Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 8/15 kur. 30-31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Kufaidika Kutokana na “Mpatanishi Mmoja kati ya Mungu na Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Agano Jipya la Mungu Lakaribia Kutimizwa
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 8/15 kur. 30-31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◻ Je! Yesu ndiye Mpatanishi kwa ajili ya Wakristo wapakwa-mafuta tu au kwa ajili ya aina ya binadamu wote, kwa kuwa 1 Timotheo 2:5, 6 yamnena kuwa ndiye “mpatanishi” yule “ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi [unaolingana, NW] kwa ajili ya wote”?

Biblia ina mafundisho ya msingi na hata kweli za kina kirefu, zilizo chakula kigumu cha kufanyia uchunguzi. Uchunguzi mmoja wa jinsi hiyo wahusisha fungu la Kristo akiwa Mpatanishi. Mtume Paulo aliandika hivi. “Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu, ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi [unaolingana, NW] kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake.”—1 Timotheo 2:5, 6.

Ili akili zetu zishike vizuri analosema Paulo, m lazima kwanza tuthamini kwamba Biblia yapanga wazi mahali pawili pa kuendewa na wanadamu waaminifu. (1) uhai mkamilifu katika paradiso ya kidunia itakayorudishwa na (2) uhai mbinguni kwa ajili ya “kundi dogo” la Kristo, hesabu yao ikiwa ni 144,000. (Luka 12:32; Ufunuo 5:10, 14:1-3) Jumuiya ya Wakristo hufundisha kwamba watu wema wote huenda mbinguni, huo ukiwa ni msimamo usiopatana na Maandiko ambao umevuruga maoni ya watu kwa ujumla, hivi kwamba Yesu aonwa kuwa mpatanishi kwa ajili ya watu wote hao. Ingawa hivyo, Biblia yaonyesha nini?

Neno la Kigiriki me·siʹtes, lenye kutumiwa kwa “mpatanishi,” lamaanisha ‘mmoja ambaye hujikuta akiwa kati ya vikundi viwili au pande mbili za wahusika.’ Huo ulikuwa ‘mtajo wa kisanifu wenye maana nyingi katika lugha ya kisheria ya Kihelleni.’ Profesa Albrecht Oepke (Theological Dictionary of the New Testament) asema kwamba me·siʹtes ulikuwa “mmoja wa mitajo ya kisanifu yenye maana za namna mbalimbali sana katika msamiati wa sheria ya [ki]Helleni.”

Lakini kwa nini Biblia yatumia mtajo wa kisheria kuhusu fungu la Yesu la kuwa mpatanishi? Kwa kupata mandhari ya nyuma, fikiria yale ambayo Paulo aliandika kuhusu Sheria ya Mungu waliyopewa Israeli wenye kukusanyika mbele ya Mlima Sinai: “Iliamriwa kwa utumishi wa malaika kwa mkono wa mjumbe [mpatanishi, NW]” (Wagalatia 3:19, 20) Mpatanishi huyo alikuwa Muesa. Alikuwa ndiye wakili wa kupatanisha kati ya Yehova na taifa la Israeli wa kimnofu. Wakili kwa ajili ya nini? Kwa ajili ya kusimamisha imara agano, au mkataba wa kisheria, kati ya Mungu na taifa hilo.a

Je! hii yamaanisha kwamba kuna maana fulani ya wazi ya kisheria yenye kuhusika katika fungu la Yesu akiwa Mpatanishi? Ndiyo. Angalia elezo la Paulo kwenye Waebrania 8:6. Baada ya kunena juu ya ile tabenakulo na viwakilishi vingine vya ufananishi vilivyokuwa chini ya agano la Sheria, yeye aliandika hivi. “[Yesu] sasa amepata huduma iliyo bora zaidi, kwa kadiri alivyo mjumbe wa agano lililo bora, lililoamriwa [lililosimamishwa imara kisheria, NW] juu ya ahadi zilizo bora.” “Agano lililo bora” lilikuwa agano jipya, lililochukua mahali pa agano lililopatanishwa na Musa. (Waebrania 8:7-13) Agano jipya ‘lilisimamishwa imara kisheria.’ Liliuweka msingi ili baadhi ya wafuasi wa Kristo, kuanza na mitume, wapate “mwingio ndani ya pale mahali patakatifu,” mbinguni kwenyewe. —Waebrania 9:24, 10:16-19, NW.

Kuna vionyeshi vingine pia vya hali ya kisheria ya fungu la Yesu akiwa Mpatanishi wa “agano jipya.” Akitoa maelezo juu ya ahadi ya Mungu kwenye Zaburi 110:4, Paulo aliandika hivi “Basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini [ndiye mwenye kutolewa awe rehani [enʹgy·os] wa agano lililo bora zaidi.” (Waebrania 7:22) Huu ndio utumizi pekee wa Kibiblia wa neno enʹgy·os. The New International Dictionary of New Testament Theology yasema “Mwenye kuwa enʹgy·os alidhamini kabisa kwamba wajibu wa kisheria ungetekelezwa.” Kwa hiyo Yesu akiwa Mpatanishi wa agano jipya atumikia akiwa rehani ya kisheria kwamba ‘tumaini lililo zuri zaidi’ lingetimizwa.—Waebrania 7:19.

Mahali penginepo Paulo atumia neno jingine lenye maana ya kisheria, ar·ra·bonʹ, lililotafsiriwa “arabuni.” Kamusi ile ile yaeleza hivi: “Neno la Kigiriki arrabōn . . . ni wazo la kisheria kutokana na lugha ya kikazi na ya kibiashara.” Angalia jinsi Paulo alivyoutumia mtajo huu wa kisheria “Yeye ambaye ametupaka mafuta ni Mungu. Pia yeye ametia muhuri wake juu yetu na ametupa sisi arabuni cha kile ambacho kitakuja, yaani, ile roho, katika mioyo yetu.” (2 Wakorintho 1:21,22, NW) Sehemu mbili hizo zote ambapo ar·ra·bonʹ lapatikana zahusu pia upakwa mafuta ambao Mungu awafanyia Wakristo kwa roho, akiwaletea ‘thawabu au urithi wa milele katika mbingu’ wakiwa wana-roho wa Mungu.—2 Wakorintho 5:1, 5, Waefeso 1:13, 14; ona Kingdom Interlinear Translation of the Greek Scriptures.

Basi, ni wazi kwamba agano jipya si mpango mlegevu tu ulio wazi kwa aina ya binadamu wote. Ni uandalizi wa kisheria uliofanywa kwa uangalifu, ambao unahusisha Mungu na Wakristo wapakwa-mafuta.

Hii yapasa kutusaidia tuelewe 1 Timotheo 2:5, 6. Hapa rejezo lenye kuhusu “mpatanishi” lilifanywa baada ya mara zile nyingine tano za kutukia kwa neno hilo katika barua zilizoandikwa mapema kidogo. Kwa sababu hiyo, ingetazamiwa kuwa Timotheo aliuelewa upatanishi wa Yesu kuwa ni fungu ambalo Yeye analo kuhusiana na agano jipya. The Pastoral Epistles, kilichotungwa na Dibelius na Conzelmann, chakiri kwamba kwenye 1 Timotheo 2:5 ‘mtajo “mpatanishi” una maana ya kisheria,’ na “ingawa katika kifungu hiki, kwa utofautiano na Ebr 8:6, [agano] halitajwi, hata hivyo ni lazima mtu ajichukulie mapema kwamba anayemaanishwa ni ‘mpatamshi wa agano,’ kama zionyeshavyo habari zenye kuzunguka.” Profesa Oepke aonelea kwamba 1 Timotheo 2.5 yamwonyesha Yesu akiwa “mwakilishi wa kesi na mshauriani wa kutengeneza mapatano.”

Huenda kielezi cha ki-siku-hizi kikasaidia kuelewesha wazi jambo hili, hasa ikiwa wewe si Mkristo mpakwa-mafuta kwa roho. Fikiria kesi ya kisheria ambamo mwakilishi wa kesi ahusika. Fungu lake huenda lisifanane kwa kadiri kubwa sana na lile la mwanasheria anayebishania haki kama vile ambavyo lingefanana na la mtu anayepatanisha au kutimiliza mkataba wa kisheria wenye kukubalika na wenye manufaa kwa pande mbili zinazohusika. Bila shaka, wewe haumo katika hiyo kesi ya kisheria, kwa hiyo katika maana hiyo yeye hakutumikii wewe akiwa mwakilishi wa kesi yako. Hata hivyo huenda yeye akawa ni rafiki yako wa karibu ambaye kwa njia nyinginezo hukupa msaada wenye thamani.

Nyakati fulani kazi ya mwakilishi wa kesi katika kesi kama hiyo ya kisheria huwa na matokeo yenye kunufaisha wengine wengi. Ndivyo ilivyo kuhusu mambo ambayo Yesu atimiza kisheria akiwa Mpatanishi wa agano jipya. Mambo hayo yatokeza kitu ambacho agano la Sheria halikutokeza, “ufalme wa makuhani” wa kimbingu. (Kutoka 19:6; 1 Petro 2:9) Wakristo wapakwa-mafuta katika Ufalme watafanya kazi pamoja na Yesu wakiwa mbinguni ili kuleta mubaraka kwa “mataifa yote ya dunia.”—Mwanzo 22:18.

Watu wa mataifa yote walio na tumaini la uhai wa milele duniani watanufaika hata sasa kutokana na utumishi mbalimbali wa Yesu. Ingawa yeye si Mpatanishi wao wa kisheria, kwa maana hawamo katika agano jipya, yeye ndiye njia yao ya kumfikia Yehova. Kristo alisema: “Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.” (Yohana 14:6) Ni lazima wote watakaopata uhai duniani waelekeze sala zao kwa Yehova kupitia Yesu. (Yohana 14:13,23, 24) Yesu atumikia pia akiwa Kuhani Mkuu mwenye huruma awezaye kutumia manufaa za dhabihu yake kwa ajili yao, akiwaruhusu wapate msamaha na wokovu wa hatimaye. — Matendo 4:12; Waebrania 4:15.

Basi, 1 Timotheo 2:5, 6 haitumii “mpatanishi” katika ile maana pana iliyo ya kikawaida katika lugha nyingi. Haisemi kwamba Yesu ni mpatanishi kati ya Mungu na aina ya binadamu wote. Bali, yarejezea Kristo akiwa Mpatanishi (au “mwakilishi wa kesi”) wa agano jipya, hii ikiwa ndiyo njia isiyohusisha hali nyingi sana ambayo Biblia yatumia mtajo huo. Pia Yesu ni ukombozi unaolingana kwa ajili ya wote walio katika agano hilo, Wayahudi na Wasio Wayahudi pia, ambao watapokea mbinguni uhai usiokufa. Mtume Yohana aliwarejezea hao kwenye 1 Yohana 2:2. Lakini alionyesha kwamba wengine pia watapokea manufaa ya dhabihu ya Kristo “Naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.”

Wale wa ‘ulimwengu wote’ ni wote ambao watapata uhai wa milele katika paradiso ya kidunia itakayorudishwa. Sasa mamilioni ya watumishi hao wakubaliwa wa Mungu wana tumaini hilo la kidunia. Wao wamwona Yesu kuwa Kuhani Mkuu na Mfalme wao, ambaye wao waweza kumfikia Yehova kila siku kupitia yeye. Wao wategemea ukombozi wa Yesu, uliopo kwa utumizi wao, sawa na vile itakavyokuwa kwa watu kama Abrahamu, Daudi, na Yohana Mbatizaji wafufuliwapo. (Mathayo 20:28) Hivyo, dhabihu ya Kristo itaiongoza aina ya binadamu wote watiifu kwenye uhai wa milele.

[Maelezo ya Chini]

a Zungumzo la maagano limo katika Mnara wa Mlinzi wa Februari 1, 1989, kurasa 10-20.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Hapa penye Mlima Sinai, Musa alitumikia akiwa mpatanishi wa agano la Sheria

[Hisani]

Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki