye Hekima kwa Ajili ya Wokovu”

“Watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu,” akatabiri mtume Paulo. (2 Timotheo 3:13) Kwa njia hiyo viwango vya kiadili vitaendelea kushuka. Ngono za ovyo-ovyo na mimba za utineja zitaendelea kupata jamii.

Wazazi wenye kutii Mungu watageukia Biblia ili wafanye watoto wao ‘wawe wenye hekima kwa ajili ya wokovu.’ (2 Timotheo 3:15, NW) Ikiwa unang’amua kwamba wewe mwenyewe unahitaji kupewa maagizo katika Biblia, hisi ukiwa huru kuwasiliana na Mashahidi wa Yehova kwa kuandikia watangazaji wa gazeti hili. Wao watafurahi kukupangia upokee maagizo hayo bila malipo. Mashahidi wa Yehova wanaweza pia kukuandalia vichapo kama vile kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako.a Hicho kina habari za Kimaandiko ambazo zimesaidia maelfu ya vijana waiponyoke mitego ya ukosefu wa adili wa ulimwengu.

Ingawa hivyo, namna gani juu ya wasichana ambao tayari wamepatwa na ile tanzia ya mimba isiyo halali? Hali kama hizo hazikosi tumaini kamwe. Mungu ‘husamehe kwa njia kubwa’ mtu anayesikitishwa kikweli na mwenendo wake. (Isaya 55:7, NW) Ingawa mambo si rahisi mtu akiwa mzazi mseja, mmoja anaweza kufanikisha useja kwa kutumia kanuni za Biblia. Mwanamke mmoja kijana aliyepata watoto watatu nje ya ndoa kabla ya kuwa Mkristo amefanya jambo lilo hilo. Yeye anajitahidi kutumia Neno la Mungu katika jamaa yake. Kwa kushirikiana kwa ukaribu na kundi la Mashahidi wa Yehova, amepata faraja na tegemezo jingi. Yeye anasema: “Hakika ni vizuri ajabu kutumikia Mungu mwenye kusamehe sana, na kuwa na ndugu na dada ambao ni wenye uelewevu. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, mimi nahisi nikiwa safi na mwenye hali njema, kiroho na kimwili.”

Bila shaka, jambo lililo bora zaidi lingekuwa kuepuka matatizo ya ngono kabla ya ndoa pale mwanzoni. Inafurahisha kwamba maelfu ya vijana leo wanafanya hivyo kwa sababu wao wanafuata mashauri ya Biblia ambayo yanafaa kwa nyakati zote.

[Maelezo ya Chini]

a Kinatangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

[Blabu katika ukurasa wa 6]

Mashahidi wa Yehova wanajaribu kukaza kikiki katika watoto wao jambo fulani lenye uvutano mwingi kuliko hofu ya UKIMWI au ya kupata mimba: hofu yenye afya kwa Yehova Mungu

[Blabu katika ukurasa wa 6]

Kulingana na makadirio fulani, kuna zaidi ya vijana milioni 12 wenye kufanya ngono katika United States tu

[Picha katika ukurasa wa 5]

Wazazi wanaweza kudumisha mazungumziano yenye kuendelea pamoja na watoto kuhusiana na mambo ya ngono

[Picha katika ukurasa wa 7]

Vijana Wakristo wataepuka mwenendo unaoweza kuharibu uhusiano wao pamoja na Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki