Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/10 uku. 2
  • Mfululizo Mpya wa Kutusaidia Kuanzisha Mafunzo ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mfululizo Mpya wa Kutusaidia Kuanzisha Mafunzo ya Biblia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unalitumia Kikamili?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Mfululizo Mpya Utakaokuwa Katika Mnara wa Mlinzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Mfululizo Utakaotusaidia Katika Huduma Yetu
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Jifunze Biblia na Watu Wanaochukua Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 12/10 uku. 2

Mfululizo Mpya wa Kutusaidia Kuanzisha Mafunzo ya Biblia

1. Ni mfululizo gani mpya utakaokuwa katika gazeti la watu wote la Mnara wa Mlinzi, nao umeandaliwa kwa kusudi gani?

1 Kuanzia mwezi ujao, kutakuwa na mfululizo mpya katika gazeti la watu wote la Mnara wa Mlinzi utakaotusaidia kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mfululizo huo una kichwa “Jifunze Kutoka Katika Neno la Mungu.” Ingawa watu fulani katika eneo watafurahia kusoma kila makala katika mfululizo huo, makala hizo hasa zimekusudiwa zizungumziwe pamoja na mwenye nyumba.

2. Ni mambo gani yaliyomo katika makala hizo?

2 Yaliyomo: Kichwa kikuu na vichwa vidogo vimeandikwa kwa njia ya maswali ya kumuuliza mwenye nyumba wakati wa mazungumzo. Maandiko makuu yameonyeshwa, hayajanukuliwa, ili mwenye nyumba afurahie kujifunza moja kwa moja kutoka katika Neno la Mungu. Mafungu ni mafupi na yanaweza kuzungumziwa mlangoni. Kila makala inarejelea kitabu Biblia Inafundisha ili kukusaidia kuendeleza funzo katika kitabu hicho ikiwezekana.

3. Tunapohubiri nyumba kwa nyumba, tunaweza kutumiaje mfululizo huo kuanzisha funzo la Biblia mlangoni?

3 Jinsi ya Kuutumia: Unapotoa magazeti, unaweza kuuliza swali linaloamsha upendezi kuhusiana na jambo linalozungumziwa katika makala kwa ujumla. Kwa mfano, toleo la Januari 1 linazungumzia thamani ya Biblia. Unaweza kuuliza: “Wewe huiona Biblia kuwa Neno la Mungu au kuwa kitabu kizuri tu? [Mruhusu ajibu.] Nina kitu chenye kupendeza kuhusu habari hiyo.” Mwonyeshe swali la kwanza, soma fungu la kwanza, kisha usome andiko lililoonyeshwa. Soma swali tena, na umwombe mwenye nyumba maoni yake. Zungumzia habari nyingi kadiri muda unavyoruhusu ukitumia maswali yaliyoorodheshwa na hoja zilizotolewa. Kabla ya kuondoka, mwonyeshe mwenye nyumba swali linalofuata na ufanye mipango hususa ya kurudi kulizungumzia. Rudi mzungumzie mambo mengine katika makala hiyo kila juma hadi wakati itakapowezekana kumletea toleo linalofuata la gazeti. Mbinu nyingine ni kutumia njia ya moja kwa moja kuanzisha funzo la Biblia. Kisha utumie makala hiyo ya gazeti kumwonyesha jinsi ambavyo funzo huongozwa.

4. Tunaweza kutumiaje makala hizo tunapofanya ziara za kurudia?

4 Unaweza pia kutumia vizuri mfululizo huo mpya unapowatembelea watu unaowapelekea magazeti kwa ukawaida na watu wengine unaowarudia. Unaweza kusema: “Kuna makala mpya katika gazeti la Mnara wa Mlinzi. Ningependa kukuonyesha jinsi inavyotumiwa.” Tunasali kwamba mfululizo huo mpya utawawezesha wengi “kupata ujuzi sahihi wa kweli.”—1 Tim. 2:4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki