MAISHA YA MKRISTO
Je, Unafaidika Kutokana na Kuyachunguza Maandiko Kila Siku?
Je, mazoea yako ya kiroho yanatia ndani kusoma andiko la Biblia na maelezo yaliyo kwenye kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku? Kama sivyo, je, unaweza kuanza mazoea hayo? Wengi husoma andiko asubuhi mapema ili watafakari mawazo hayo wanapoendelea na shughuli zao za kila siku. (Yos 1:8; Zb 119:97) Unawezaje kunufaika zaidi unaposoma andiko? Soma mistari inayotangulia na kufuata andiko hilo ili uelewe muktadha. Fikiria kuhusu simulizi la Biblia linaloonyesha kanuni inayozungumziwa katika andiko hilo. Kisha, ufikirie jinsi ya kutumia kanuni hiyo katika maisha yako. Ukifanya maamuzi kwa kutegemea Biblia, maisha yako yataongozwa na Neno la Mungu nawe utanufaika.—Zb 119:105.
Ulimwenguni pote, familia za Betheli hutumia kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku wakati wa kiamsha-kinywa. Katika miaka ya hivi karibuni, video nyingi za ibada hiyo ya asubuhi zimewekwa katika JW Broadcasting® kwenye sehemu ya PROGRAMU NA MATUKIO. Ni lini mara ya mwisho ulipotazama video hizo? Labda habari zinazozungumziwa ndizo unazohitaji hasa. Kwa mfano, simulizi kumhusu Loti linawezaje kukusaidia unapofanya maamuzi?
TAZAMA VIDEO YENYE KICHWA MSIUPENDE ULIMWENGU (1YO 2:15), KISHA UJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Ni kanuni gani iliyokuwa msingi wa mazungumzo ya Ibada hii ya Asubuhi?
Simulizi kumhusu Loti linaonyeshaje hatari za kuupenda ulimwengu na vitu vilivyo katika ulimwengu?—Mwa 13:12; 14:12; 19:3, 12, 13, 24-26
Tunaonyeshaje kwamba tunampenda Yehova si ulimwengu na vitu vilivyo katika ulimwengu?
Ninaweza kuonyeshaje kwamba ninalithamini Neno la Yehova siku nzima?