Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 4/1 uku. 9
  • Kuhubiri Katika Nyakati Zilizo Hatari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuhubiri Katika Nyakati Zilizo Hatari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Hospitali— Wakati Wewe Ni Mgonjwa
    Amkeni!—1991
  • Usisahau Kamwe Wewe Ni Shahidi!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 4/1 uku. 9

Wapiga-Mbiu wa Ufalme Waripoti

Kuhubiri Katika Nyakati Zilizo Hatari

MTUME Paulo alitabiri kwamba “siku za mwisho nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo zi[nge]kuwa hapa.” (2 Timotheo 3:1, NW) Jinsi maneno hayo yamethibitika kuwa sahihi! Watu wa El Salvador katika Amerika ya Kati wamepatwa na uhakika huu mchungu. Kwa zaidi ya mwongo mmoja, nchi hiyo ilikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoleta taabu na kifo kwa maelfu mengi. Vita vimekwisha sasa, lakini taabu imebaki. Uhalifu umeongezeka sana baada ya vita. Mtangazaji mmoja wa televisheni alisema hivi majuzi: “Ujeuri na wizi wa mabavu sasa ni tukio la kila siku.”

Mashahidi wa Yehova pia wameathiriwa na wimbi hili la uhalifu. Wezi wamevunja Majumba ya Ufalme mengi nao wameiba vikuza sauti. Katika visa kadhaa vikundi vya vijana wenye silaha wameingilia Majumba ya Ufalme mikutano ya Kikristo inapoendelea, wakiiba pesa, saa, na vitu vinginevyo vyenye thamani kutoka kwa wahudhuriaji. Wakiwa katika shughuli zao za kila siku, Mashahidi kadhaa hata wameuawa na majambazi.

Wajapopata vipingamizi hivi, Mashahidi wa Yehova katika El Salvador wanaendelea kuhubiri kwa bidii habari njema. Wanafanya hivi kwa kutii agizo hili la Kimaandiko: “Na sharti Injili ihubiriwe kwanza katika mataifa yote.” (Marko 13:10) Bado kuna wengi katika nchi hii wanaotazamia sana tumaini la Ufalme ambalo Biblia inatoa, nao Mashahidi wanajitahidi kufikia kila mmoja wao. Kuhubiri vivihivi kunathibitika kuwa njia yenye matokeo ya kuhubiri.

Shahidi mmoja, alipokuwa akitibiwa katika hospitali fulani alitumia kila fursa kuzungumza na wagonjwa wengineo juu ya ahadi za Mungu za wakati ujao, kama zipatikanavyo katika Biblia. Mtu mmoja aliyekuwa mgonjwa sana aliomboleza hivi: “Hivi karibuni nitakufa!” Lakini mtazamo wenye huzuni wa mgonjwa huyo haukumvunja moyo Shahidi huyo kumweleza habari njema za Ufalme wa Mungu. Badala ya hivyo, yeye alimsomea mtu huyo kwa sauti kubwa kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, kilichotangazwa na Mashahidi wa Yehova. Siku chache baadaye, Shahidi huyo akaondoka hospitali hiyo, akifikiri kwa sikitiko kwamba mtu huyo alikuwa akifa.

Miaka minne baadaye ilimbidi Shahidi huyo atibiwe katika hospitali nyingine. Akiwa huko, mgonjwa fulani alimwendea na kusema: “Je, unanikumbuka?” Alikuwa yule mtu aliyekuwa amekutana naye miaka minne iliyopita, mtu aliyedhaniwa atakufa! Lilishangaza na kufurahisha kama nini mtu huyo alipomkumbatia na kuongeza hivi: “Sasa mimi pia ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova!” Mtu huyo alikuwa amekubali tumaini la Biblia la wakati ujao, akajifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, na kuweka maisha yake wakfu kwa Yehova. Hakuwa Shahidi tu bali alikuwa akishiriki katika huduma ya wakati wote akiwa painia wa kawaida kwa karibu miaka miwili.

Katika kisa hiki, mbegu za kweli zilizokuwa zimepandwa katika njia ya vivihivi zilifikia moyo wenye kuitikia. Pendeleo hili la kusaidia watu wapate ujuzi wa ile kweli huwasukuma Wakristo wa kweli waendelee na kazi ya kuhubiri zijapokuwa nyakati hizi “za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki