Mfululizo Mpya Utakaokuwa Katika Mnara wa Mlinzi
Katika Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi, tumekuwa tukitumia makala za mfululizo za Mnara wa Mlinzi “Jifunze Kutoka Katika Neno la Mungu” kuanzisha mafunzo ya Biblia. Kuanzia Januari tutakuwa tukitumia mfululizo wenye kichwa “Majibu ya Maswali ya Biblia,” utakaokuwa ukipatikana kwenye ukurasa wa nyuma wa toleo la watu wote. Tunaweza kutumia mfululizo wa “Majibu ya Maswali ya Biblia” katika huduma sawa na vile tulivyokuwa tukitumia mfululizo wa “Jifunze Kutoka Katika Neno la Mungu.” (km 12/10 uku. 2) Kama ilivyokuwa awali, Huduma Yetu ya Ufalme itakuwa na mapendekezo tunayoweza kutumia katika Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi.