Jitahidi Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza
Kuanzia mwezi wa Mei mwaka wa 2011, wahubiri walitiwa moyo waanzishe mafunzo ya Biblia katika Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi. Ili kutusaidia kufanya hivyo, gazeti la watu wote la Mnara wa Mlinzi lina makala hususa yenye kichwa “Majibu ya Maswali ya Biblia.” Kwa hiyo, mkutano wa utumishi wa shambani ambao hufanywa katika Jumamosi ya kwanza ya mwezi unapaswa kuonyesha jinsi makala hiyo inavyoweza kutumiwa kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mkutano huo unapaswa kutia ndani onyesho la jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia.
Wazee wanaweza kuamua kila kikundi cha utumishi kikutane peke yake katika Jumamosi ya kwanza, au wanaweza kuamua vikundi vyote vikutane pamoja kwenye Jumba la Ufalme. Hata hivyo, ikiwa makutaniko kadhaa yanatumia Jumba moja la Ufalme, hakuna kutaniko linalopaswa kubadilisha siku ya kuanzisha mafunzo ya Biblia ili tu vikundi vya utumishi vikutane pamoja.