Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 3/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Agano Jipya la Mungu Lakaribia Kutimizwa
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Kufaidika Kutokana na “Mpatanishi Mmoja kati ya Mungu na Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Mtakuwa “Ufalme wa Makuhani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Agano
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 3/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Waebrania 9:16 husema kwamba ni lazima aliyelifanya agano afe ili agano liwe na nguvu. Lakini Mungu ndiye alifanya agano jipya, naye hakufa. Kwa hiyo twaweza kuelewaje mstari huo?

Twasoma kwenye Waebrania 9:15-17: “Na kwa sababu hii [Kristo] ni mjumbe wa agano jipya, ili, mauti ikiisha kufanyika kwa kukomboa makosa yaliyokuwa chini ya agano la kwanza, hao walioitwa waipokee ahadi ya urithi wa milele. Maana agano la urithi lilipo, lazima iwepo mauti yake [mwanadamu] aliyelifanya. Kwa maana agano la urithi lina nguvu palipotukia kufa kwa mtu; kwa kuwa halina nguvu kabisa, akiwa yu hai yeye [mwanadamu] aliyelifanya.”a

Yehova ndiye Mfanyi hasa wa agano jipya. Kwenye Yeremia 31:31-34, Mungu alitabiri mahususi kwamba yeye mwenyewe angefanya hilo agano jipya pamoja na watu wake. Mtume Paulo anukuu andiko hilo kwenye Waebrania 8:8-13, inayoonyesha kwamba Paulo alitambua kwamba Mungu mwenyewe, ndiye alianzisha agano hilo la kimungu.

Hata hivyo, katika Waebrania sura 9, Paulo aliendelea kushughulika na madaraka mbalimbali ya Yesu kuhusiana na agano jipya. Kristo alikuja akiwa Kuhani Mkuu wa agano hilo. Kwa upande mwingine, Yesu alikuwa ndiye dhabihu ya agano jipya; ni “damu yake Kristo” pekee iwezayo ‘kusafisha dhamiri zetu na matendo mafu.’ Kristo alikuwa pia Mpatanishi wa agano hilo, sawa na Musa alivyokuwa mpatanishi wa agano la Sheria.—Waebrania 9:11-15.

Paulo alitaja kwamba kifo kilihitajiwa ili kuhalalisha maagano kati ya Mungu na wanadamu. Agano la Sheria ni mfano mmoja. Musa alikuwa mpatanishi walo, mwenye kufanyiza mwafaka huo kati ya Mungu na Israeli ya kimnofu. Hivyo Musa alikuwa na daraka la maana naye alikuwa ndiye mwanadamu aliyeshughulika na Waisraeli walipokuwa wakiingia katika agano hilo. Hivyo Musa angeweza kuonwa kuwa mfanya agano wa kibinadamu wa agano la Sheria lililoanzishwa na Yehova. Lakini je, Musa alihitaji kumwaga damu yake ya uhai ili agano la Sheria liwe na nguvu? La. Badala yake wanyama walitolewa, damu yao ikiwa badala ya damu ya Musa.—Waebrania 9:18-22.

Vipi lile agano jipya kati ya Yehova na taifa la Israeli ya kiroho? Yesu Kristo alikuwa na daraka tukufu la kijumbe, Mpatanishi kati ya Yehova na Israeli ya kiroho. Ingawa Yehova ndiye alianzisha agano hilo, lilimtegemea Yesu Kristo. Zaidi ya kuwa Mpatanishi walo, Yesu alishughulika moja kwa moja katika mnofu na wale ambao wangekuwa wa kwanza kuingizwa katika agano hilo. (Luka 22:20, 28, 29) Isitoshe, alistahili kuandaa dhabihu iliyohitajiwa ili kuhalalisha agano hilo. Dhabihu hiyo haikuwa ya wanyama tu bali ya uhai mkamilifu wa kibinadamu. Kwa hiyo Paulo angeweza kumrejezea Yesu kuwa mfanya agano wa kibinadamu wa agano jipya. Baada ya ‘Kristo kuingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu,’ agano jipya likawa halali.—Waebrania 9:12-14, 24.

Katika kusema kuhusu Musa na Yesu kuwa wafanya agano wa kibinadamu, Paulo hakuwa anadokeza kwamba yeyote kati yao alikuwa ameanzisha maagano hayo moja moja, ambayo kwa kweli yalikuwa yamefanywa na Mungu. Bali, wanadamu hao wawili wakiwa wapatanishi walihusika kwa ukaribu sana katika kufanyiza maagano hayo moja moja. Na katika kila kisa, kifo kilihitajiwa—wanyama wakiwa badala ya Musa, na Yesu akitoa damu ya uhai wake mwenyewe kwa ajili ya wale walio katika agano jipya.

[Maelezo ya Chini]

a Maneno mawili ya Kigiriki yaliyotumiwa hapa kuwa ‘mfanya agano’ hufasiriwa kihalisi kuwa “-a (yule) aliyejifanyia mwenyewe agano” au “-a (yule) anayefanya agano.”—The Kingdom Interlinear Translation of the Greek Scriptures, kilichotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc., na The Interlinear Greek-English New Testament, cha Dr. Alfred Marshall.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki