-
Stefano—“Amejaa Kibali cha Mungu na Nguvu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
SURA YA 6
Stefano—“Akiwa Amejaa Kibali cha Mungu na Nguvu”
Ujasiri wa Stefano akiwa mbele ya Sanhedrini
1-3. (a) Stefano anakabili hali gani ngumu, naye anatendaje? (b) Tutachunguza maswali gani?
STEFANO yuko mahakamani, mbele ya wanaume 71 katika jumba kubwa ambalo huenda liko karibu na hekalu la Yerusalemu. Mahakama hiyo inayoitwa Sanhedrini, imekutana ili kusikiliza kesi ya Stefano. Mahakimu wenyewe ni watu mashuhuri, wenye mamlaka, na wengi wao wanamdharau mwanafunzi huyo wa Yesu. Kuhani Mkuu Kayafa, ambaye alikuwa mkuu wa mahakama hiyo Yesu Kristo ilipohukumiwa kifo miezi michache iliyopita, ndiye aliyeitisha kikao hicho. Je, Stefano anaogopa?
2 Sura ya Stefano inaonekana tofauti kabisa. Mahakimu wanapomkazia macho, wanaona kwamba uso wake ni “kama uso wa malaika.” (Mdo. 6:15) Malaika ni wajumbe wa Yehova Mungu, nao hawana sababu yoyote ya kuogopa bali huwa watulivu na wenye amani. Ndivyo alivyo Stefano—hata mahakimu hao wenye chuki kali wanaona hilo wazi. Ni nini kinachomwezesha kuwa mtulivu hivyo?
3 Leo, Wakristo wanaweza kujifunza mengi kutokana na jibu la swali hilo. Pia, tunahitaji kujua jinsi Stefano alivyojikuta katika hali hiyo mbaya. Alikuwa ameiteteaje imani yake awali? Nasi tunaweza kumwiga jinsi gani?
“Wakawachochea Watu” (Mdo. 6:8-15)
4, 5. (a) Kwa nini Stefano alithaminiwa sana kutanikoni? (b) Stefano alikuwa “amejaa kibali cha Mungu na nguvu” jinsi gani?
4 Tayari tumejifunza kwamba Stefano alithaminiwa sana katika kutaniko changa la Kikristo. Katika sura ya tano ya kitabu hiki, tuliona kwamba alikuwa miongoni mwa wanaume saba wanyenyekevu waliojitolea kuwasaidia mitume walipoombwa wafanye hivyo. Unyenyekevu wake unaonekana wazi unapozingatia vipawa alivyokuwa navyo. Andiko la Matendo 6:8 linasema kwamba alikuwa akifanya “mambo makubwa ya ajabu na ishara,” kama baadhi ya mitume. Pia, tunaambiwa kwamba alikuwa “amejaa kibali cha Mungu na nguvu.” Maneno hayo yanamaanisha nini?
5 Neno la Kigiriki “kibali cha Mungu” linaweza kutafsiriwa pia “neema.” Inaonekana watu wengi walivutiwa sana na Stefano kwa sababu alishughulika nao kwa fadhili na heshima. Alizungumza kwa usadikisho sana hivi kwamba wasikilizaji wake waliona unyoofu wake wa moyoni na kweli muhimu alizokuwa akizungumzia. Alikuwa na nguvu nyingi kwa sababu alikuwa na roho ya Yehova, naye alikubali mwongozo wake. Badala ya kuwa na kiburi kwa sababu ya vipawa na uwezo wake, alielekeza sifa zote kwa Yehova na kuwahangaikia kwa upendo watu aliokuwa akizungumza nao. Si ajabu kwamba hata wapinzani wake walimwogopa!
6-8. (a) Stefano alishtakiwa nini, na kwa nini? (b) Kwa nini mfano wa Stefano ni muhimu kwa Wakristo leo?
6 Wanaume kadhaa walisimama ili kubishana na Stefano, lakini “hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na roho iliyomwongoza kusema.”a Wakiwa wamekasirika, “wakawashawishi watu kwa siri” walete mashtaka dhidi ya mfuasi huyo wa Kristo asiye na hatia. Pia, “wakawachochea watu,” wazee na waandishi, ili Stefano akamatwe kwa nguvu na kumpeleka kwenye Sanhedrini. (Mdo. 6:9-12) Washtaki hao walidai kwamba anamkufuru Mungu na Musa. Jinsi gani?
7 Washtaki hao wa uwongo walidai kwamba Stefano amemkufuru Mungu na kwamba amesema makufuru dhidi ya “mahali hapa patakatifu,” yaani, hekalu la Yerusalemu. (Mdo. 6:13) Pia, walidai amemkufuru Musa, kwa kuwa aliidharau Sheria ya Musa, kwa kubadili desturi na mapokeo yaliyoanzishwa na Musa. Hilo lilikuwa shtaka zito sana, kwa sababu Wayahudi wa wakati huo walikazia sana hekalu, Sheria ya Musa, na mapokeo mengi yaliyopitishwa kwa mdomo, waliyoyaongeza kwenye Sheria. Kwa sababu hiyo, Stefano alionwa kuwa mtu hatari, anayestahili kifo!
8 Kwa kusikitisha, watu wengi wa dini hutumia mbinu hizo kuwasumbua watumishi wa Mungu. Leo, wafuasi wa dini huwachochea wenye mamlaka wawatese Mashahidi wa Yehova. Tunaweza kufanya nini tunapokabili mashtaka ya uwongo? Tunaweza kujifunza mengi kutokana na mfano wa Stefano.
Kutoa Ushahidi kwa Ujasiri Kuhusu “Mungu wa Utukufu” (Mdo. 7:1-53)
9, 10. Wachambuzi fulani hudai nini, na ni jambo gani tunalopaswa kukumbuka?
9 Kama ilivyotajwa mwanzoni, uso wa Stefano ulikuwa mtulivu kama wa malaika, alipokuwa akisikiliza mashtaka dhidi yake. Kwa hiyo Kayafa akamgeukia na kumwuliza: “Je, mambo hayo ni ya kweli?” (Mdo. 7:1) Sasa ulikuwa wakati wa Stefano kuongea, naye hakusita kufanya hivyo!
10 Wachambuzi fulani hudai kwamba Stefano aliongea kwa muda mrefu na hakujibu mashtaka aliyoshtakiwa. Lakini, ukweli ni kwamba Stefano alituwekea mfano mzuri sana wa ‘kutetea’ habari njema. (1 Pet. 3:15) Kumbuka, alishtakiwa kwamba amemkufuru Mungu kwa kulivunjia heshima hekalu na amemkufuru Musa kwa kuidharau Sheria. Stefano alijibu kwa kuzungumzia vipindi vitatu katika historia ya taifa la Israeli, akikazia mambo fulani hususa. Acheni tuzungumzie vipindi hivyo.
11, 12. (a) Stefano aliutumiaje vizuri mfano wa Abrahamu? (b) Kwa nini Stefano alimtaja Yosefu?
11 Kipindi cha wazee wa ukoo. (Mdo. 7:1-16) Stefano alianza kwa kuzungumza kuhusu Abrahamu, aliyeheshimiwa na Wayahudi kwa sababu ya imani yake. Akianza kwa kuzungumzia jambo ambalo wote walikubaliana, Stefano alikazia kwamba Yehova, “Mungu wa utukufu,” alimtokea Abrahamu alipokuwa Mesopotamia. (Mdo. 7:2) Abrahamu alikuwa mkaaji mgeni katika Nchi ya Ahadi. Wakati huo, hakukuwa na hekalu wala Sheria ya Musa. Hivyo, mtu anawezaje kusisitiza kwamba uaminifu wa mtu kwa Mungu unategemea hekalu na Sheria ya Musa?
12 Yosefu, aliyezaliwa katika ukoo wa Abrahamu, aliheshimiwa sana pia na baraza hilo lililokuwa likimsikiliza Stefano. Hata hivyo, Stefano aliwakumbusha kwamba ndugu za Yosefu, mababa wa makabila ya Israeli, walimtesa mtu huyo mwadilifu na kumuuza utumwani. Hata hivyo, Mungu alimtumia kuokoa Israeli wakati wa njaa kali. Inaonekana kwamba Stefano aliona ulinganisho huo ulio wazi kati ya maisha ya Yosefu na ya Yesu Kristo. Lakini, ili umati huo uendelee kumsikiliza kwa makini, hakutaja jambo hilo wakati huo.
13. Mazungumzo kuhusu Musa yalijibu jinsi gani mashtaka yaliyoletwa dhidi ya Stefano, na ni jambo gani linalojitokeza wazi katika mazungumzo ya Stefano?
13 Nyakati za Musa. (Mdo. 7:17-43) Stefano alisema mengi kuhusu Musa. Alikuwa na sababu nzuri ya kufanya hivyo kwa kuwa wengi katika Sanhedrini walikuwa Masadukayo, waliokataa vitabu vingine vyote vya Biblia isipokuwa vile vilivyoandikwa na Musa. Pia, kumbuka Stefano alishtakiwa kwamba amemkufuru Musa. Maneno ya Stefano yalijibu shtaka hilo moja kwa moja, kwa kuwa yalionyesha wazi kwamba anamheshimu sana Musa na Sheria. (Mdo. 7:38) Alitaja kwamba Musa pia alikataliwa na watu aliokuwa akijaribu kuwaokoa. Walimkataa alipokuwa na umri wa miaka 40. Zaidi ya miaka 40 baadaye, walipinga uongozi wake mara kadhaa.b Jambo moja linajitokeza wazi katika mazungumzo ya Stefano: Mara kwa mara, watu wa Mungu waliwakataa watu waliowekwa rasmi na Yehova kuwaongoza.
14. Stefano alitumia masimulizi ya Musa jinsi gani ili kutegemeza hoja yake?
14 Stefano aliwakumbusha wasikilizaji wake kuwa Musa alikuwa ametabiri kwamba nabii kama Musa angetokea katika Israeli. Nabii huyo ni nani, naye angepokewa jinsi gani? Stefano aliamua kutojibu swali hilo hadi mwisho wa mazungumzo yake. Alitaja jambo lingine muhimu: Musa alijua kwamba mahali popote panaweza kuwa patakatifu, kama vile mahali palipokuwa na kichaka kinachowaka moto, ambapo Yehova alizungumza naye. Basi, je, ni lazima Yehova aabudiwe katika jengo fulani hususa, kama vile hekalu la Yerusalemu? Acheni tuone.
15, 16. (a) Kwa nini hoja ya hema la ibada ilikuwa muhimu katika mazungumzo ya Stefano? (b) Stefano alisema nini kuhusu hekalu la Sulemani?
15 Hema la ibada na hekalu. (Mdo. 7:44-50) Stefano aliikumbusha mahakama hiyo kwamba kabla hekalu lolote lile halijajengwa Yerusalemu, Mungu alimwagiza Musa ajenge hema la ibada ambalo lingeweza kuhamishwa. Kwa kuwa Musa mwenyewe aliabudu kwenye hema la ibada, hakuna yeyote kati yao angeweza kudai kwamba hema hilo la ibada halikufaa kwa sababu halikuwa hekalu.
16 Baadaye, Sulemani alijenga hekalu Yerusalemu. Roho ya Mungu ilimchochea kusema jambo muhimu katika sala yake. Kama Stefano alivyosema, “Aliye Juu Zaidi haishi katika nyumba zilizojengwa kwa mikono.” (Mdo. 7:48; 2 Nya. 6:18) Yehova anaweza kutumia hekalu kutimiza makusudi yake, lakini si kwamba hana njia nyingine. Basi, mbona waabudu wake wahisi kwamba ibada ya kweli inategemea jengo fulani lililojengwa kwa mikono ya wanadamu? Stefano alimalizia hoja yake kwa kishindo kwa kunukuu kitabu cha Isaya: “Mbingu ni kiti changu cha ufalme, nayo dunia ni kiti cha miguu yangu. Mtanijengea nyumba ya aina gani? Asema Yehova. Au pako wapi mahali pangu pa kupumzikia? Mkono wangu uliumba vitu hivi vyote, sivyo?”—Mdo. 7:49, 50; Isa. 66:1, 2.
17. Katika mazungumzo yake, Stefano (a) alionyesha nini kuhusu mtazamo wa wasikilizaji wake na (b) alijibuje mashtaka dhidi yake?
17 Unapochunguza mambo ambayo Stefano alisema mbele ya Sanhedrini, je, huoni kwamba alijibu kwa ustadi mambo aliyoshtakiwa? Alionyesha kwamba sikuzote kusudi la Yehova hutimizwa, na halizuiwi na mapokeo au desturi za wanadamu. Wale waliokuwa wakiabudu katika jengo hilo lenye kuvutia lililokuwa Yerusalemu na kushikilia desturi na mapokeo yaliyohusiana na Sheria ya Musa hawakuelewa kusudi la Sheria na hekalu! Ni kana kwamba Stefano alikuwa akisema: Njia bora zaidi ya kuheshimu Sheria na hekalu ni kumtii Yehova. Ni wazi kwamba maneno ya Stefano yalitetea vizuri matendo yake mwenyewe, kwa kuwa alifanya yote awezayo ili kumtii Yehova.
18. Tunawezaje kumwiga Stefano?
18 Tunaweza kujifunza nini kutokana na hotuba ya Stefano? Aliyajua Maandiko vizuri. Sisi pia tunapaswa kujifunza kwa bidii Neno la Mungu ili tuweze kulitumia “sawasawa neno la kweli.” (2 Tim. 2:15) Lazima pia tujifunze kuwa na neema na kutumia busara kama alivyofanya Stefano. Watu waliokuwa wakimsikiliza walikuwa wabishi sana! Hata hivyo, aliweza kuzungumza nao kwa muda mrefu, akizungumzia mambo ambayo hata wao waliyakubali na kuyathamini. Pia, alizungumza nao kwa heshima, akiwaita wazee wa mahakama hiyo, “akina baba.” (Mdo. 7:2) Sisi pia tunapaswa kutangaza kweli za Neno la Mungu “kwa upole na heshima kubwa.”—1 Pet. 3:15.
19. Stefano alitangaza hukumu za Yehova mbele ya Sanhedrini jinsi gani?
19 Hata hivyo, hatuepuki kutangaza kweli za Neno la Mungu ili tu tusiwakasirishe watu; wala hatupunguzi uzito wa ujumbe wa hukumu za Yehova. Stefano alituwekea mfano mzuri. Bila shaka, aliona wazi kwamba uthibitisho wote aliotoa mbele ya Sanhedrini haukuwa na maana yoyote machoni pa mahakimu hao wenye mioyo migumu. Kwa hiyo, akichochewa na roho takatifu, alimalizia mazungumzo yake kwa kuwaambia bila woga kwamba walikuwa tu kama baba zao waliomkataa Yosefu, Musa, na manabii wote. (Mdo. 7:51-53) Isitoshe, mahakimu hao wa Sanhedrini walikuwa wamemuua Masihi, ambaye Musa na manabii wengine wote walitabiri kuja kwake. Kwa kweli, walikuwa wameivunja kabisa Sheria ya Musa!
“Bwana Yesu, Pokea Roho Yangu” (Mdo. 7:54–8:3)
“Waliposikia mambo hayo wakawaka hasira moyoni na kuanza kumsagia meno yao.”—Matendo 7:54
20, 21. Sanhedrini ilitendaje iliposikia maneno ya Stefano, naye Yehova alimtia nguvu jinsi gani?
20 Mahakimu hao walikasirishwa sana na mambo ya kweli ambayo Stefano aliwaambia. Bila kukawia, wakaanza kumsagia meno yao. Haikosi mwanamume huyo mwadilifu alikumbuka jinsi Bwana wake Yesu alivyotendewa kikatili, naye alijua kwamba hataonyeshwa rehema hata kidogo.
21 Stefano alihitaji ujasiri ili kukabili hali iliyokuwa mbele yake. Bila shaka alitiwa moyo sana na maono ambayo Yehova alimwonyesha. Stefano aliuona utukufu wa Mungu, akamwona Yesu akiwa amesimama upande wa kulia wa Yehova! Stefano alipokuwa akisimulia maono hayo, mahakimu hao waliziba masikio kwa mikono yao. Kwa nini? Mapema, Yesu alikuwa ameiambia mahakama hiyo kwamba yeye ndiye Masihi na kwamba angeketi upande wa kulia wa Baba yake. (Marko 14:62) Maono ya Stefano yalithibitisha kwamba Yesu alisema kweli. Hakuna shaka kwamba mahakama hiyo ilikuwa imemsaliti na kumuua Masihi! Kwa pamoja wakamrukia wamtoe nje ili apigwe kwa mawe na kufa.c
22, 23. Kifo cha Stefano kilifanana jinsi gani na kifo cha Bwana wake, na kwa nini Wakristo leo wanaweza kuwa na usadikisho kama wa Stefano?
22 Stefano alikufa kama vile Bwana wake alivyokufa, akiwa na amani moyoni, akimtumaini kabisa Yehova na hakuwa na kinyongo chochote kuelekea waliomuua. Alisema, “Bwana Yesu, pokea roho yangu,” labda kwa sababu bado angeweza kumwona Mwana wa binadamu pamoja na Yehova katika maono. Huenda Stefano alijua maneno haya yenye kutia moyo yaliyosemwa na Yesu: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.” (Yoh. 11:25) Mwishowe, Stefano alisali moja kwa moja kwa Mungu kwa sauti kubwa: “Yehova, usiwahesabie dhambi hii.” Baada ya kusema hayo, akalala usingizi katika kifo.—Mdo. 7:59, 60.
23 Hivyo, Stefano akawa mfia-imani wa kwanza kati ya wafuasi wa Kristo. (Ona sanduku lenye kichwa “Stefano—Alikuwa Shahidi au Mfia-Imani?”) Hata hivyo, jambo la kusikitisha ni kwamba hakuwa wa mwisho. Leo, watumishi waaminifu wa Yehova wameuawa na wafuasi wa dini, wanasiasa, na wapinzani wengine wakatili. Hata hivyo, tuna sababu nzuri ya kuwa na usadikisho kama aliokuwa nao Stefano. Sasa, Yesu anatawala akiwa Mfalme, na ana nguvu nyingi alizopewa na Baba yake. Hakuna kitakachomzuia kuwafufua wafuasi wake waaminifu.—Yoh. 5:28, 29.
24. Sauli alichangiaje kuuawa kwa Stefano, na kifo cha Stefano kilikuwa na matokeo gani mazuri baadaye?
24 Kijana Sauli alikuwa akitazama mambo yote yaliyokuwa yakiendelea. Aliunga mkono kuuawa kwa Stefano, hata alitunza mavazi ya nje ya wale waliokuwa wakimpiga kwa mawe. Muda mfupi baadaye aliongoza katika kuwanyanyasa vikali Wakristo. Lakini kifo cha Stefano kingekuwa na matokeo mazuri baadaye. Mfano wake uliwaimarisha Wakristo wengine waendelee kuwa waaminifu mpaka mwisho kama alivyofanya. Isitoshe, Sauli, ambaye baadaye alikuja kujulikana kama Paulo, alisikitishwa sana baadaye kwa sababu ya msimamo wake Stefano alipokuwa akiuawa. (Mdo. 22:20) Alichangia kumwua Stefano, lakini baadaye alitambua makosa yake na kukiri hivi: “Nilikuwa mkufuru na mtesaji na mtu mwenye dharau.” (1 Tim. 1:13) Ni wazi kwamba, Paulo hakumsahau kamwe Stefano, na mambo yenye kuchochea sana aliyosema siku hiyo. Isitoshe, katika baadhi ya hotuba zake na barua alizoandika, Paulo alitia ndani mambo ambayo Stefano alitaja. (Mdo. 7:48; 17:24; Ebr. 9:24) Baadaye, Paulo aliiga imani na ujasiri wa Stefano, mtu aliyekuwa “amejaa kibali cha Mungu na nguvu.” Je, sisi pia tutafanya hivyo?
a Baadhi ya wapinzani hao walikuwa sehemu ya “Sinagogi la Watu Waliowekwa Huru.” Huenda walikuwa watu waliokuwa wamekamatwa na Waroma kisha wakaachiliwa, au huenda walikuwa watumwa waliowekwa huru kisha wakawa Wayahudi wageuzwa imani. Baadhi yao walikuwa wenyeji wa Kilikia, alikotoka Sauli wa Tarso. Masimulizi hayo hayataji iwapo Sauli alikuwa miongoni mwa Wakilikia waliokuwa wameshindwa kuthibitisha kwamba walikuwa sahihi kuhusu madai yao dhidi ya Stefano.
b Stefano anazungumzia habari ambazo hazipatikani kwingineko katika Biblia. Habari hizo zinatia ndani elimu ambayo Musa alipata alipokuwa Misri, umri aliokuwa nao alipokimbia Misri, na muda aliokaa Midiani.
c Chini ya sheria ya Roma, inaelekea kwamba Sanhedrini haikuwa na mamlaka ya kumhukumu mtu kifo. (Yoh. 18:31) Vyovyote vile, inaonekana kwamba Stefano aliuawa na umati uliokuwa na hasira, bali si hukumu ya kifo iliyokuwa ikitekelezwa.
-
-
Kutangaza “Habari Njema Kumhusu Yesu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
SURA YA 7
Kutangaza “Habari Njema Kumhusu Yesu”
Filipo aweka mfano mzuri katika kueneza Injili
1, 2. Ni kwa njia gani jitihada za kuzuia kazi ya kuhubiri habari njema katika karne ya kwanza hazikufanikiwa?
MATESO makali yameanza, na Sauli akaanza “kulishambulia” kutaniko—maneno ambayo katika lugha ya awali, yanamaanisha kulitesa kutaniko kikatili. (Mdo. 8:3) Wanafunzi wanatawanyika. Huenda kwa watu fulani ikaonekana kwamba lengo la Sauli la kuumaliza Ukristo litatimia. Hata hivyo, kwa sababu ya kutawanyika kwa Wakristo jambo fulani lisilotarajiwa linatokea. Jambo gani?
2 Wakristo hao waliotawanyika wakaanza ‘kutangaza habari njema ya lile neno’ katika nchi ambazo wamekimbilia. (Mdo. 8:4) Hebu wazia! Mateso hayakuzuia habari njema bali yalichangia kuenea kwa ujumbe huo! Kwa kuwatawanya wanafunzi, bila kukusudia, watesaji hao wamesaidia kazi ya kuhubiri Ufalme ienee katika maeneo ya mbali. Kama tutakavyoona, jambo fulani linalofanana na hilo limetokea katika siku zetu.
“Wale Waliotawanyika” (Mdo. 8:4-8)
3. (a) Filipo alikuwa nani? (b) Kwa nini Samaria haikuwa imehubiriwa sana, na Yesu alitabiri nini kuhusu eneo hilo?
3 Filipo ni mmoja wa “wale waliotawanyika.”a (Mdo. 8:4; ona sanduku “Filipo ‘Mweneza-Injili,’”) Alienda Samaria, jiji ambalo halikuwa limehubiriwa sana kwa sababu wakati fulani Yesu aliwaagiza mitume hivi: “Msiingie katika jiji lolote la Wasamaria; badala yake, nendeni kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.” (Mt. 10:5, 6) Hata hivyo, Yesu alijua kwamba baada ya muda fulani ushahidi kamili ungetolewa Samaria, kwa sababu kabla ya kurudi mbinguni, alisema: “Mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”—Mdo. 1:8.
4. Wasamaria walipokeaje habari njema alizowatangazia Filipo, na huenda ni kwa sababu gani?
4 Filipo aliona kwamba shamba la Samaria lilikuwa ‘jeupe kwa ajili ya kuvunwa.’ (Yoh. 4:35) Ujumbe wake uliwaburudisha watu waliokuwa wakiishi huko, na tunaweza kuelewa sababu. Wayahudi hawakuchangamana na Wasamaria, na wengi wao walionyesha chuki yao waziwazi. Kinyume na hilo, Wasamaria waliona kwamba ujumbe wa habari njema uliwapa tumaini watu wote bila ubaguzi, nao ulikuwa kinyume kabisa na mtazamo wa ubaguzi wa Mafarisayo. Kwa kuwahubiria Wasamaria kwa bidii na bila ubaguzi, Filipo alionyesha kwamba hakuathiriwa na maoni ya ubaguzi ya wale waliokuwa wanawadharau. Kwa hiyo, haishangazi kwamba umati wote wa Wasamaria ulikuwa ukimsikiliza Filipo “kwa pamoja.”—Mdo. 8:6.
5-7. Toa mifano inayoonyesha jinsi kutawanywa kwa Wakristo kumesaidia kueneza habari njema.
5 Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, mateso hayajawazuia watu wa Mungu kuendelea na kazi yao ya kuhubiri leo. Wakristo waliolazimika kuhama, iwe kwa sababu ya kufungwa gerezani au kuhamishiwa nchi nyingine, wametumia fursa hiyo kuhubiri ujumbe wa Ufalme katika maeneo hayo mapya. Kwa mfano, wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu, Mashahidi wa Yehova waliwahubiria wafungwa wenzao katika kambi za mateso za Nazi. Myahudi mmoja aliyekutana na Mashahidi katika kambi hizo alisema hivi: “Ujasiri wa wafungwa waliokuwa Mashahidi wa Yehova ulinihakikishia kwamba imani yao ilikuwa na msingi wa Kimaandiko—nami nikawa Shahidi.”
6 Katika visa fulani hata wale waliowatesa walihubiriwa na kukubali ujumbe. Kwa mfano, Ndugu Franz Desch alipokuwa katika kambi ya mateso ya Gusen nchini Austria, alijifunza Biblia na ofisa mmoja wa Nazi. Wazia shangwe yao, miaka mingi baadaye, wanaume hao wawili walipokutana kwenye kusanyiko la Mashahidi wa Yehova, wote wakiwa wahubiri wa habari njema!
7 Ndivyo ilivyokuwa wakati mateso yaliposababisha Wakristo katika nchi moja wakimbilie nchi nyingine. Miaka ya 1970, ushahidi mkubwa ulitolewa nchini Msumbiji wakati Mashahidi kutoka Malawi walipolazimika kukimbilia huko. Baadaye upinzani ulipotokea nchini Msumbiji, kazi ya kuhubiri iliendelea. Francisco Coana anasema: ‘Baadhi yetu tulikamatwa mara kadhaa kwa sababu ya kazi yetu ya kuhubiri. Lakini, tulipoona wengi wakiitikia ujumbe wa Ufalme, tulikuwa na hakika kwamba Mungu anatusaidia, kama alivyowasaidia Wakristo wa karne ya kwanza.’
8. Mabadiliko ya kisiasa na ya kiuchumi yamekuwa na matokeo gani katika kazi ya kuhubiri?
8 Bila shaka, si mateso tu yaliyochangia kuenea kwa Ukristo katika maeneo mengine. Mabadiliko ya kisiasa na ya kiuchumi yamewezesha ujumbe wa Ufalme uhubiriwe kwa watu wa lugha na mataifa mengi. Watu fulani kutoka katika maeneo yenye vita na hali ngumu za kiuchumi wamehamia katika nchi zenye utulivu na kujifunza Biblia wakiwa huko. Ongezeko la wakimbizi limefungua maeneo mapya ya lugha za kigeni. Je, unafanya yote uwezayo ili kuwahubiria watu “kutoka mataifa yote na makabila na jamii na lugha” walio katika eneo lenu?—Ufu. 7:9.
“Nipeni Mimi Pia Mamlaka Hii” (Mdo. 8:9-25)
“Simoni alipoona kwamba watu walipokea roho takatifu mitume walipoweka mikono juu yao, akawatolea pesa.”—Matendo 8:18
9. Simoni alikuwa nani, na kwa nini alivutiwa na Filipo?
9 Filipo alifanya ishara nyingi jijini Samaria. Aliwaponya walemavu na kuwafukuza roho waovu. (Mdo. 8:6-8) Mtu mmoja alivutiwa sana na uwezo wa Filipo wa kufanya miujiza. Aliitwa Simoni, naye alikuwa mchawi ambaye aliheshimiwa sana hivi kwamba watu walikuwa wakisema: “Mtu huyu ndiye Nguvu za Mungu.” Simoni alijionea mwenyewe nguvu za kweli za Mungu kutokana na miujiza iliyofanywa na Filipo, naye akawa mwamini. (Mdo. 8:9-13) Hata hivyo, baadaye nia ya Simoni ilijaribiwa. Jinsi gani?
10. (a) Petro na Yohana walifanya nini jijini Samaria? (b) Simoni alifanya nini alipoona wapya wakipokea roho takatifu baada ya Petro na Yohana kuwawekea mikono?
10 Mitume walipoona kwamba kulikuwa na ongezeko kubwa jijini Samaria, waliwatuma Petro na Yohana huko. (Ona sanduku “Petro Atumia ‘Funguo za Ufalme.’”) Mitume hao wawili walipofika waliweka mikono yao juu ya wanafunzi wapya, na kila mmoja wao akapokea roho takatifu.b Simoni alipoona hivyo, alistaajabu. Akawaambia mitume hao: “Nipeni mimi pia mamlaka hii, ili yeyote nitakayeweka mikono juu yake apokee roho takatifu.” Simoni hata alitaka kuwapa pesa wamuuzie pendeleo hilo takatifu!—Mdo. 8:14-19.
11. Petro alimwambia Simoni nini, naye Simoni aliitikiaje?
11 Petro alimkaripia Simoni na kumwambia: “Fedha yako na iangamie pamoja nawe, kwa sababu ulidhani utanunua zawadi ya bure ya Mungu kwa kutumia pesa. Wewe huna sehemu wala fungu katika jambo hili, kwa maana moyo wako si mnyoofu machoni pa Mungu.” Kisha, Petro akamhimiza Simoni atubu na kuomba msamaha. Petro akasema: ‘Mwombe Yehova dua, ili ikiwezekana, usamehewe nia mbaya ya moyo wako.’ Inaonekana kwamba Simoni hakuwa mtu mwovu; alitaka kufanya yaliyo sawa, lakini kwa muda hakuwa na maoni yanayofaa. Kwa hiyo, akawasihi mitume: “Mwombeni Yehova dua kwa ajili yangu ili nisipatwe na lolote kati ya mambo mliyosema.”—Mdo. 8:20-24.
12. “Usimoni” ni nini, na dini zinazodai kuwa za Kikristo zimetumbukiaje katika mtego huo?
12 Karipio hilo lapaswa pia kuwa onyo kwa Wakristo leo. Neno “usimoni” latokana na kisa hicho nalo linamaanisha kununua au kuuza vyeo, hasa vya kanisa. Usimoni umeenea sana katika dini zinazodai kuwa za Kikristo. Kitabu kimoja kinasema: ‘Historia ya mabaraza ya siri ya Mapapa inaonyesha wazi kwamba hakujawahi kuwa na uchaguzi wowote wa kanisa usiokuwa na usimoni, na katika visa vingi, usimoni wenyewe ulikuwa usimoni mbaya sana, wenye kuaibisha, tena ulifanywa waziwazi.’—The Encyclopædia Britannica (1878).
13. Wakristo wanapaswa kuepuka usimoni kwa njia gani?
13 Wakristo wanapaswa kujihadhari na dhambi ya usimoni. Kwa mfano, hawapaswi kujaribu kupata mapendeleo kutanikoni kwa kuwapa zawadi au kuwasifu kupita kiasi ndugu wenye madaraka. Kwa upande mwingine, ndugu hao wenye madaraka wanapaswa kuwa waangalifu wasiwaonyeshe watu wenye mali upendeleo. Yote hayo ni usimoni. Watumishi wote wa Mungu wanapaswa kujiendesha kama ‘walio wadogo,’ na kuonyesha subira huku wakiiruhusu roho takatifu ya Yehova iweke rasmi wale wanaostahili. (Luka 9:48) Katika tengenezo la Mungu, hakuna nafasi kwa ajili ya watu wanaojaribu ‘kujitafutia utukufu wao wenyewe.’—Met. 25:27.
“Je, Kweli Unajua Unayosoma?” (Mdo. 8:26-40)
14, 15. (a) “Towashi Mwethiopia” alikuwa nani, na Filipo alikutana naye jinsi gani? (b) Mwethiopia huyo aitikiaje ujumbe wa Filipo, na kwa nini uamuzi wake wa kubatizwa haukutokana tu na msisimko? (Ona maelezo ya chini.)
14 Malaika wa Yehova anamwambia Filipo aende kwenye barabara inayoshuka kutoka Yerusalemu mpaka Gaza. Muda mfupi baadaye, Filipo anaelewa sababu ya kutumwa baada ya kukutana na towashi Mwethiopia ambaye “alikuwa akimsoma kwa sauti kubwa nabii Isaya.” (Ona sanduku “‘Towashi’ Katika Maana Gani?”) Roho takatifu ya Yehova ilimwongoza Filipo alikaribie gari la mtu huyo. Huku akikimbia kandokando ya gari hilo, Filipo alimuuliza Mwethiopia huyo: “Je, kweli unajua unayosoma?” Mwethiopia akajibu: “Ninawezaje kuyaelewa mtu fulani asiponiongoza?”—Mdo. 8:26-31.
15 Mwethiopia akamsihi Filipo apande kwenye gari. Wazia mazungumzo yaliyofuata! Kwa muda mrefu, haikujulikana ni nani anayezungumziwa katika unabii unaohusu “kondoo,” au “mtumishi,” katika kitabu cha Isaya. (Isa. 53:1-12) Hata hivyo, walipokuwa wakiendelea na safari, Filipo alimfafanulia kwamba Yesu Kristo ndiye anayezungumziwa katika unabii huo. Kama wale waliobatizwa siku ya Pentekoste, mwaka wa 33 W.K., Mwethiopia huyo ambaye tayari alikuwa Myahudi mgeuzwa imani akajua mara moja jambo analopaswa kufanya. Kisha akamwambia Filipo. “Tazama! Hapa kuna maji; ni nini kinachonizuia kubatizwa?” Bila kukawia, Filipo akambatiza Mwethiopia huyo!c (Ona sanduku “Kubatizwa ‘Mahali Penye Maji.’”) Kisha, roho ya Mungu ikamwongoza Filipo kwenda katika mgawo mwingine huko Ashdodi, ambako aliendelea kutangaza habari njema.—Mdo. 8:32-40.
16, 17. Malaika wanahusika jinsi gani katika kazi ya kuhubiri leo?
16 Wakristo leo wana pendeleo la kushiriki kazi kama iliyofanywa na Filipo. Mara nyingi, wanaposafiri wanatumia nafasi hiyo kuwahubiria watu ujumbe wa Ufalme. Katika visa vingi, wanapopata mtu mnyoofu, hawashangai kwa sababu Biblia inaonyesha wazi kwamba malaika wanaelekeza kazi ya kuhubiri ili ujumbe huo ufikie “kila taifa na kabila na lugha na watu.” (Ufu. 14:6) Yesu alitabiri kwamba malaika wangeelekeza kazi ya kuhubiri. Katika mfano wa ngano na magugu, Yesu alisema kwamba wakati wa mavuno, au umalizio wa mfumo wa mambo, “wavunaji ni malaika.” Pia, alisema, viumbe hao wa kiroho “watakusanya kutoka katika Ufalme wake vitu vyote vinavyosababisha kukwazika na watu wenye mazoea ya kuasi sheria.” (Mt. 13:37-41) Wakati huohuo, malaika watakusanya watu watakaorithi Ufalme wa mbinguni, kisha watakusanya “umati mkubwa” wa “kondoo wengine,” ambao Yehova anawavuta katika tengenezo lake.—Ufu. 7:9; Yoh. 6:44, 65; 10:16.
17 Jambo moja linalothibitisha kwamba malaika wanaelekeza kazi yetu ni kwamba watu fulani tunaowapata katika huduma yetu husema kwamba wamekuwa wakisali ili wapate mwongozo wa kiroho. Fikiria jambo moja lililoonwa: Wahubiri wawili wa Ufalme walikuwa wakihubiri pamoja na mtoto mdogo. Ilipofika mchana, wahubiri hao walipotaka kuondoka kwenye eneo, yule mtoto alitaka sana waende nyumba inayofuata. Alienda kubisha mlango huo! Mwanamke alipoufungua mlango, Mashahidi hao wawili wakakaribia ili kuzungumza naye. Walishangaa kusikia kwamba mwanamke huyo alikuwa ametoka tu kusali mtu amtembelee na kumsaidia kuelewa Biblia. Funzo la Biblia likaanzishwa!
“Mungu, ikiwa upo, tafadhali nisaidie”
18. Kwa nini hatupaswi kamwe kuipuuza huduma yetu?
18 Ukiwa mmoja wa wahubiri katika kutaniko la Kikristo, una pendeleo la kushiriki bega kwa bega katika kazi ya kuhubiri ambayo leo inafanywa kwa kiwango kikubwa zaidi. Usilipuuze kamwe pendeleo hilo. Ukidumu katika kazi hiyo, utapata shangwe kubwa inayotokana na kutangaza “habari njema kumhusu Yesu.”—Mdo. 8:35.
a Filipo huyu si mtume Filipo. Badala yake, ni Filipo ambaye, kama Sura ya 5 ya kitabu hiki inavyoeleza, alikuwa mmoja wa “wanaume saba wenye sifa nzuri” ambao waliwekwa rasmi kusimamia ugawaji wa kila siku wa chakula kati ya Wakristo wajane waliozungumza Kigiriki na waliozungumza Kiebrania katika jiji la Yerusalemu.—Mdo. 6:1-6.
b Inaonekana kwamba kwa kawaida wanafunzi wapya walitiwa mafuta, au kupokea roho takatifu walipobatizwa. Baada ya kupokea roho hiyo, wakawa na tumaini la kutawala wakiwa wafalme na makuhani pamoja na Yesu mbinguni. (2 Kor. 1:21, 22; Ufu. 5:9, 10; 20:6) Hata hivyo, katika kisa hiki, Wakristo wapya hawakutiwa mafuta walipobatizwa. Walipokea roho takatifu pamoja na uwezo wa kufanya miujiza walipowekewa mikono na Petro na Yohana.
c Huo haukuwa msisimko tu. Kwa kuwa alikuwa Myahudi mgeuzwa imani, tayari alikuwa na ujuzi wa Maandiko, kutia ndani unabii kuhusu Masihi. Baada ya kuelewa jukumu la Yesu katika mpango wa Mungu, hakuna jambo lililomzuia kubatizwa.
-
-
Kutangaza “Habari Njema Kumhusu Yesu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
SURA YA 7
Kutangaza “Habari Njema Kumhusu Yesu”
Filipo aweka mfano mzuri katika kueneza Injili
1, 2. Ni kwa njia gani jitihada za kuzuia kazi ya kuhubiri habari njema katika karne ya kwanza hazikufanikiwa?
MATESO makali yameanza, na Sauli akaanza “kulishambulia” kutaniko—maneno ambayo katika lugha ya awali, yanamaanisha kulitesa kutaniko kikatili. (Mdo. 8:3) Wanafunzi wanatawanyika. Huenda kwa watu fulani ikaonekana kwamba lengo la Sauli la kuumaliza Ukristo litatimia. Hata hivyo, kwa sababu ya kutawanyika kwa Wakristo jambo fulani lisilotarajiwa linatokea. Jambo gani?
2 Wakristo hao waliotawanyika wakaanza ‘kutangaza habari njema ya lile neno’ katika nchi ambazo wamekimbilia. (Mdo. 8:4) Hebu wazia! Mateso hayakuzuia habari njema bali yalichangia kuenea kwa ujumbe huo! Kwa kuwatawanya wanafunzi, bila kukusudia, watesaji hao wamesaidia kazi ya kuhubiri Ufalme ienee katika maeneo ya mbali. Kama tutakavyoona, jambo fulani linalofanana na hilo limetokea katika siku zetu.
“Wale Waliotawanyika” (Mdo. 8:4-8)
3. (a) Filipo alikuwa nani? (b) Kwa nini Samaria haikuwa imehubiriwa sana, na Yesu alitabiri nini kuhusu eneo hilo?
3 Filipo ni mmoja wa “wale waliotawanyika.”a (Mdo. 8:4; ona sanduku “Filipo ‘Mweneza-Injili,’”) Alienda Samaria, jiji ambalo halikuwa limehubiriwa sana kwa sababu wakati fulani Yesu aliwaagiza mitume hivi: “Msiingie katika jiji lolote la Wasamaria; badala yake, nendeni kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.” (Mt. 10:5, 6) Hata hivyo, Yesu alijua kwamba baada ya muda fulani ushahidi kamili ungetolewa Samaria, kwa sababu kabla ya kurudi mbinguni, alisema: “Mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”—Mdo. 1:8.
4. Wasamaria walipokeaje habari njema alizowatangazia Filipo, na huenda ni kwa sababu gani?
4 Filipo aliona kwamba shamba la Samaria lilikuwa ‘jeupe kwa ajili ya kuvunwa.’ (Yoh. 4:35) Ujumbe wake uliwaburudisha watu waliokuwa wakiishi huko, na tunaweza kuelewa sababu. Wayahudi hawakuchangamana na Wasamaria, na wengi wao walionyesha chuki yao waziwazi. Kinyume na hilo, Wasamaria waliona kwamba ujumbe wa habari njema uliwapa tumaini watu wote bila ubaguzi, nao ulikuwa kinyume kabisa na mtazamo wa ubaguzi wa Mafarisayo. Kwa kuwahubiria Wasamaria kwa bidii na bila ubaguzi, Filipo alionyesha kwamba hakuathiriwa na maoni ya ubaguzi ya wale waliokuwa wanawadharau. Kwa hiyo, haishangazi kwamba umati wote wa Wasamaria ulikuwa ukimsikiliza Filipo “kwa pamoja.”—Mdo. 8:6.
5-7. Toa mifano inayoonyesha jinsi kutawanywa kwa Wakristo kumesaidia kueneza habari njema.
5 Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, mateso hayajawazuia watu wa Mungu kuendelea na kazi yao ya kuhubiri leo. Wakristo waliolazimika kuhama, iwe kwa sababu ya kufungwa gerezani au kuhamishiwa nchi nyingine, wametumia fursa hiyo kuhubiri ujumbe wa Ufalme katika maeneo hayo mapya. Kwa mfano, wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu, Mashahidi wa Yehova waliwahubiria wafungwa wenzao katika kambi za mateso za Nazi. Myahudi mmoja aliyekutana na Mashahidi katika kambi hizo alisema hivi: “Ujasiri wa wafungwa waliokuwa Mashahidi wa Yehova ulinihakikishia kwamba imani yao ilikuwa na msingi wa Kimaandiko—nami nikawa Shahidi.”
6 Katika visa fulani hata wale waliowatesa walihubiriwa na kukubali ujumbe. Kwa mfano, Ndugu Franz Desch alipokuwa katika kambi ya mateso ya Gusen nchini Austria, alijifunza Biblia na ofisa mmoja wa Nazi. Wazia shangwe yao, miaka mingi baadaye, wanaume hao wawili walipokutana kwenye kusanyiko la Mashahidi wa Yehova, wote wakiwa wahubiri wa habari njema!
7 Ndivyo ilivyokuwa wakati mateso yaliposababisha Wakristo katika nchi moja wakimbilie nchi nyingine. Miaka ya 1970, ushahidi mkubwa ulitolewa nchini Msumbiji wakati Mashahidi kutoka Malawi walipolazimika kukimbilia huko. Baadaye upinzani ulipotokea nchini Msumbiji, kazi ya kuhubiri iliendelea. Francisco Coana anasema: ‘Baadhi yetu tulikamatwa mara kadhaa kwa sababu ya kazi yetu ya kuhubiri. Lakini, tulipoona wengi wakiitikia ujumbe wa Ufalme, tulikuwa na hakika kwamba Mungu anatusaidia, kama alivyowasaidia Wakristo wa karne ya kwanza.’
8. Mabadiliko ya kisiasa na ya kiuchumi yamekuwa na matokeo gani katika kazi ya kuhubiri?
8 Bila shaka, si mateso tu yaliyochangia kuenea kwa Ukristo katika maeneo mengine. Mabadiliko ya kisiasa na ya kiuchumi yamewezesha ujumbe wa Ufalme uhubiriwe kwa watu wa lugha na mataifa mengi. Watu fulani kutoka katika maeneo yenye vita na hali ngumu za kiuchumi wamehamia katika nchi zenye utulivu na kujifunza Biblia wakiwa huko. Ongezeko la wakimbizi limefungua maeneo mapya ya lugha za kigeni. Je, unafanya yote uwezayo ili kuwahubiria watu “kutoka mataifa yote na makabila na jamii na lugha” walio katika eneo lenu?—Ufu. 7:9.
“Nipeni Mimi Pia Mamlaka Hii” (Mdo. 8:9-25)
“Simoni alipoona kwamba watu walipokea roho takatifu mitume walipoweka mikono juu yao, akawatolea pesa.”—Matendo 8:18
9. Simoni alikuwa nani, na kwa nini alivutiwa na Filipo?
9 Filipo alifanya ishara nyingi jijini Samaria. Aliwaponya walemavu na kuwafukuza roho waovu. (Mdo. 8:6-8) Mtu mmoja alivutiwa sana na uwezo wa Filipo wa kufanya miujiza. Aliitwa Simoni, naye alikuwa mchawi ambaye aliheshimiwa sana hivi kwamba watu walikuwa wakisema: “Mtu huyu ndiye Nguvu za Mungu.” Simoni alijionea mwenyewe nguvu za kweli za Mungu kutokana na miujiza iliyofanywa na Filipo, naye akawa mwamini. (Mdo. 8:9-13) Hata hivyo, baadaye nia ya Simoni ilijaribiwa. Jinsi gani?
10. (a) Petro na Yohana walifanya nini jijini Samaria? (b) Simoni alifanya nini alipoona wapya wakipokea roho takatifu baada ya Petro na Yohana kuwawekea mikono?
10 Mitume walipoona kwamba kulikuwa na ongezeko kubwa jijini Samaria, waliwatuma Petro na Yohana huko. (Ona sanduku “Petro Atumia ‘Funguo za Ufalme.’”) Mitume hao wawili walipofika waliweka mikono yao juu ya wanafunzi wapya, na kila mmoja wao akapokea roho takatifu.b Simoni alipoona hivyo, alistaajabu. Akawaambia mitume hao: “Nipeni mimi pia mamlaka hii, ili yeyote nitakayeweka mikono juu yake apokee roho takatifu.” Simoni hata alitaka kuwapa pesa wamuuzie pendeleo hilo takatifu!—Mdo. 8:14-19.
11. Petro alimwambia Simoni nini, naye Simoni aliitikiaje?
11 Petro alimkaripia Simoni na kumwambia: “Fedha yako na iangamie pamoja nawe, kwa sababu ulidhani utanunua zawadi ya bure ya Mungu kwa kutumia pesa. Wewe huna sehemu wala fungu katika jambo hili, kwa maana moyo wako si mnyoofu machoni pa Mungu.” Kisha, Petro akamhimiza Simoni atubu na kuomba msamaha. Petro akasema: ‘Mwombe Yehova dua, ili ikiwezekana, usamehewe nia mbaya ya moyo wako.’ Inaonekana kwamba Simoni hakuwa mtu mwovu; alitaka kufanya yaliyo sawa, lakini kwa muda hakuwa na maoni yanayofaa. Kwa hiyo, akawasihi mitume: “Mwombeni Yehova dua kwa ajili yangu ili nisipatwe na lolote kati ya mambo mliyosema.”—Mdo. 8:20-24.
12. “Usimoni” ni nini, na dini zinazodai kuwa za Kikristo zimetumbukiaje katika mtego huo?
12 Karipio hilo lapaswa pia kuwa onyo kwa Wakristo leo. Neno “usimoni” latokana na kisa hicho nalo linamaanisha kununua au kuuza vyeo, hasa vya kanisa. Usimoni umeenea sana katika dini zinazodai kuwa za Kikristo. Kitabu kimoja kinasema: ‘Historia ya mabaraza ya siri ya Mapapa inaonyesha wazi kwamba hakujawahi kuwa na uchaguzi wowote wa kanisa usiokuwa na usimoni, na katika visa vingi, usimoni wenyewe ulikuwa usimoni mbaya sana, wenye kuaibisha, tena ulifanywa waziwazi.’—The Encyclopædia Britannica (1878).
