HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 17-18
Wanaume Wenye Kiasi Huwazoeza na Kuwakabidhi Wengine Majukumu
Ndugu wenye uzoefu huonyesha kiasi, upendo, na wanaonyesha wanafikiria mahitaji ya wakati ujao wanapowazoeza na kuwakabidhi majukumu akina ndugu wenye umri mdogo. Jinsi gani?
Teua wale wenye uwezo wa kushughulikia majukumu zaidi katika utumishi wa Yehova
Eleza waziwazi kile kinachohitajika ili kutimiza kazi fulani
Andaa pesa, vifaa, na msaada unaohitajika ili kutimiza kazi
Fuatilia maendeleo ya yule unayemzoeza, na umhakikishie kwamba unaamini kwamba ana uwezo wa kukamilisha kazi hiyo
JIULIZE, ‘Ninaweza kuwakabidhi wengine majukumu gani?’