Kutoa Utumishi Mtakatifu Kwa Woga wa Kimungu
1 Wakati wa mwaka wa utumishi wa 1988, Sosaiti imepokea barua nyingi zenye kutoa uthamini wa kutoka moyoni kwa ajili ya programu ya kusanyiko la mzunguko “Thamani Inayozidi ya Kumtumikia Yehova.” Barua hizo zimeonyesha hisi kama ile ya mtunga zaburi aliyesema: “Hakika siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu kwingineko.” (Zab. 84:10) Tunajua kwamba ninyi nyote mna hisia zinazofanana na hizo juu ya pendeleo kubwa la kutumikia Yehova na kwamba ninyi pia mlinufaishwa na programu hiyo.
2 Kuanzia Septemba, programu mpya ya kusanyiko la mzunguko itakuwa na kichwa “Kutoa Utumishi Mtakatifu Kwa Woga wa Kimungu.” (Ebr. 12:28) Huku ulimwengu ukipuuza Yehova kipumbavu na kudharau ujumbe wa Ufalme wake, sisi tunafurahia pendeleo letu la kutoa utumishi mtakatifu kwa woga wa kimungu. Kweli kweli, woga unaofaa wa Yehova ni “chanzo cha hekima”; ni “safi,” ukitusukuma sisi tufanye mapenzi yake. (Zab. 19:9; 111:10, NW) Programu ya kusanyiko la mzunguko ya mwaka wa utumishi wa 1989 itatusaidia sisi kuthamini kikamili zaidi woga wa Yehova ni nini na jinsi tunavyoweza kuudhihirisha katika utumishi wetu kwake.
3 Programu hiyo itakapokuwa ikifunguka tutajifunza jinsi woga wa kimungu unavyopasa kutuathiri sisi katika huduma yetu, katika uhudhuriaji mikutano wetu, na katika maisha yetu ya siku baada ya siku. Uhitaji wa kufunga pengo lo lote kati ya yale tunayojua na yale tunayofanya yatazungumziwa. Lazima tujue si jambo la kufanya tu bali pia jinsi ya kutumia mambo tunayojifunza ili kwamba tujinufaishe sisi wenyewe na wengine na kumletea Mungu wetu sifa.
4 Hotuba ya watu wote ina kichwa “Kwa Nini Kuogopa Mungu wa Kweli?” Hakikisha kuwaalika wanafunzi wako wa Biblia pamoja na watu wengine wanaopendezwa. Kweli kweli, sisi sote tunataka kupanga shughuli zetu ili tuhudhurie na kunufaishwa kikamili na programu hii nzuri ya siku mbili. Mwangalizi wa mzunguko wenu atawajulisheni mahali na tarehe ambazo zimeratibiwa kundi lenu.