Je, Unaweza Kuwaalika?
Makutaniko mengi yana wahubiri wasioweza kutimiza mengi katika utumishi kwa sababu wamedhoofika kiafya au wamezeeka. (2 Kor. 4:16) Je, unaweza kumwalika mhubiri aliye katika hali hiyo ajiunge nawe unapojifunza na mwanafunzi wako wa Biblia? Ikiwa hawezi kutoka nje, unaweza kuongoza funzo katika nyumba ya mhubiri huyo. Je, nyakati fulani unaweza kufanya mipango ya kuhubiri na mhubiri huyo nyumba kwa nyumba angalau kwa muda mfupi au kwenda naye kwenye ziara moja au mbili za kurudia? Wahubiri wengi wenye umri mkubwa wana uzoefu mwingi katika utumishi. Kwa hiyo, si wao tu watakaotiwa moyo na jitihada zako. Wewe pia utafaidika. (Rom. 1:12) Kwa kuongezea, Yehova atakuthawabisha unapojitahidi kuonyesha upendo kwa njia hiyo.—Met. 19:17; 1 Yoh. 3:17, 18.