Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 6/1 uku. 32
  • Usikose “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Usikose “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • “Tumaini Katika Yehova” Mkusanyiko wa Wilaya—Usiukose!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Usikose “Wasifaji Wenye Shangwe” Mkusanyiko wa Wilaya
    Amkeni!—1995
  • Hudhuria “Wapendao Uhuru” Mkusanyiko Wa Wilaya!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kwa Nini Yakupasa Uhudhurie “Ujitoaji Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 6/1 uku. 32

Usikose “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya!

Siku nne zenye kuthawabisha za maagizo ya Biblia zakungoja wewe. Uwepo wakati programu ianzapo saa 7:30 alasiri siku ya Alhamisi. Onea shangwe ile hotuba yenye kuamsha mawazo “Je! Rafiki Zako Ni Rafiki za Yehova?” na pia hotuba ya msingi, “Lugha Iliyo Safi kwa Mataifa Yote.” Hotuba ya kumalizia alasiri, “Kuokoa Uhai Wako kwa Damu—Jinsi Gani?,” itajibu swali hili: “Je! kweli damu yahitajiwa ili kuokoa uhai?

Kipindi cha Ijumaa asubuhi chaanza saa 3:30. Wewe na uwepo kunufaika na ile hotuba yenye kupekua mawazo, “Kristo ‘Alichukia Kutotii Sheria’—Je! Wewe Wakuchukia?” na ile hotuba yenye kuchochea, “Kataa Misisimuo ya Kilimwengu, Fuatia Mambo Halisi ya Ufalme.” Wakati wa alasiri, madokezo yenye kutumika juu ya njia za kuishi kulingana na uwezo wako wa kiuchumi yataandaliwa. Wazazi wataonyeshwa jinsi wao waweza kutimiza wajibu wao mbalimbali kwa matokeo, na drama ya ki-siku-hizi itatolea vijana mwongozo bora kabisa kuhusu kushiriki katika utendaji wa ziada shuleni baada ya masomo.

Kipindi cha asubuhi ya Jumamosi kitakazia hotuba juu ya wakfu na ubatizo, na pia kizungumzie uhitaji wa kufanya dhabihu ili kufanya funzo la kibinafsi la Biblia. “Gari-Vita la Kimbingu la Yehova Lasonga Mbele” ni hotuba yenye motisha katika programu ya alasiri. Pia, kutakuwako vikumbusha thabiti kuhusu daraka letu la Kikristo kusaidia wale waliopofushwa na dini bandia, na usaidizi wenye kutumika utatolewa ili kutimiza daraka hili.

Utataka kuwapo asubuhi ya Jumapili ili usikie ule ujumbe wenye nguvu nyingi utakaotolewa dhidi ya Jumuiya ya Wakristo na makasisi wayo. Hiyo itafuatwa na wonyesho wa drama ya mavazi kamili ikitegemea matukio yanayohusu maisha za Yehu na Yonadabu. Halafu, alasiri, hakikisha kuisikia hotuba ya watu wote, “Ungamanishweni na Lugha Iliyo Safi.”

Wakati wa Novemba na Desemba mikusanyiko imeratibiwa kotekote katika Afrika Mashariki, kwa hiyo kutakuwa na mmoja si mbali kutoka nyumbani kwako. Omba habari kwa Mashahidi wa Yehova wa kwenu ili ujue wakati na mahali pa ule ulio karibu kabisa na wewe.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki