Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/98 uku. 8
  • Nataka Funzo la Biblia!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nataka Funzo la Biblia!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Mafunzo Zaidi ya Biblia Yanatakwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Je! Unatoa Mafunzo ya Biblia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Kuanzisha Mafunzo Katika Broshua Anataka
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Anza Mafunzo ya Biblia—Sasa Ndio Wakati Unaofaa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 11/98 uku. 8

Nataka Funzo la Biblia!

1 Wengi wetu tumeeleza tamaa ya funzo la Biblia, na ni vizuri. Kazi ya kuongoza funzo la Biblia ndiyo hutufanya tutimize mradi wetu wa kufanya wanafunzi wapya. (Mt. 28:19, 20) Na bado wengi wetu tumekosa kuona shangwe ya pekee ya kufundisha mtu kweli kwa miezi kadhaa, labda kwa miaka. Twaweza kufanya nini kuhusu hilo mwezi wa Novemba? Kwa kuwa kitabu Ujuzi kinatolewa mwezi huu, twaweza kufanya jitihada ya pekee kukitumia kuanzisha mafunzo mapya ya Biblia.

2 Tenga Mwisho-Juma Mmoja au Zaidi: Twatia moyo kila mtu atenge wakati fulani mwezi huu akazie kuanzisha funzo jipya la Biblia. Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wanapaswa kuteua mwisho-juma au miisho-juma ya kutumiwa hususa kwa ajili ya kusudi hili kisha wapange vikundi vyao vijitahidi kufanya ziara za kurudia pamoja.

3 Lete maandishi yenu ya ziara za kurudia kwenye mikutano hii ya utumishi. Kisha warudie wote walioonyesha kupendezwa, waliochukua fasihi, au waliohudhuria mikutano. Fanya kila ziara ukiwa na kusudi hususa la kuanzisha funzo la Biblia.

4 Toa Wonyesho wa Funzo la Biblia: Kwenye mikutano iliyoteuliwa ya utumishi, wonyesho uliotayarishwa vizuri wapaswa kutolewa, kuonyesha jinsi ya kuanzisha funzo kwenye ziara ya kurudia. Waweza kusema hivi: “Watu wengi wana Biblia, lakini hawatambui kwamba ina majibu ya maswali ya maana ambayo sisi sote hukabili maishani. [Mwonyeshe yaliyomo katika kitabu Ujuzi, na usome vichwa vya sura ya 3, 5, 6, 8, na 9.] Kwa kutumia msaada huu wa kujifunza kwa muda wa saa moja hivi kila juma, waweza kupata uelewevu wa msingi kuhusu Biblia kwa miezi michache tu. Ikiwa ungependa kuteua mojawapo ya habari hizi, nitafurahi kukuonyesha jinsi ambavyo programu hiyo hufanywa.” Mtu akisita kujifunza kwa sababu ya kuwa na ratiba yenye shughuli nyingi, mweleze kwamba pia tuna programu iliyofupishwa. Mtolee broshua Anataka, na ujitolee kujifunza somo moja fupi kila juma kwa dakika 15-30.

5 Sote tukifanya jitihada iliyoungana kuanzisha mafunzo na tukisali kupata baraka za Yehova katika jitihada zetu, kwa kweli tutapata mafunzo mapya! (1 Yh. 5:14, 15) Ukitaka funzo la Biblia, hii yaweza kuwa fursa yako ya kuanzisha moja.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki