Sanduku la Swali
◼ Unapaswa Kufanya Nini Ukiagizwa Uache Kuhubiri?
Katika pindi fulani, polisi wamewafikia wahubiri wakiwa katika huduma na kuwaeleza kwamba wanavunja sheria, kisha wakawaagiza waache kuhubiri. Ukiagizwa uondoke, unapaswa kufanya hivyo mara moja na kwa heshima. (Mt. 5:41; Flp. 4:5) Usijaribu kushughulikia hali hiyo peke yako kwa kuzungumza na polisi kuhusu haki zetu za kisheria. Kama inawezekana, andika namba ya beji ya polisi anayehusika na kituo chake cha kazi, na ufanye hivyo kwa busara. Kisha, waeleze wazee mara moja, nao wawasiliane na ofisi ya tawi kuhusu tukio hilo. Vivyo hivyo, ukiombwa uondoke kwenye majengo fulani na msimamizi, mtunzaji, au mwakilishi wa mwenye majengo hayo, unapaswa kuondoka mara moja, kisha uwaeleze wazee. Unaweza kuepuka matatizo kwa kushughulika na wenye mamlaka kwa njia ya upole na unyenyekevu.—Met. 15:1; Rom. 12:18.