Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 3/1 kur. 30-31
  • Yesu Awatuma Wanafunzi 70

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Awatuma Wanafunzi 70
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wahudumu Wasiokengeushwa Fikira
  • Masomo Kwetu
  • “Nendeni Mkafanye Wanafunzi”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
  • “Nifuateni, Nami Nitawafanya Kuwa Wavuvi Watu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Wanahitajiwa kwa Haraka—Wafanya Kazi Zaidi wa Mavuno!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 3/1 kur. 30-31

Walifanya Mapenzi ya Yehova

Yesu Awatuma Wanafunzi 70

ILIKUWA ni vuli ya mwaka wa 32 W.K. Ni miezi sita tu iliyobakia kabla ya kifo cha Yesu. Kwa sababu hiyo, ili kuharakisha kazi ya kuhubiri na kuwaongezea mazoezi zaidi baadhi ya wafuasi wake, aliwachagua wanafunzi 70 na “kuwatuma wawili-wawili kumtangulia kuingia katika kila jiji na mahali ambako yeye mwenyewe alikuwa akitaka kwenda.”—Luka 10:1.a

Yesu aliwatuma wanafunzi wake “kumtangulia” ili watu waweze kuamua upesi zaidi ikiwa walimwunga mkono Mesiya au walimpinga wakati ambapo Yesu mwenyewe aliwasili baadaye. Lakini kwa nini aliwatuma “wawili-wawili”? Kwa wazi, ni ili kwamba wapate kutiana moyo walipokabili upinzani.

Akikazia kwamba kazi yao ya kuhubiri ni ya hima, Yesu aliwaambia wafuasi wake hivi: “Kwa kweli, mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana-mkubwa wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Luka 10:2) Huko kufananisha kazi hiyo na mavuno kulifaa, kwa maana kukawia kokote wakati wa mavuno kungeweza kutokeza kupotezwa kwa mazao yenye thamani. Hivyohivyo, ikiwa wanafunzi wangepuuza mgawo wao wa kuhubiri, uhai wenye thamani ungepotea!—Ezekieli 33:6.

Wahudumu Wasiokengeushwa Fikira

Yesu aliwaagiza zaidi wanafunzi wake hivi: “Msichukue kibeti, wala mfuko wa chakula, wala makubazi, na msikumbatie yeyote katika kusalimu barabarani.” (Luka 10:4) Lilikuwa jambo la kidesturi kwa msafiri kubeba sio tu kibeti na chakula bali pia jozi zaidi ya makubazi, kwa maana soli zingeweza kuchakaa na gidamu zingeweza kukatika. Lakini wanafunzi wa Yesu hawakupaswa kuwa na wasiwasi juu ya mambo hayo. Badala yake, walipaswa kuwa na itibari kwamba Yehova angewatunza kupitia Waisraeli wenzao, ambao miongoni mwao ukaribishaji-wageni ulikuwa desturi.

Lakini kwa nini Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasimkumbatie yeyote katika salamu? Je, wangekuwa wenye ubaridi, hata wenye ufidhuli? La hasha! Neno la Kigiriki a·spaʹzo·mai, linalomaanisha kukumbatia katika salamu, huenda likamaanisha zaidi ya neno la heshima “jambo” au “uwe na siku njema.” Huenda pia likatia ndani busu za kidesturi, kukumbatiana, na mazungumzo marefu ambayo yangefuata wakati ambapo wajuani wawili walikutana. Mwelezaji mmoja asema hivi: “Salamu miongoni mwa watu wa Mashariki hazikutia ndani, kama vile miongoni mwetu, kuinama kidogo, au kunyoosha mkono, lakini zilifanywa kwa kukumbatiana kwingi, na kuinama kwingi, na hata kujiangusha-angusha chini. Yote hayo yalihitaji wakati mwingi.” (Linganisha 2 Wafalme 4:29.) Hivyo Yesu aliwasaidia wafuasi wake waepuke vikengeusha-fikira visivyo vya lazima, ingawa vilikuwa vya kidesturi.

Mwishowe, Yesu aliwaambia wanafunzi wake kwamba walipoingia katika nyumba, wakakaribishwa, walipaswa ‘kukaa katika nyumba hiyo, wakila na kunywa vitu ambavyo wao wangeandaa.’ Lakini ikiwa waliingia katika jiji fulani na kutopokewa vizuri, walipaswa ‘kutoka na kwenda waingie katika njia zalo pana na kusema, “Hata vumbi lililoshikamana na miguu yetu kutoka katika jiji lenu twalifuta dhidi yenu.”’ (Luka 10:7, 10, 11) Kufuta au kukung’uta vumbi kutoka miguuni mwa mtu kungeonyesha kwamba, kwa amani, wanafunzi walikuwa wakiiachia nyumba au jiji lisilowapokea yale ambayo yangefuata hatimaye kutoka kwa Mungu. Lakini wale waliowapokea wanafunzi wa Yesu kwa fadhili walijiweka katika hali ya kuja kupokea baraka. Pindi nyingine Yesu aliwaambia mitume wake hivi: “Yeye awapokeaye nyinyi hunipokea mimi pia, naye anipokeaye mimi humpokea yeye pia aliyenituma. Na yeyote yule ampaye mmoja wa wadogo hawa kikombe tu cha maji baridi ya kunywa kwa sababu ni mwanafunzi, nawaambia nyinyi kwa kweli, huyo hatapoteza thawabu yake kwa vyovyote.”—Mathayo 10:40,42.

Masomo Kwetu

Utume wa kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu na kufanya wanafunzi sasa unatekelezwa na Mashahidi wa Yehova zaidi ya 5,000,000 ulimwenguni pote. (Mathayo 24:14; 28:19, 20) Wao hung’amua kwamba ujumbe wao ni wa hima. Kwa hiyo, wao hutumia wakati wao kikamili, wakiepuka vikengeusha-fikira ambavyo vingewazuia kutoa uangalifu kamili kwa mgawo wao wenye maana.

Mashahidi wa Yehova hujitahidi kuchangamkia wote wanaokutana nao. Hata hivyo, hawashiriki tu katika maongezi ya kipuuzi, wala hawahusiki katika mijadala juu ya masuala ya kijamii au katika majaribio ya ulimwengu huu yasiyofua dafu ya kurekebisha ukosefu mbalimbali wa haki. (Yohana 17:16) Badala ya hivyo, wao hukazia mazungumzo yao ule utatuzi wa pekee wa kudumu wa matatizo ya mwanadamu—Ufalme wa Mungu.

Mara nyingi, Mashahidi wa Yehova huonekana wakihubiri wawili-wawili. Je, mengi zaidi hayangetimizwa ikiwa kila mmoja wao angehubiri peke yake? Labda. Hata hivyo, Wakristo leo hutambua manufaa za kuhubiri sambamba na mwamini mwenzao. Hilo hutoa kadiri fulani ya kinga watoapo ushahidi katika maeneo hatari. Kuhubiri pamoja na mwenzi pia huwawezesha wapya zaidi kunufaika na ustadi wa wahubiri wa habari njema wenye uzoefu. Kwa kweli, wote wawili waweza kuchangia badilishano la kitia-moyo.—Mithali 27:17.

Bila shaka, kazi ya kuhubiri ndiyo ya hima zaidi ambayo inafanywa katika “siku [hizi] za mwisho.” (2 Timotheo 3:1) Mashahidi wa Yehova wanafurahia kuwa na utegemezo wa udugu wa ulimwenguni pote ambao katika huo wao hufanya kazi “sambamba kwa ajili ya imani ya habari njema.”—Wafilipi 1:27.

[Maelezo ya Chini]

a Biblia fulani na hati za kale za Kigiriki husema kwamba Yesu aliwatuma wanafunzi “sabini na wawili.” Hata hivyo, kuna utegemezo mwingi wa hati juu ya tafsiri “sabini.” Tofauti hii ya kiufundi haipasi kutukengeusha fikira kutoka kwenye hoja kuu, kwamba Yesu alituma kikundi kikubwa cha wanafunzi wake kwenda kuhubiri.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki