‘Fanya Mambo Yote kwa Ajili ya Habari Njema’
1. Mhubiri wa Ufalme yuko tayari kufanya nini kwa ajili ya wengine, na kwa nini?
1 Mtume Paulo alihisi kwamba ana wajibu wa kuwatangazia wengine habari njema. (1 Kor. 9:16, 19, 23) Vivyo hivyo, ikiwa tunahangaikia hali njema ya milele ya watu, tutachochewa kujitahidi tuwezavyo kuwahubiria habari njema.
2. Tunapohubiri, tunapaswa kuwa tayari kufanya mabadiliko gani, na kwa nini?
2 Hubiri Wakati na Mahali Ambapo Watu Wanapatikana: Mvuvi mzuri anatupa nyavu wakati na mahali ambapo ni rahisi kuwapata samaki, bali si wakati na mahali panapomfaa. Sisi pia, tukiwa “wavuvi wa watu,” huenda tukahitaji kufanya mabadiliko fulani ili kuwapata watu katika eneo letu na hivyo kufurahia hata zaidi pendeleo la kukusanya “samaki wa kila aina.” (Mt. 4:19; 13:47) Je, tunaweza kuwatembelea watu nyumbani kwao saa za jioni au kuzungumza nao barabarani mapema asubuhi? Lengo la Paulo lilikuwa “kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema,” na alitumia kila nafasi kufanya hivyo.—Mdo. 17:17; 20:20, 24.
3, 4. Tukiwa katika huduma, tunaweza kubadilikana kulingana na hali jinsi gani, na matokeo yatakuwa nini?
3 Badili Utangulizi Wako Upatane na Mahitaji: Mara nyingi wavuvi hubadili mbinu zao ili wavue samaki wa aina fulani. Tunawezaje kuhubiri habari njema za Ufalme kwa njia inayowavutia watu katika eneo letu? Tunapaswa kuanzisha mazungumzo kwa busara kuhusu jambo fulani linalowahangaisha watu kwa ujumla, kisha tusikilize kwa makini mambo wanayosema kuhusu jambo hilo. (Yak. 1:19) Tunaweza kuuliza swali la maoni ili tuwachochee wajieleze. (Met. 20:5) Kwa njia hiyo, tunaweza kubadili mazungumzo yetu ili kugusa mioyo yao. Paulo alikuwa “mambo yote kwa watu wa namna zote.” (1 Kor. 9:22) Kubadilikana kulingana na mahitaji ya watu katika eneo letu ni muhimu ili kuwafikia mioyo.
4 Ni shangwe kubwa kama nini kuwahubiria watu “habari njema za jambo bora”! (Isa. 52:7) Na ‘tufanye mambo yote kwa ajili ya habari njema’ ili tuwafikie watu wengi iwezekanavyo.—1 Kor. 9:23.