Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 7/15 kur. 4-7
  • Kwa Nini Hofu Imeshika Ulimwengu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Hofu Imeshika Ulimwengu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hofu ya Ulimwenguni Pote ina Umaana
  • Jambo Ambalo Ulimwengu Huu Waweza Kutazamia
  • Wakati wa Shangwe, Si wa Kuhofu
  • Sitawisha Moyo wa Kumhofu Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kuogopa Mungu Je! Kunaweza Kukunufaisha Wewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Hofuni Yehova na Kulitukuza Jina Lake Takatifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Kujifunza Kupata Furaha Katika Kumhofu Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 7/15 kur. 4-7

Kwa Nini Hofu Imeshika Ulimwengu?

NI NANI anayetaka kuishi kwa hofu? Mtu wa kawaida atamani usalama, bila uhai wake wala mali zake kutishwa. Kwa hiyo, wengi huhama maeneo yenye uhalifu mwingi. Lakini, visababishi vya hofu vipo kila mahali.

Hatari zitokanazo na silaha za nyukilia na aksidenti za mitambo ya nyukilia hufanya wanadamu wawe na hofu ya kuangamizwa. Jeuri yenye kuongezeka kasi huendeleza hofu. Wengi wanahofu kwamba UKIMWI utakuwa maradhi yenye kuua zaidi katika karne hii. Kuharibiwa kwa mazingira yetu ni miongoni mwa visababishi vingine vya hofu. Je! hofu hizo hasa zina umaana fulani? Na je, twaweza kupata kuwa na tumaini la kuishi katika ulimwengu bila hofu kama hiyo?

Hofu ya Ulimwenguni Pote ina Umaana

Hofu yenye kuenea leo ina umaana kwa sababu ya mambo yaliyotabiriwa katika Biblia. Katika unabii wake kuhusu siku za mwisho, Yesu Kristo alitaja hali ambazo zingetokeza hofu. Alisema hivi: “Taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.” Yesu alitaja pia “kuongezeka kwa maasi.” Tangu 1914, vita, njaa, matetemeko ya dunia, na uasi-sheria usio na kifani umetokeza hofu kuu na vifo vingi.—Mathayo 24:7-14.

Hata mitazamo ya watu inatokeza hofu leo. Kwenye 2 Timotheo 3:1-4, twasoma maneno ya kiunabii ya mtume Paulo: “Siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu.” Si ajabu kwamba kuna hofu nyingi sana leo kwa kuwa twazungukwa na watu kama hao katika hizi siku za mwisho!

Jambo Ambalo Ulimwengu Huu Waweza Kutazamia

Yesu alilinganisha kipindi hiki na zile siku za mwisho za ulimwengu wa wakati wa Noa. Bila shaka kulikuwa na hofu kubwa wakati huo, kwani masimulizi ya kihistoria ya Biblia yasema hivi: “Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia ikajaa dhuluma.” Kwa hiyo, “Mungu akamwambia [Noa], Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu, kwa sababu wameijaza dunia dhuluma.” (Mwanzo 6:11, 13) Ulimwengu huo mwovu ulikuwa na jeuri sana hivi kwamba Mungu aliumaliza kwa Furiko la duniani pote. Hata hivyo, kwa sababu ya upendo wake, Yehova Mungu alimhifadhi Noa mwadilifu pamoja na familia yake.—2 Petro 2:5.

Kwa hiyo, ulimwengu wa sasa wenye jeuri waweza kutazamia nini? Mungu huchukia kutojali hali-njema ya wengine kijeuri. Hilo lathibitishwa na maneno ya mtunga-zaburi: “Bwana humjaribu mwenye haki; bali nafsi yake humchukia asiye haki, na mwenye kupenda udhalimu.” (Zaburi 11:5) Yehova alikomesha ulimwengu wenye jeuri wa siku ya Noa. Basi, je, tusitazamie kwamba Mungu atakomesha ulimwengu huu uliojaa jeuri yenye kutokeza hofu?

Mtume Petro alipuliziwa kimungu aseme juu ya kuwapo kwa Kristo na kutabiri juu ya uharibifu wa ulimwengu mwovu wa sasa. Yeye aliandika: “Katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe, na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa.” Ndipo Petro akatumia neno “mbingu” kuwakilisha mfumo wa utawala usiokamilika juu ya wanadamu na neno “nchi” kuwakilisha jamii ya wanadamu wasio na uadilifu. “Maana,” akasema, “[wao] hufumba macho yao wasione neno hili ya kuwa zilikuwako mbingu tangu zamani, na nchi pia, imefanyizwa kutoka kwa maji, na ndani ya maji, kwa neno la Mungu; kwa hayo dunia ile ya wakati ule [siku ya Noa] iligharikishwa na maji, ikaangamia. Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu.”—2 Petro 3:3-7.

Akifuatia wazo ilo hilo, Paulo alitaja kwamba Kristo na malaika wake wenye nguvu wangelipiza “kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu; watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele.” (2 Wathesalonike 1:6-9) Kitabu cha mwisho cha Biblia chasema juu ya kukusanywa kwa mataifa kwa ajili ya “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” na kinatuhakikishia kwamba Yehova ‘ataharibu hao waiharibuo nchi.’—Ufunuo 11:18; 16:14-16.