13. Wakristo wanapaswa kuepuka usimoni kwa njia gani?
13 Wakristo wanapaswa kujihadhari na dhambi ya usimoni. Kwa mfano, hawapaswi kujaribu kupata mapendeleo kutanikoni kwa kuwapa zawadi au kuwasifu kupita kiasi ndugu wenye madaraka. Kwa upande mwingine, ndugu hao wenye madaraka wanapaswa kuwa waangalifu wasiwaonyeshe watu wenye mali upendeleo. Yote hayo ni usimoni. Watumishi wote wa Mungu wanapaswa kujiendesha kama ‘walio wadogo,’ na kuonyesha subira huku wakiiruhusu roho takatifu ya Yehova iweke rasmi wale wanaostahili. (Luka 9:48) Katika tengenezo la Mungu, hakuna nafasi kwa ajili ya watu wanaojaribu ‘kujitafutia utukufu wao wenyewe.’—Met. 25:27.
“Je, Kweli Unajua Unayosoma?” (Mdo. 8:26-40)
14, 15. (a) “Towashi Mwethiopia” alikuwa nani, na Filipo alikutana naye jinsi gani? (b) Mwethiopia huyo aitikiaje ujumbe wa Filipo, na kwa nini uamuzi wake wa kubatizwa haukutokana tu na msisimko? (Ona maelezo ya chini.)
14 Malaika wa Yehova anamwambia Filipo aende kwenye barabara inayoshuka kutoka Yerusalemu mpaka Gaza. Muda mfupi baadaye, Filipo anaelewa sababu ya kutumwa baada ya kukutana na towashi Mwethiopia ambaye “alikuwa akimsoma kwa sauti kubwa nabii Isaya.” (Ona sanduku “‘Towashi’ Katika Maana Gani?”) Roho takatifu ya Yehova ilimwongoza Filipo alikaribie gari la mtu huyo. Huku akikimbia kandokando ya gari hilo, Filipo alimuuliza Mwethiopia huyo: “Je, kweli unajua unayosoma?” Mwethiopia akajibu: “Ninawezaje kuyaelewa mtu fulani asiponiongoza?”—Mdo. 8:26-31.
15 Mwethiopia akamsihi Filipo apande kwenye gari. Wazia mazungumzo yaliyofuata! Kwa muda mrefu, haikujulikana ni nani anayezungumziwa katika unabii unaohusu “kondoo,” au “mtumishi,” katika kitabu cha Isaya. (Isa. 53:1-12) Hata hivyo, walipokuwa wakiendelea na safari, Filipo alimfafanulia kwamba Yesu Kristo ndiye anayezungumziwa katika unabii huo. Kama wale waliobatizwa siku ya Pentekoste, mwaka wa 33 W.K., Mwethiopia huyo ambaye tayari alikuwa Myahudi mgeuzwa imani akajua mara moja jambo analopaswa kufanya. Kisha akamwambia Filipo. “Tazama! Hapa kuna maji; ni nini kinachonizuia kubatizwa?” Bila kukawia, Filipo akambatiza Mwethiopia huyo!c (Ona sanduku “Kubatizwa ‘Mahali Penye Maji.’”) Kisha, roho ya Mungu ikamwongoza Filipo kwenda katika mgawo mwingine huko Ashdodi, ambako aliendelea kutangaza habari njema.—Mdo. 8:32-40.
16, 17. Malaika wanahusika jinsi gani katika kazi ya kuhubiri leo?
16 Wakristo leo wana pendeleo la kushiriki kazi kama iliyofanywa na Filipo. Mara nyingi, wanaposafiri wanatumia nafasi hiyo kuwahubiria watu ujumbe wa Ufalme. Katika visa vingi, wanapopata mtu mnyoofu, hawashangai kwa sababu Biblia inaonyesha wazi kwamba malaika wanaelekeza kazi ya kuhubiri ili ujumbe huo ufikie “kila taifa na kabila na lugha na watu.” (Ufu. 14:6) Yesu alitabiri kwamba malaika wangeelekeza kazi ya kuhubiri. Katika mfano wa ngano na magugu, Yesu alisema kwamba wakati wa mavuno, au umalizio wa mfumo wa mambo, “wavunaji ni malaika.” Pia, alisema, viumbe hao wa kiroho “watakusanya kutoka katika Ufalme wake vitu vyote vinavyosababisha kukwazika na watu wenye mazoea ya kuasi sheria.” (Mt. 13:37-41) Wakati huohuo, malaika watakusanya watu watakaorithi Ufalme wa mbinguni, kisha watakusanya “umati mkubwa” wa “kondoo wengine,” ambao Yehova anawavuta katika tengenezo lake.—Ufu. 7:9; Yoh. 6:44, 65; 10:16.
17 Jambo moja linalothibitisha kwamba malaika wanaelekeza kazi yetu ni kwamba watu fulani tunaowapata katika huduma yetu husema kwamba wamekuwa wakisali ili wapate mwongozo wa kiroho. Fikiria jambo moja lililoonwa: Wahubiri wawili wa Ufalme walikuwa wakihubiri pamoja na mtoto mdogo. Ilipofika mchana, wahubiri hao walipotaka kuondoka kwenye eneo, yule mtoto alitaka sana waende nyumba inayofuata. Alienda kubisha mlango huo! Mwanamke alipoufungua mlango, Mashahidi hao wawili wakakaribia ili kuzungumza naye. Walishangaa kusikia kwamba mwanamke huyo alikuwa ametoka tu kusali mtu amtembelee na kumsaidia kuelewa Biblia. Funzo la Biblia likaanzishwa!
“Mungu, ikiwa upo, tafadhali nisaidie”
18. Kwa nini hatupaswi kamwe kuipuuza huduma yetu?
18 Ukiwa mmoja wa wahubiri katika kutaniko la Kikristo, una pendeleo la kushiriki bega kwa bega katika kazi ya kuhubiri ambayo leo inafanywa kwa kiwango kikubwa zaidi. Usilipuuze kamwe pendeleo hilo. Ukidumu katika kazi hiyo, utapata shangwe kubwa inayotokana na kutangaza “habari njema kumhusu Yesu.”—Mdo. 8:35.
a Filipo huyu si mtume Filipo. Badala yake, ni Filipo ambaye, kama Sura ya 5 ya kitabu hiki inavyoeleza, alikuwa mmoja wa “wanaume saba wenye sifa nzuri” ambao waliwekwa rasmi kusimamia ugawaji wa kila siku wa chakula kati ya Wakristo wajane waliozungumza Kigiriki na waliozungumza Kiebrania katika jiji la Yerusalemu.—Mdo. 6:1-6.
b Inaonekana kwamba kwa kawaida wanafunzi wapya walitiwa mafuta, au kupokea roho takatifu walipobatizwa. Baada ya kupokea roho hiyo, wakawa na tumaini la kutawala wakiwa wafalme na makuhani pamoja na Yesu mbinguni. (2 Kor. 1:21, 22; Ufu. 5:9, 10; 20:6) Hata hivyo, katika kisa hiki, Wakristo wapya hawakutiwa mafuta walipobatizwa. Walipokea roho takatifu pamoja na uwezo wa kufanya miujiza walipowekewa mikono na Petro na Yohana.
c Huo haukuwa msisimko tu. Kwa kuwa alikuwa Myahudi mgeuzwa imani, tayari alikuwa na ujuzi wa Maandiko, kutia ndani unabii kuhusu Masihi. Baada ya kuelewa jukumu la Yesu katika mpango wa Mungu, hakuna jambo lililomzuia kubatizwa.
-