Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 15
“Unafikiri inawezekana kumjua Mungu? [Ngoja jibu.] Utakubali kwamba ni vigumu kumwamini mtu tusiyemjua. Biblia hututia moyo tumtafute Mungu. [Soma Matendo 17:27.] Makala hizi zatuonyesha jinsi tunavyoweza kumjua Mungu zaidi.”
Amkeni! Mei 22
“Viongozi wa ulimwengu wamejaribu njia nyingi za kutatua matatizo yetu. Njia moja mpya wanayotumia ni ile ya kuunganisha ulimwengu. Katika gazeti hili, unaweza kusoma jinsi ambavyo huenda ikawa jitihada hiyo mpya imeathiri tayari maisha yako sasa. Pia unaweza kusoma juu ya utatuzi wa ulimwenguni pote uliotabiriwa katika Biblia.” Kisha soma Mathayo 6:9, 10.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Matukio ya karibuni yanasababisha wengi wajiulize kwa nini watu wasio na hatia wanakufa ghafula. Umewahi kufikiria ni kwa nini watu hufa? [Ngoja jibu, kisha ufungue kwenye chati iliyo katika ukurasa wa 7.] Ungependa kuona kile ambacho Biblia husema kuhusu mojawapo ya mapokeo ya kawaida?” Ikiwezekana, soma andiko moja lililopo hapo.
Amkeni! Juni 8
“Watu wengi huona kwamba dini hupingana na sayansi. Wengine hata huona kwamba haiwezekani kwa mtu aliye na mawazo ya kisayansi aamini Mungu. Wewe waonaje hilo? [Ngoja jibu.] Gazeti la Amkeni! lazungumzia habari hii katika njia yenye kuarifu sana.”