Wakati wa Shangwe, Si wa Kuhofu

Badala ya kuhofishwa na yale yanayotabiriwa na Biblia juu ya ulimwengu huu, watu wanyoofu wana sababu za kuwafanya wawe na shangwe. Hivi karibuni Yehova atakomesha ulimwengu huu mwovu, lakini atafanya hivyo kwa mafaa ya wale wapendao uadilifu. Ni nini kitakachofuata uharibifu wa mfumo wa sasa wa mambo utakaoletwa na Mungu? Ah, ni mfumo mpya chini ya Ufalme wa Mungu wa kimbingu, ambao Yesu alifundisha wafuasi wake wasali juu yao! Yeye alisema hivi: “Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe. Ufalme wako uje. Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Twaweza kutazamia mabadiliko gani mapenzi ya Mungu yatendekapo hapa duniani?

Vita na ogofyo layo litakuwa limetoweka. Zaburi 46:9 lasema hivi: “[Yehova Mungu] avikomesha vita hata mwisho wa dunia; avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari [ya vita].” Kisha watu “wataketi kila mtu chini ya mzabibu wake, na chini ya mtini wake; wala hapana mtu atakayewatia hofu.”—Mika 4:4.

Maradhi hatari hayatasababisha hofu tena wala kuua watu. Ahadi ya kimungu ni hii: “Wala hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa.” (Isaya 33:24) Hicho ni chanzo cha shangwe kama nini!

Hofu zinazotokana na uhalifu na jeuri pia zitakuwa mambo yaliyopita. Zaburi 37:10, 11 laahidi hivi: “Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo, utapaangalia mahali pake wala hatakuwapo. Bali wenye upole watairithi nchi, watajifurahisha kwa wingi wa amani.”

Amani na usalama wa kweli utachukuaje mahali pa hofu za siku hizi? Kupitia serikali moja yenye uadilifu—Ufalme wa Mungu. Kuhusu wakati wetu, Danieli 2:44 lasema hivi: “Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.” Mfalme aliyewekwa rasmi na Yehova, Yesu Kristo, ‘ni lazima atawale akiwa mfalme mpaka Mungu awe ameweka maadui wote chini ya miguu yake.’ (1 Wakorintho 15:25, New World Translation) Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu utatimiza kusudi la awali la Mungu la kuwa na dunia paradiso inayokaliwa milele na wanadamu wenye furaha.—Luka 23:43; Ufunuo 20:6; 21:1-5.

Katika dunia hiyo Paradiso, kutakuwa na hofu moja tu ifaayo. Itakuwa ni “hofu ya Yehova.” (Mithali 1:7, NW) Kwa kweli twapaswa kuwa na hofu hiyo hata sasa, kwa sababu hiyo ni staha na kicho cha juu sana kikiwa na hofu ya kutompendeza Mungu kwa sababu twathamini upendo wake wenye fadhili na wema wake. Hofu hiyo humaanisha tuwe na tumaini hakika kwa Yehova na kumtii kwa uaminifu.—Zaburi 2:11; 115:11.

Matukio yenye kutia hofu yaonyesha siku hizi kuwa siku za mwisho. Hata hivyo, tukithibitisha upendo wetu kwa Mungu twaweza kufurahi badala ya kuwa wenye hofu. Unabii mbalimbali wa Biblia waonyesha kwamba uharibifu wa kimungu u karibu. Badala yao kutakuwa na mpya wenye uadilifu ulioahidiwa na Yehova Mungu. (2 Petro 3:13) Hakika, chini ya utawala wa Ufalme, hivi karibuni kutakuwa na ulimwengu bila hofu isiyofaa.

[Sanduku katika ukurasa wa 6]

UWEZO WA NAKALA MOJA

TOMASZ, mwanaume mmoja kijana kutoka Poland, alipatwa na matatizo ya kisheria yaliyomfanya atoroke nchi hiyo. Kwa miezi sita aliomba-omba lifti kotekote Ulaya, akilala katika hema na kufanya kazi tofauti-tofauti. Wakati uo huo, swali moja lilikuwa akilini mwake nyakati zote: Ni nini kusudi la uhai?

Swali la Tomasz lilijibiwa alipopewa nakala ya Mnara wa Mlinzi ya Kipoland. Aliisoma mara kadhaa na kutambua kwamba gazeti hilo lilikuwa na kweli ambayo amekuwa akitafuta. Tomasz aliomba-omba lifti kwa kilometa 200 hadi ofisi ya tawi ya Watch Tower katika Selters/Taunus, Ujerumani. Akifika Jumatatu moja jioni, alitoa gazeti lake la Mnara wa Mlinzi na kusema: “Ningependa mtu fulani anieleze mengi zaidi kuhusu yaliyomo katika gazeti hili. Nifanye nini?”

Jioni hiyo, Mashahidi wa Yehova wawili walizungumza na Tomasz kuhusu kusudi la uhai, wakitumia Biblia ikiwa msingi wa mazungumzo yao. Akitamani kujifunza mengi, Tomasz alirudi kwenye ofisi ya tawi kila siku katika juma hilo, akijifunza Biblia na kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.

Tomasz aliamua kurudi Poland, ingawa angekabili matatizo huko. Kwa hiyo, siku ya Ijumaa, siku nne tu baada ya kufika kwenye ofisi ya tawi ya Selters, Tomasz alifunga safari ya kwenda nyumbani. Mara moja alianza kujifunza pamoja na Mashahidi wa Yehova nchini Poland. Tomasz alifanya maendeleo ya haraka naye akaanza kuongea kwa bidii na wengine juu ya yale alikuwa akijifunza. Mnamo Oktoba 1993, miezi minne tu baada ya safari yake ya kwanza ya kwenda Selters, alibatizwa akiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova.

Nakala moja tu ya Mnara wa Mlinzi ilimsaidia mwanaume huyo kijana achunguze kusudi la uhai!

[Picha katika ukurasa wa 7]

Chini ya Ufalme unaotawalwa na Yesu Kristo, ulimwengu hautashikwa na hofu tena kamwe

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki