Onyesha Wengine Ufikirio—Sehemu ya 2
1 Kadiri iwezekanavyo kwa kufaa, sisi twataka kudumisha uhusiano mzuri na watu wanaoishi katika jumuiya yetu. Hilo lataka kwamba tuonyeshe ufikirio na staha kwa haki na hisia zao.
2 Mashahidi wa Yehova wanajulikana kwa adabu zao njema. Viwango vyetu vya kujiendesha katika ujirani, shuleni, na katika mahali pa kazi, na pia kwenye makusanyiko yetu, vimekuwa habari ya maelezo mengi yenye sifa.—Ona Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 1989, ukurasa 20.
3 Bila shaka, mwenendo mzuri, hutia ndani mambo mengi, kama vile ufuatiaji wa haki, bidii-nyendelevu, na adili njema. Hutia ndani pia kustahi wakaaji wanaoishi katika eneo linalozunguka Jumba la Ufalme letu. Mwenendo wetu wa kimungu kwa habari nyingine huenda ukapuuzwa tukishindwa kuonyesha jirani zetu ufikirio. Paulo alituhimiza tuwe na ‘mwenendo kama inavyoipasa injili.’—Flp. 1:27.
4 Biblia hutuhimiza ‘tufanye yote kwa utukufu wa Mungu,’ na hilo latia ndani kuonyesha watu wa nje ufikirio. (1 Kor. 10:31-33) ‘Tukiangalia mambo ya wengine,’ hatutajidukiza katika uwanja wao bila kufikiria. (Flp. 2:4) Tutaepuka pia kuingilia katika utendaji wa kibiashara wa wafanya-biashara wa mahali hapo.
5 Kuonyesha wengine ufikirio—tukiwa ndani na pia nje ya kutaniko—ni wonyesho wa nje wa vile tuhisivyo mioyoni mwetu. Yale tufanyayo na kusema yapasa kuonyesha kwamba ‘twapenda jirani zetu kama nafsi zetu.’—Mt. 7:12; 22:39.