Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/10 uku. 1
  • Tunatanguliza Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tunatanguliza Nini?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unatimiza Huduma Yako Kikamili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Unatanguliza Nini Maishani Mwako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • ‘Fuata Hatua Zake kwa Ukaribu’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Kazi Yetu Kuu Ni Huduma ya Kikristo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 7/10 uku. 1

Tunatanguliza Nini?

1. Yesu alionyeshaje kuwa kazi ya kuhubiri ilikuwa muhimu kwake?

1 Yesu alitanguliza kazi ya kuhubiri. Alifanya kazi hiyo kwa bidii, akatembea mamia ya kilomita kotekote Palestina ili aweze kuwahubiria watu wengi iwezekanavyo. Alirahisisha maisha yake ili aweze kukazia fikira huduma yake na kutumia wakati mwingi katika kazi hiyo. (Mt. 8:20) Umati ulipojaribu kumzuia asitoke kwao ili awaponye wagonjwa wao, alisema hivi: “Ni lazima nitangaze habari njema ya ufalme wa Mungu kwenye majiji mengine pia, kwa sababu nilitumwa kufanya hivyo.”—Luka 4:43.

2. Kwa nini kazi ya kuhubiri ilikuwa muhimu sana kwa Yesu?

2 Kwa nini kazi ya kuhubiri ilikuwa muhimu sana kwa Yesu? Hangaiko lake kuu lilikuwa kutakaswa kwa jina la Yehova. (Mt. 6:9) Upendo aliokuwa nao kumwelekea Baba yake wa mbinguni ulimsukuma kutimiza mapenzi ya Baba yake na kutii sheria Zake zote. (Yoh. 14:31) Zaidi ya hayo, aliwajali watu kikweli na alitaka kuwasaidia.—Mt. 9:36, 37.

3. Tutaonyeshaje kuwa tunakazia fikira kazi ya kuhubiri?

3 Mwige Yesu: Inaweza kuwa vigumu kutanguliza kazi ya kuhubiri kama Yesu alivyofanya, kwa kuwa ulimwengu unadai wakati mwingi kutoka kwetu na pia, kuna mambo mengi yanayoweza kukengeusha fikira zetu. (Mt. 24:37-39; Luka 21:34) Kwa hiyo, tunapaswa kuhakikisha kuwa tunatanguliza mambo yaliyo muhimu zaidi, kwa kupangia wakati wa kutayarisha na kushiriki kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri. (Flp. 1:10) Pia, tunajitahidi kudumisha maisha rahisi na tunaepuka kuutumia ulimwengu kwa ukamili.—1 Kor. 7:31.

4. Kwa nini ni muhimu sana kutanguliza mambo yanayofaa sasa?

4 Anapokuwa na wakati mchache, mtu aliye na hekima hutanguliza jambo lililo muhimu. Kwa mfano, akijua kuwa dhoruba mbaya inakuja, yeye atatumia wakati wake na nguvu zake kuhakikisha kuwa familia yake itakuwa salama na kuwaonya majirani wake. Hivyo, ataweka kando mambo yasiyo muhimu. Wakati uliobaki kabla dhoruba ya Har–Magedoni haijafika umepungua. (Sef. 1:14-16; 1 Kor. 7:29) Ili tuweze kujiokoa na kuwaokoa wale wanaotusikiliza, ni lazima tujiangalie sisi wenyewe na kufundisha kwetu tunapokuwa kutanikoni au katika utumishi wa shambani. (1 Tim. 4:16) Ndiyo, kuokoka kwetu kunategemea kutanguliza kazi yetu ya kuhubiri!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki