Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 6/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Sheria Za Nani Utakazotanguliza?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Tembea Kama Ufundishwavyo na Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
    Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
  • Iweni Waaminifu kwa Mungu “Aonaye Sirini”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 6/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Ni kwa nguvu za kadiri gani Mkristo apaswa kukinza kutiwa kwa damu mishipani ambako kumeagizwa au kuruhusiwa na mamlaka ya mahakama?

Kila hali ni tofauti kabisa, hivyo basi hakuna mwongozo wa kisheria wenye kuhusisha mambo yote kuhusu jambo hilo. Wakristo wajulikana kwa “kumpa Kaisari yaliyo ya Kaisari” kwa heshima, wakiwa wanatii sheria za serikali ya kilimwengu. Hata hivyo, wao wang’amua kwamba wajibu wao mkubwa zaidi kumpa ‘Mungu yaliyo ya Mungu,’ si kuvunja sheria yake.—Marko 12:17.

Warumi 13:1-7, NW, yazungumza juu ya uhusiano wa Wakristo kwa “mamlaka za juu zaidi.” Serikali hizo zina mamlaka ya kutekeleza sheria au kutoa mielekezo, kwa kawaida kuendeleza hali njema ya ujumla ya halaiki ya watu. Na serikali ‘zauchukua upanga’ ili kutekeleza sheria zao na ‘kuonyesha hasira kisasi juu ya mtu anayezoea lililo baya kulingana na sheria zao.’ Wakiwa wenye kujitiisha kwa mamlaka za juu zaidi, Wakristo hutamani kutii sheria na amri za mahakama, lakini ujitiisho huo ni lazima uwe wa kadiri inayohusu. Ikiwa Mkristo aombwa anyenyekee kitu fulani ambacho kingekuwa mvunjo wa sheria ya juu zaidi ya Mungu, sheria ya kimungu huja kwanza; huchukua mahali pa kwanza.

Sheria fulani za ki-siku-hizi ambazo ni njema kwa msingi huenda zikatumiwa vibaya ili kutoa mamlaka ya kulazimisha Mkristo kutiwa damu mishipani. Katika kisa hicho ni lazima Wakristo wachukue msimamo ule ule ambao mtume Petro alichukua: “Ni lazima sisi tutii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.”—Matendo 5:29, NW.

Yehova aliwaamuru Waisraeli hivi: “Ila ujihadhari [uazimie kwa imara, NW] kwamba usile damu, kwani ile damu ndiyo uhai; na uhai usile pamoja na nyama.” (Kumbukumbu 12:23) Tafsiri ya Biblia ya Kiyahudi ya 1917 husomeka hivi: “Ila tu uwe thabiti katika kutokula damu.” Na Isaac Leeser aliutafsiri hivi mstari huo: “Ila tu uwe imara ili kutokula damu.” Je! hiyo yasikika kama kwamba watumishi wa Mungu wangechukua mambo hivi hivi tu au kujiachilia tu kwa habari ya kuunga mkono sheria yake?

Wakristo wamekuwa na sababu nzuri ya kupiga moyo konde kabisa kutii Mungu, hata ikiwa serikali inawaelekeza vingine. Profesa Robert L. Wilken aandika hivi: “Si kwamba tu Wakristo walikataa utumishi wa kijeshi [wa Kiroma] bali pia hawangekubali cheo cha umma wala kutwaa daraka lolote la kusimamia majiji.” (The Christians as the Romans Saw Them) Kukataa kungeweza kumaanisha kubandikwa jina la kuwa wavunja-sheria au kulaaniwa wapelekwe kwenye uwanja wa mapambano ya Kiroma.

Wakristo leo ni lazima pia wawe thabiti, waazimie kwa imara kutovunja sheria ya kimungu, hata ikiwa kufanya hivyo kwawatia katika hali fulani ya hatari kuhusiana na serikali za kilimwengu. Sheria iliyo ya juu kabisa ya ulimwengu wote mzima—sheria ya Mungu—yawataka waepuke kutumia damu vibaya, kama vile Wakristo waamriwavyo kuepuka uasherati (ukosefu wa adili katika ngono). Biblia huyaita makatazo hayo kuwa “yaliyo lazima.” (Matendo 15:19-21, 28, 29) Sheria hiyo ya kimungu haipasi kuchukuliwa kimchezo, kama jambo la kutiiwa ikiwa tu yafaa kufanya hivyo au kama haitokezi matatizo yoyote. Sheria ya Mungu ni lazima itiiwe!

Basi, twaweza kuthamini ni kwa nini msichana Mkristo aliyetajwa katika ukurasa wa 12 aliambia mahakama moja kwamba “aliona kutiwa damu mishipani kuwa ni kuuvamia mwili wake na akakulinganisha na kulala mwanamke kinguvu.” Je! mwanamke yeyote Mkristo, kijana au mzee, angejitiisha bila kujali sana alalwe kinguvu, hata ikiwa kuna ruhusa ya kisheria kwamba uasherati huo wa kulalwa kinguvu utekelezwe?

Vivyo hivyo, yule msichana wa miaka 12 aliyenukuliwa katika ukurasa ule ule hakuacha shaka lolote kwamba ‘yeye angepigana na kutiwa kokote kwa damu mishipani kwa mamlaka ya mahakama, kwa nguvu zote awezazo kupata, kwamba angepiga makelele na kujing’ang’ania, kwamba angekivuta kile chombo cha kudunga sindano kimtoke mkononi na angejaribu kuiharibu damu iliyo katika mfuko wenye kuning’inia juu ya kitanda chake.’ Yeye alikuwa ameazimia kwa imara kuitii sheria ya kimungu.

Yesu aliondoka kwenye eneo wakati umati wa watu ulipotaka kumfanya mfalme. Vivyo hivyo, ikiwa yaelekea kutakuwa na kutiwa damu mishipani kwenye kuruhusiwa na mamlaka ya mahakama, Mkristo angeweza kuchagua kuepuka kuingilika kwa mvunjo huo wa sheria ya Mungu. (Mathayo 10:16; Yohana 6:15) Wakati ule ule, Mkristo apaswa kwa hekima kutafuta matibabu badala, hivyo akifanya jitihada halisi kuendeleza uhai na kupata tena afya kamili.

Kama Mkristo angefanya jitihada za kujikakamua sana ili kuepuka mvunjo wa sheria ya Mungu juu ya damu, wenye mamlaka wangeweza kumfikiria kuwa mvunja-sheria au kumfanya astahili kushtakiwa. Ikiwa adhabu ingetokea, Mkristo huyo angeweza kuyaona hayo kuwa mateso kwa ajili ya uadilifu. (Linganisha 1 Petro 2:18-20.) Lakini katika visa vilivyo vingi, Wakristo wameepuka kutiwa damu mishipani na wakarudiwa na afya kwa kupata matibabu ya wenye ujuzi wa kutosha, hivi kwamba hakukutokea matatizo yoyote ya kisheria yenye kudumu. Na lililo la maana zaidi, wao wamedumisha uaminifu wao wa kimaadili kwa Mpaji-Uhai na Hakimu wao Wa Kimungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki