Trakti Habari za Ufalme ya Wakati Ufaao Kugawanywa Ulimwenguni Pote
1 Mnamo Jumapili, Aprili 23, hotuba ya watu wote ya pekee itatolewa juu ya mada yenye kuvuta usikivu “Mwisho wa Dini Bandia U Karibu.” Kwenye umalizio wa mkutano siku hiyo, trakti Habari za Ufalme yenye kuchochea fikira ya kurasa nne itatolewa. Ujumbe wa wakati ufaao ulio ndani yayo utagawanywa ulimwenguni pote wakati wa kipindi cha majuma matatu kutoka Aprili 24 hadi Mei 14.
2 Katika sehemu zote za ulimwengu, watu wanafadhaika. Haidhuru ni wapi wanapoishi, wanakumbwa na matatizo. Trakti Habari za Ufalme itakuwa na upendezi halisi kwa wale wanaohangaika kwa moyo mweupe juu ya yale yanayotokea, kwa kuwa itawaelekeza kwenye Neno la Mungu kuwa chanzo kisichokosea cha mwongozo kwa binadamu. (Zab. 119:105) Sisi sote twatazamia kupata nakala ya trakti Habari za Ufalme inapotolewa mnamo Aprili 23. Kwa sasa, kuna mengi ya kufanya katika kutayarishia kampeni hiyo kubwa ya majuma matatu.
3 Tia Moyo Wote Washiriki kwa Bidii: Ni nani watakaoweza kushiriki katika kazi hiyo? Kwa hakika kila mtu ambaye tayari ni mhubiri atakuwa na hamu ya kufanya hivyo! Namna gani wanafunzi wa Biblia wanaohudhuria mikutano ya kutaniko kwa ukawaida? Baadhi yao wameshirikiana nasi kwa muda mrefu sana na wanafanya maendeleo thabiti. Ikiwa wamepatanisha maisha zao na kanuni za Kimaandiko, je, wao wanastahili kuhesabiwa kuwa wapiga-mbiu wa Ufalme? Mhubiri anayeongoza funzo hilo la Biblia aweza kuzungumzia jambo hilo na mwanafunzi, na ikiwa mwanafunzi anataka kushiriki katika utumishi wa shambani, wazee wawili watapitia pamoja naye habari kwenye kurasa 98 na 99 ya kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu. Hilo lapasa kufanywa upesi iwezekanavyo ili wale wanaostahili kuwa wahubiri wasiobatizwa washiriki kikamili katika kampeni hiyo. Wanafunzi wa Biblia ambao hawastahili bado kuhesabiwa kuwa wahubiri wasiobatizwa waweza bado kutiwa moyo kushiriki trakti Habari za Ufalme hii ya wakati ufaao na watu wanaowafahamu au na washiriki wa familia.—Ona Mnara wa Mlinzi, Novemba 15, 1988, ukurasa 17, fungu 8.
4 Kazi hii si ngumu; kila mtu aweza kushiriki. Wazazi waweza kutia ndani vipindi vya mazoezi na trakti Habari za Ufalme hii ikiwa sehemu ya funzo la Biblia la familia la kila juma ili washiriki wote wa familia wawe wametayarishwa vizuri kuitoa nyumba kwa nyumba. Kwa kawaida utoaji sahili ni mzuri zaidi. Baada ya utangulizi mfupi, toa trakti Habari za Ufalme kwa mwenye nyumba, na umtie moyo kuisoma. Wenye nyumba wanapoonyesha kupendezwa, weka rekodi ya hilo ili uweze kurudi kukuza kupendezwa huko. (1 Kor. 3:6, 7) Ufunguo wa mafanikio ni kuwa na utoaji sahili, uliotayarishwa vizuri.
5 Kutakuwa na “mengi ya kufanya” wakati wa Aprili na Mei. Katika toleo la mwezi ujao la Huduma ya Ufalme Yetu, habari ya ziada itaandaliwa katika nyongeza yenye kichwa “Mengi ya Kufanya Katika Kazi ya Bwana.”—1 Kor. 15:58, NW.