Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 3/15 kur. 8-9
  • Ishara ya Siku za Mwisho

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ishara ya Siku za Mwisho
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Mitume Waomba Ishara
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • “Ni Nini Itakayokuwa Ishara ya Kuwapo Kwako?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Sababu Hatukuambiwa “Siku Ile na Saa Ile”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Ishara ya Siku za Mwisho
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 3/15 kur. 8-9

Maisha na Huduma ya Yesu

Ishara ya Siku za Mwisho

Kufikia sasa ni alasiri ya Jumanne. Yesu akiwa ameketi juu ya Mlima wa Mizeituni, akitazama hekalu lililo chini, Petro, Andrea, Yakobo, na Yohana wamjia kwa faragha. Wao wahangaikia hekalu, kwa kuwa Yesu ndipo tu ametabiri kwamba ‘ndani yalo hamna jiwe ambalo litaachwa juu ya jiwe.’

Lakini kwa wazi wao wana mengi zaidi katika akili zao wakaribiapo Yesu. Majuma machache mapema kidogo, yeye alikuwa amenena juu ya “kuwapo” kwake, wakati “ambapo Mwana wa binadamu apaswa kufunuliwa.” Na katika pindi ya mapema kidogo, alikuwa amewaambia juu ya “umalizio wa mfumo wa mambo.” Kwa hiyo mitume wana hamu ya kuulizia sana.

“Tuambie,” wao wasema, “mambo hayo [yenye kutokeza uharibifu wa Yerusalemu na hekalu lao] yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” Kwa kweli, swali lao ni la sehemu tatu. Kwanza, wao wataka kujua juu ya mwisho wa Yerusalemu na hekalu lao, halafu kuhusu kuwapo kwa Yesu katika mamlaka ya Ufalme, na hatimaye juu ya mwisho wa mfumo mzima wa mambo.

Katika jibu lake refu, Yesu ajibu sehemu zote tatu za swali hilo. Yeye aandaa ishara ambayo yatambulisha wakati mfumo wa mambo ya Kiyahudi utaisha; lakini aandaa zaidi. Pia atoa ishara ambayo itawaweka chonjo wanafunzi wake wa wakati ujao kwamba wanaishi wakati wa kuwapo kwake na karibu na mwisho wa mfumo mzima wa mambo.

Miaka ipitapo, mitume waanza kuona utimizo wa unabii wa Yesu. Ndiyo, mambo yale yale aliyotabiri yaanza kutukia katika siku yao. Hivyo, Wakristo walio hai miaka 37 baadaye, katika 70 W.K., hawashtukiwi na uharibifu wa mfumo wa Kiyahudi na hekalu lao.

Hata hivyo, kuwapo kwa Kristo na umalizio wa mfumo wa mambo hakutukii katika 70 W.K. Kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme kwatukia baadaye sana. Lakini wakati gani? Ufikirio wa unabii wa Yesu wafunua hilo.

Yesu atabiri kwamba kutakuwako “vita na ripoti za vita.” “Taifa litainuka dhidi ya taifa,” na kutakuwako upungufu wa vyakula, matetemeko ya dunia, na magonjwa ya kipuku. Wanafunzi wake watachukiwa na kuuawa. Manabii wa bandia watainuka na kuongoza wengi vibaya. Kutotii sheria kutaongezeka, na upendo wa idadi iliyo kubwa zaidi utapoa. Wakati uo huo, habari njema za Ufalme wa Mungu zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ziwe ushahidi kwa mataifa yote.

Ingawa unabii wa Yesu ulikuwa na utimizo wenye mipaka kabla ya uharibifu wa Yerusalemu katika 70 W.K., utimizo wao mkubwa hutukia wakati wa kuwapo kwake na umalizio wa mfumo wa mambo. Pitio la uangalifu la matukio ya ulimwengu tangu 1914 hufunua kwamba unabii wa Yesu wenye matukio makubwa umekuwa ukipata utimizo mkubwa kuanzia mwaka huo.

Sehemu nyingine ya ishara ambayo Yesu atoa ni kuonekana kwa “kitu cha kunyarafisha kinachosababisha uharibifu.” Katika 66 W.K. kitu hiki cha kunyarafisha (cha kuchukiza) kilitokea kwa namna ya “majeshi yenye kupiga kambi” ya Roma ambayo yalizunguka Yerusalemu na kufukua ukuta wa hekalu. Hicho “kitu cha kunyarafisha” kilisimama kisipopaswa.

Katika utimizo mkubwa wa ishara, hicho kitu cha kunyarafisha ni Ushirika wa Mataifa na mwandamizi wao, Umoja wa Mataifa. Tengenezo hili la amani ya ulimwengu huonwa na Jumuiya ya Wakristo kuwa badala ya Ufalme wa Mungu. Lo, ni jambo la kunyarafu kama nini! Kwa hiyo, baada ya muda mamlaka za kisiasa zenye kushirikiana na UM zitageukia Jumuiya ya Wakristo (Yerusaiemu wa ufananisho) na kumwacha mkiwa.

Hivyo Yesu alitabiri kwamba: “Kutakuwako dhiki kubwa ya namna ambayo haijatukia tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa, la, wala haitatukia tena.” Ingawa uharibifu wa Yerusalemu katika 70 W.K. ulikuwa dhiki kubwa kweli kweli, kukiwa na watu zaidi ya milioni moja wenye kuripotiwa kuwa waliuawa, haukuwa dhiki kubwa kuliko Gharika ya duniani pote katika siku ya Noa. Kwa hiyo utimizo mkubwa wa kisehemu hiki cha unabii wa Yesu ungali utatimizwa. Mathayo 24:2-22; 13:40, 49; Marko 13:3-20; Luka 21:7-24; 19:43, 44; 17:20-30; 2 Timotheo 3:1-5, NW.

◆ Ni kitu gani chaharakisha swali la mitume, lakini kwa wazi ni kitu gani kingine walicho nacho katika akili zao?

◆ Ni sehemu gani ya unabii wa Yesu iliyotimizwa katika 70 W.K., lakini ni nini hakikutukia wakati huo?

◆ Unabii wa Yesu ulipata lini utimizo wa kwanza, lakini ni lini unapokuwa na utimizo mkubwa?

◆ Ni nini kitu cha kunyarafisha katika utimizo wacho wa kwanza na wa mwisho?

◆ Kwa nini dhiki kubwa haikuwa na utimizo wa mwisho kwa uharibifu wa Yerusalemu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki