Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 4/1 kur. 3-4
  • Dini—Je, Ni Mwiko Kuizungumza?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dini—Je, Ni Mwiko Kuizungumza?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Je! Dini Yoyote Ni Nzuri vya Kutosha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kuzoea Dini Safi Kwa Ajili Ya Kuokolewa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Dini ya Kweli—Namna ya Kuitambua
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 4/1 kur. 3-4

Dini—Je, Ni Mwiko Kuizungumza?

“KUNA habari za aina mbili nisizozungumza kamwe: dini na siasa!” Huo ni mwitikio wa mara kwa mara Mashahidi wa Yehova wanapozungumza na wengine kuhusu Biblia. Na maoni hayo yanaeleweka.

Watu wanapojadili siasa, hasira kali huenda zikawaka na mabishano kufuata. Wengi hawadanganyiki kwa ahadi zisizo na maana nao hutambua kwamba mara nyingi wanasiasa hutafuta mamlaka, umashuhuri, na pesa tu. Kwa kusikitisha, nyakati nyingine tofauti za kisiasa hutokeza jeuri.

‘Lakini,’ huenda ukafikiri, ‘je, sivyo ilivyo na dini pia? Je, uchochezi wa kidini haukutokeza magombano ya siku hizi?’ Katika Ireland ya Kaskazini, Wakatoliki wa Kiroma na Waprotestanti kwa muda mrefu wamepambana. Katika Balkani, washiriki wa Kanisa Orthodoksi la Mashariki, Wakatoliki wa Kiroma, na wengineo waligombania eneo. Tokeo likawa nini? Ukatili na uadui usiokoma.

Wakikabiliwa na tisho la kifo, wengi hujaribu kuficha itikadi zao na zile za familia zao. Katika Afrika, uhasama wa kidini wa karne nyingi kati ya watu wa Jumuiya ya Wakristo na wafuasi wa dini za kigeni na pia za kikabila ulifanya wazazi wawape watoto wao majina mawili yaliyowapa kiasi fulani cha ulinzi, desturi ambayo inaendelea hata leo. Hivyo, kijana aweza kusema ni mshiriki wa kanisa au adai kuwa ni wa dini nyingine kwa kutumia jina moja bali si lile jingine. Itikadi za kidini za mtu fulani ziwezapo kumgharimu uhai wake, basi si ajabu kwamba atasitasita kuzungumza dini peupe.

Kwa wengine, dini ni mwiko kuzungumzwa hata uhai wao usipotishwa. Wao huogopa kwamba kuzungumza juu ya itikadi zao na mtu fulani wa dini tofauti kutaongoza kwenye mabishano yasiyo na maana. Na bado wengine huamini kwamba dini zote ni nzuri. Wao husema kwamba, ikiwa yale mtu anayoamini yanamridhisha ni bure kuzungumza juu ya tofauti zilizopo.

Hata wanafunzi wenye bidii wa mambo ya dini hawapatani. Katika makala yake “Masomo na Mgawanyo wa Dini,” The New Encyclopædia Britannica chasema hivi: “Ni nadra sana . . . kumekuwa na upatano miongoni mwa wasomi kuhusu asili ya [dini] . . . Hivyo, habari hiyo imekuwa yenye mabishano katika historia yote.”

Kamusi moja hufafanua dini kuwa “wonyesho wa itikadi ya mtu na kicho kwa aliye na nguvu zipitazo za wanadamu anayetambuliwa kuwa muumba na mkuu wa ulimwengu wote mzima.” Jambo hili lingepasa kufanya dini itimize fungu kubwa maishani. Kwa kweli, dini imekuwa jambo la ulimwengu wote mzima la kufanyiza historia ya binadamu. “Hakujawahi kuwa na jumuiya,” chasema Oxford Illustrated Encyclopedia of Peoples and Cultures, “ambayo haikutafuta kuleta utaratibu na maana kupitia aina fulani ya dini.” Ikihusisha mambo ya msingi kama vile “utaratibu” na “maana” katika maisha, kwa kweli dini haistahili kubishaniwa au kufanyiwa mjadala. Badala ya hilo, inastahili mazungumzo—yaani, yafikiriwe kwa uzito—pamoja na mtu mwingine. Lakini pamoja na nani, na ni faida gani yaweza kupatikana kutokana na mazungumzo hayo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki