Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/88 kur. 1-2
  • Wasaidie Wazee-Wazee na Wagonjwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wasaidie Wazee-Wazee na Wagonjwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UTUMISHI WA SHAMBANI
  • KUFIKA KWENYE MIKUTANO
  • WAHUSISHE KATIKA RATIBA YETU
  • Wakumbuke Waaminifu Wenye Umri Mkubwa Zaidi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Kutimiza Mahitaji ya Walio na Umri Mkubwa Kati Yetu—Takwa Gumu la Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • ‘Kuendelea Kuangalia’ Masilahi za Watu Wazee-Wazee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Yehova Anawatunza kwa Upendo Watumishi Wake Waliozeeka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 2/88 kur. 1-2

Wasaidie Wazee-Wazee na Wagonjwa

1 Makundi yaliyo mengi yana wahubiri ambao wanaendelea kuzeeka au wale ambao wana vizuizi vya kimwili. Huenda wakahitaji msaada wa kufika kwenye mikutano au kwenda kwenye utumishi wa shambani.

2 Wengine wametumikia kwa uaminifu kwa miaka mingi, nao wana tamaa ya kuendelea kushiriki katika utendaji wa kundi ijapokuwa vizuizi vyao. Dada mmoja aliye na umri unaokaribia 90 alisema: “Mimi ninampenda Yehova sana sana hivi kwamba lazima niwe na ushirika katika utumishi na kuhudhuria mikutano ili nimthibitishie jambo hilo.” (1 Kor. 15:58) Je! wewe hukubali kwamba watu wa namna hii wanahitaji msaada wetu?

UTUMISHI WA SHAMBANI

3 Ingawa wazee-wazee na wagonjwa wengi wanapata shangwe kwa kumtumikia Muumba wao, wengine hawahisi kwamba wao wanaweza kuchangia mengi. “Kwa sasa mimi nahisi kwamba utumishi wangu si mkubwa, lakini ni shangwe kubwa kumtumikia Muumba wangu,” akasema painia mmoja mwenye umri wa miaka 93. Baada ya kufanya kazi na dada huyu, mwangalizi wa mzunguko mmoja alisema hivi: “Yeye alikuwa kitia-moyo sana kwangu kuliko mimi nilivyokuwa kwake. Dada huyo anaongezea zaidi ile roho ya upainia.” Je! kuna jambo fulani tunaloweza kufanya ili kuwajulisha hawa kwamba tunawathamini sana?

4 Mara nyingi mwaliko wa kushiriki pamoja nasi kwenye utumishi wa shambani unathaminiwa sana. Ikiwa wengine wana tatizo la kutembea, je! sisi tungeweza kuwa pamoja nao wakiwa kwenye kiti cha magurudumu wakati tunapofanya kazi ya barabarani? (Mit. 17:17) Je! tungeweza kuwapeleka wahubiri hawa kwenye nyumba zisizo na ngazi? Je! wao wangeweza kwenda pamoja nasi kwenye ziara za kurudia au mafunzo ya Biblia? Au je! sisi tunajifunza Biblia pamoja na mtu ambaye anaweza kuwa na hiari ya kwenda kwenye nyumba ya mzee-mzee kwa ajili ya funzo?

5 Je! kuna jambo lo lote tunaloweza kufanya kuwasaidia wale ambao wamezuiliwa nyumbani mwao wawe na shirika lenye maana katika utumishi wa shambani? Namna gani kudokeza kwamba watumie simu? Labda sisi tungeweza kutoa majina na anwani za watu wanaoishi katika sehemu zisizoruhusiwa watu, wale wasio nyumbani, au watu wenye kupendezwa ambao wanaweza kuandikiwa barua. Painia mmoja mgonjwa aliandika hivi: “Mimi nimelemaa sana kwa ugonjwa wa yabisi kavu ambao umeenea mwili wangu wote nami siwezi kutembea. Lakini . . . bado mimi naweza kuongea, kuandika, kupiga simu, na kupelekea watu magazeti.” Dada huyo anawashukuru ndugu na dada zake waaminifu kwa kumsaidia awe na shirika kamili katika huduma.—Ebr. 6:10-12.

KUFIKA KWENYE MIKUTANO

6 Waefeso 4:25 inasema: Sisi “tu viungo, kila mmoja kiungo cha mwenzake.” Hivyo sisi tunataka kuwasaidia ndugu zetu wenye umri mkubwa na walio wagonjwa ili wafike kwenye mikutano. (Flp. 2:4) Jambo hilo linaweza kufanywa jinsi gani? Ikiwa wengine wanaogopa kuendesha gari wakati wa usiku, je! sisi tunaweza kuwachukua katika gari letu? Huenda wengine wakawa na uwezo wa kusafiri kwa kutumia magari ya abiria au hata kutembea mradi wana mtu wa kuambatana nao. Je! wewe ungeweza kusaidia katika njia hii?

7 Wengine wenye umri mkubwa ambao wamezuiwa nyumbani wamenufaika kutokana na mikutano kupitia kwa simu. Kwa wengine, mikutano imerekodiwa kisha wakaisikiliza wakati mwingine. Dada mmoja aliulizwa amtembelee dada asiyejiweza kila juma ili arudie pamoja naye mambo makuu ya mkutano. “Mimi hutumia dakika chache kumjulisha habari za karibuni pamoja na matangazo na mambo ambayo yanatendeka kundini. Pia mimi humpelekea karatasi ya karibuni ya mapitio ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Sisi tunafurahia sana wakati huu pamoja. Jambo hili linamwezesha yeye aende sambamba na kundi ingawa huwa hayupo.”

WAHUSISHE KATIKA RATIBA YETU

8 Je! wewe unaweza kuchukua nafasi ya kwanza kuwatolea msaada ndugu na dada wenye umri mkubwa? Tafuta njia za kusaidia. Jitoe mwenyewe kwa hiari. Je! kuna njia nyingine ambazo unaweza kusaidia, kama vile kuwanunulia mahitaji yao au kuwapeleka kwenye miadi? Ndugu na dada zetu wenye umri mkubwa watakuwa wenye uthamini sana kwa ajili ya hangaiko letu na msaada wenye upendo.

9 Kuwasaidia wazee-wazee na wagonjwa kunaweza kuthibitika kuwa kwenye kutajirisha sana. Wenye umri mkubwa wamepata kuona mengi maishani na mara nyingi wao wamejifunza kuishi na hali zenye magumu; hivyo, maoni na mawazo yao ya mambo yaliyopita yanaweza kuwa yenye thamani kubwa kwetu. (Mit. 16:31) Ona raha na manufaa ya kibinafsi ya kuwasaidia wazee-wazee na walio wagonjwa.—Matendo. 20:35; Rum. 1:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki