Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/07 uku. 7
  • Kampeni Kubwa Zaidi Duniani ya Kuhubiri!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kampeni Kubwa Zaidi Duniani ya Kuhubiri!
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Jehovah’s Witnesses—Organized to Share the Good News
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Vifaa Vinavyoelimisha, Vinavyochochea, na Vinavyoimarisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Mashahidi wa Yehova Tengenezo Linalotegemeza Jina
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Video Mpya! Jinsi ya Kuitumia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 12/07 uku. 7

Kampeni Kubwa Zaidi Duniani ya Kuhubiri!

Kwa zaidi ya miaka 100, Mashahidi wa Yehova wamepangwa kitengenezo ili washiriki katika kazi ya kutangaza habari njema. (1 Kor. 9:23) Katika kampeni hiyo kubwa zaidi kuwahi kufanywa duniani, tunahubiri ujumbe huo katika mamia ya lugha. Tunahubiri ujumbe huo katika nchi zaidi ya 230. (Mt. 24:14) Lakini kwa nini kazi hiyo ni muhimu sana? Na imetimizwaje ulimwenguni pote?

Video Jehovah’s Witnesses—Organized to Share the Good News inajibu maswali hayo kwa kuzungumzia kwa undani jinsi kazi hiyo ya ulimwenguni pote ilivyotimizwa. Unapoitazama, fikiria maswali yafuatayo: (1) Utendaji wetu umepangwa na kusimamiwa jinsi gani? (2) Idara za Uandikaji, Huduma za Tafsiri, Sanaa, na Utayarishaji wa Kaseti na Video zinachangiaje kuenezwa kwa habari njema? (3) Lengo la uchapishaji na usafirishaji wetu wa hali ya juu ni nini? (Yoh. 17:3) (4) Ni vichapo vingapi vinavyochapishwa kwa mwaka mmoja? (5) Vichapo vyetu vinavyotegemea Biblia vinatimiza nini? (Ebr. 4:12) (6) Ni jambo gani limefanywa ili kuwasaidia kiroho wale wenye matatizo ya kuona au kusikia? (7) Kazi yetu inategemezwaje? (8) Tunafaidikaje kutokana na kazi ya Huduma za Habari za Kihospitali, Idara ya Utumishi, na Idara ya Kusanyiko? (9) Ukiwa Shahidi wa Yehova, video hii imeongezaje uthamini wako kuelekea (a) jitihada ambazo tengenezo la Yehova linafanya ili kuhubiri habari njema? (b) familia zaidi ya 100 za Betheli ulimwenguni pote? (c) mazoezi ambayo waangalizi na wamishonari wanapewa? (d) umuhimu wa kuanza kila siku kwa kuchunguza andiko la Biblia na kujitayarisha kwa ajili ya mikutano ya kutaniko kila juma? (e) faida za kuhudhuria mikutano yetu ya Kikristo? (f) mambo yatakayoletwa na Paradiso duniani? (Isa. 11:9) (g) kushiriki kwa ukamili katika kazi inayoendelea ya mavuno?—Yoh. 4:35.

Umepata matokeo gani mazuri baada ya kuwaonyesha watu wako wa ukoo, marafiki, ziara zako za kurudia, na mafunzo ya Biblia video hiyo? Mbona usitazame video hiyo na mtu mwingine unapomhubiria habari njema?—Mt. 28:19, 20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki