Nendeni! Mkafanye Wanafunzi
1, 2. (a) Maneno “sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia” yangehusu kadiri mpya namna gani baada ya wakati ya kupita? (b) Yesu alionyeshaje kwamba mgawo wa Kikristo wa kutoa ushuhuda haungekoma wakati wa Wakristo wa karne ya kwanza?
KWA habari ya wakati na eneo, mgawo wa kuaga wa Yesu wa kuwa mashahidi kwenye miisho ya dunia, ambao umeandikwa katika Matendo 1:8, haukukoma na Wakristo wa kwanza. Walifanya kazi nzuri kwa kutangaza “habari njema” mbali sana kwa kadiri walivyoweza “katika ulimwengu wote” au ‘katika kuumba kote kuliko chini ya mbingu’ katika siku zao. (Kol. 1:5, 6, 23, NW) Walakini kwa kadiri wakati ulivyopita maneno hayo yangehusu kadiri mpya, kwa kadiri ambavyo idadi ya watu yenye kuongezeka ilivyosambaa juu ya kontinenti sita na visiwa vingi, kwa halisi “kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.”
2 Yesu alijua jambo hilo vizuri. Kwa ajili ya faida ya wanafunzi wake—si Wakristo wa karne ya kwanza tu bali Wakristo wote kufika miaka hii, sana-sana Wakristo wale wenye kuishi duniani wakati wa “mwisho wa taratibu ya mambo” —Kristo aliyefufuliwa alisema hivi:
“Mimi nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi. Na, tazama! mimi nipo pamoja na ninyi siku zote mpaka mwisho wa taratibu ya mambo.”—Mt. 28:18-20, NW.
3. Kulingana na mwanachuo mmoja, Wakristo waliotiwa mafuta wangekuwa na kazi gani ya kutimiza?
3 Hapo kuna uthibitisho kwa mtu ye yote anayeuhitaji kwamba mgawo ambao Kristo aliwapa wanafunzi wake siku ya kupaa kwake mbinguni haukutimizwa kabisa katika karne ya kwanza W.K. Ungeendelea kutimizwa kufika “mwisho wa taratibu ya mambo.” Na nani? Kwa kupendeza, kuhusu Matendo 1:8, Profesa F. F. Bruce wa Rylands anasema hivi: “Kama vile Yesu Mwenyewe alivyokuwa ametiwa mafuta wakati wa ubatizo Wake kwa Roho Takatifu na nguvu, ndivyo wanafunzi Wake sasa walivyopaswa kutiwa mafuta kwa njia iyo hiyo na kuwezeshwa kuendeleza kazi yake. Kazi hiyo ingekuwa kazi ya kutoa ushuhuda—mazungumzo ambayo yanatokeza katika mahubiri ya mitume katika [kitabu cha] Matendo (linganisha Sura 2:32; 3:15; 5:32; 10:39; 13:31; 22:15, n.k.). Nabii mmoja wa [Agano la Kale] alikuwa ameita Israeli mashahidi wa Mungu katika ulimwengu (Isa. 43:10; 44:8); kazi ambayo Israeli ikiwa taifa haikuwa imetimiza ilitwaliwa na Yesu, akiwa Mtumishi mkamilifu wa Bwana, naye akaipitisha kwa wanafunzi Wake.”
4. Mabaki wamekuwa wakitimiza mgawo huo tangu wakati gani, na sababu gani jambo hilo lilihitaji imani nyingi sana?
4 Ndiyo, mgawo wa kuwa mashahidi kwenye miisho ya dunia na kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote wakati huu wa “mwisho wa taratibu ya mambo” wanapewa mabaki waliotiwa mafuta wa Israeli wa kiroho, ambao wakiwa jamii ni “mtumishi” wa Yehova na “mashahidi” wake. (Isa. 43:10-12) Wamekuwa wakitimiza kwa uaminifu mgawo huo sana-sana tangu mwaka 1919. Lakini Wakristo hao waliotiwa mafuta ambao ni maelfu chache wangewezaje kufikia mabilioni ya wanadamu waliotawanyika “kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia”? Ilihitaji imani nyingi sana kama nini kuweza kufikiri tu juu ya kazi hiyo!
5. Ni njia zipi ambazo zimesaidia Wakristo wa kisasa kueneza ushuhuda kwenye miisho ya dunia?
5 Soma kwa mara nyingine historia ya kisasa ya Mashahidi wa Yehovaa nawe utaona kwamba mojayapo ya njia kubwa zinazotumiwa kueneza ujumbe wa Ufalme mbali na karibu imekuwa kugawa magazeti, yaani, Mnara wa Mlinzi na gazeti mwenzi wake Amkeni! (zamani liliitwa Golden Age, kisha Consolation). Magazeti hayo ambayo msingi wake ni Biblia kwa halisi yameenezwa mamilionib nyingi kwa lugha zaidi ya 100 na kwenye pembe nne za dunia.
“MAJESHI YA WAPANDA FARASI”
6, 7. (a) Mabaki waliotiwa mafuta wanafananishwa namna gani katika Ufunuo, sura ya 9, nao wanaweza kutumia nini? (b) Wanafananisha nini? (c) Kitabu “Then Is Finished the Mystery of God’ kilitoa maelezo gani juu ya unabii huo?
6 Katika, Ufunuo sura ya 9, mabaki waliotiwa mafuta wanafananishwa na “malaika wanne,” au wajumbe, wanaofunguliwa toka utumwani wa Babeli Mkuu, “kwenye mto mkubwa Frati.” (Mistari 14, 15) Wajumbe hao waliofunguliwa wanaweza kutumia “majeshi ya wapanda farasi” yenye hesabu “elfu ishirini mara elfu kumi,” au 200,000,000, ambayo kwa njia ya mfano yanatumiwa ‘kuua’ sehemu kubwa ya wanadamu. (Mistari 16-19) “Farasi” katika njozi hiyo wanafananisha njia zinazotumiwa na mabaki waliotiwa mafuta kutangaza ujumbe wa hukumu wa Yehova ambao hasa unaelekezwa juu ya Jumuiya ya Wakristo, sehemu yenye kulaumika zaidi ya “Babeli Mkuu” (milki ya ulimwengu ya dini ya uongo).
7 Kikiieleza njozi hiyo yenye kuvuta akili, kitabu “Then Is Finished The Mystery of God” kinasema hivi: “Kupiga mbio kwa ‘farasi’ hao wa mfano kuliongezeka sana wakati magazeti ya Sosaiti yalipoanza kutolewa barabarani, nyumba kwa nyumba, duka kwa duka.” (Kurasa 246, 247) Basi, ingawa “farasi” hao wa mfano wanatia ndani vitabu, vijitabu na trakti, bila shaka magazeti yametimiza sehemu ya maana katika kueneza ushuhuda wa Ufalme “kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia,” nayo yangali yanaitimiza.c
8. Mabaki waliotiwa mafuta vilevile wamtii amri ya Kristo ya ‘kwenda kufanya wanafunzi’ kwa njia gani?
8 Si kwamba tu mabaki yaliotiwa mafuta wameongoza kwa juhudi na ujasiri farasi hao wa mfano juu ya ngome za dini ya uongo, bali pia wametii amri ya Kristo ya ‘kwenda kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza.’ Tangu mwaka 1935 hesabu yenye kuongezeka ya watu wamesoma ujumbe wa hukumu ambao umechapwa kuhusu milki ya ulimwengu ya dini ya uongo nao wametii agizo la kimungu la ‘kutoka katika “Babeli Mkuu.” ‘ (Ufu. 18:1-4) Wamejiweka wakf kwa Yehova Mungu nao wamebatizwa “katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu.” Wao wenyewe wakiwa wamesaidiwa na Mnara wa Mlinzi na Amkeni, wamejiunga na mabaki waliotiwa mafuta kugawa magazeti hayo mazuri mbali na karibu, ndiyo, “hata miisho ya dunia.”—Isa. 49:6.
JE! WEWE U MTANGAZAJI MWENYE BIDII WA “HABARI NJEMA”?
9. Wajibu wa kila Mkristo ni nini?
9 Agizo la kuwa mashahidi “kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia” na kwenda ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote’ linahusu wote wanaodai kuwa Wakristo. Hivyo, mashahidi wote wa Yehova walio wakf wanapaswa kuwa na nia kubwa, yenye kuongozwa na moyo ya kushiriki kutimiza mgawo huo wenye pendeleo.
10. Washiriki wa “mkutano mkubwa” wanapaswa kukumbuka nini? (b) Hata hivyo, maoni ya wengine wamekuwa nini?
10 Iwapo sasa wewe ni mshiriki wa “mkutano mkubwa,” unaosimuliwa katika Ufunuo 7:9-17, kumbuka kwamba ili ‘kuokoka dhiki kubwa’ lazima uendelee kusema: “Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo,” nawe usiache kumtolea Yehova ‘utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake’ (NW). Hata hivyo, hivi karibuni wengine wamesitawisha maoni ya kwamba inatosha kuhudhuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo mara moja kwa mwaka, kusonga pamoja na maarifa ya karibuni ya Biblia kwa kusoma vitabu vya Sosaiti, kuhudhuria mikutano pindi kwa pindi na kuacha mwanga wao uangaze kwa kuishi maisha mazuri na kutoa ushuhuda pindi kwa pindi iwapo nafasi na wakati nafasi ya kufanya hivyo inapojitokeza.
11. Je! mgawo wa Kikristo unaweza kutimizwa kwa kuishi maisha mazuri peke yake, au kwa njia gani nyingine?
11 Lakini je! hiyo inatosha? Ushuhuda wa Kikristo ungeweza kutolewaje “kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia” kama Wakristo wa kwanza na mabaki waliotiwa mafuta wa kisasa wangeketi tu mahali walipokuwa, wakiishi maisha mazuri? Ili ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,’ kwanza walipaswa ‘KWENDA’! Ndiyo, walipaswa kuondoka na kutoa ushuhuda “nyumba kwa nyumba” na “katika nyumba za watu.” (Matendo 5:42, New World Translation; Today’s English Version) Kutoa ushuhuda waziwazi ni sehemu ya lazima ya “utumishi mtakatifu.”
12. Huenda wengine wakawa wamesahau nini, nao sasa wanatiwa moyo wafanye nini?
12 Wewe unasimama wapi? Je! umekuwa mhubiri wa Ufalme ambaye amepata furaha ya moyoni kwa kujulisha “habari njema” na pia hukumu za Yehova kupitia kwa “farasi” wa mfano, sana-sana magazeti ya Sosaiti? Iwapo umelegea au kuacha kabisa, je! ni kwa sababu umeacha kuona maana ya kiroho ya utendaji huo, yaani, kusaidia mabaki waliotiwa mafuta watimize mgawo wao wa “kutangaza mwaka wa nia njema upande wa Yehova na siku ya kisasi upande wa Mungu wetu”? (Isa. 61:1, 2, 5, NW) Basi huu ndio wakati wako kupata tena furaha hiyo kwa kujishughulisha tena katika utumishi wa Yehova.
JE! UNAONA VIGUMU KUSEMA UNAVYOTAKA?
13, 14. (a) Huenda wengine wakawa wameacha kuhubiri nyumba kwa nyumba kwa sababu gani? (b) Ni mapendekezo gani yanayofaa yanayotolewa yawasaidie washinde woga wao?
13 Pengine umeona kutoa ushuhuda nyumba kwa nyumba kukiwa kugumu kwa sababu husemi kwa ufasaha unayotaka kusema. Au pengine wewe ni mmoja wa mamilioni wanaothamini kusoma magazeti ya Sosaiti na kukutana na Mashahidi wa Yehova katika Majumba yao ya Ufalme, lakini ambao hawajapata kushiriki katika kazi ya kutoa ushuhuda nyumba kwa nyumba kwa sababu ya kuogopa hawatajua la kusema. Unafahamu vizuri kwamba ni lazima ushuhuda utolewe “kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia” na kwamba lazima wanafunzi wafanywe “kutoka kwa watu wa mataifa yote,” lakini hujioni unaweza kutazamana na watu mlangoni pao. Unajua kwamba lazima ufanye hivyo nawe unatimiza matakwa ya Kimaandiko lakini unaona huwezi. Moyo wako unathamini kabisa kweli ya Neno la Mungu, walakini miguu yako inakataa kukupeleka kwenye mlango wa kwanza kwa sababu unaogopa kwamba midomo yako haitasema maneno unayotaka. Unaweza kufanya nini?
14 Unaweza kuanza kwa kuchukua Biblia yako na kusoma kwa mara nyingine Warumi 10:8-15. Hiyo inapaswa kufanya miguu yako itake kutoka nje na “kuhubiri habari ya mema.” Halafu, mwombe Yehova nguvu—ndiyo ‘yeye atoaye nguvu.’ (Flp. 4:13, NW; linganisha Matendo 1:8.) Kisha, wakati mwingine uendapo kwenye Jumba la Ufalme au kwenye funzo la kitabu la kundi la mahali pako, mwulize mmoja wapo wa wazee Wakristo akujulishe Shahidi mwenye ujuzi wa kutangaza “habari njema” nyumba kwa nyumba. Mhubiri huyo wa Ufalme atakutazamia ushirikishe wenye nyumba katika mazungumzo yenye msingi wa Biblia tangu hapo mwanzoni. Inaelekea sana atapendekeza kwamba mtumie wakati mfupi pamoja mkichunguza matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kabla ya kwenda nyumba kwa nyumba kutoa magazeti hayo mazuri kwa watu.
15. Sababu gani kazi ya kugawa magazeti ni njia inayofaa ya kupata ujuzi katika kutoa ushuhuda nyumba kwa nyumba na katika kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani?
15 Kutoa ushuhuda kwa kutumia magazeti ni njia inayofaa wakati wa kuanza upya au kuanza tena kufanya kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Bila shaka ni mojayapo ya njia rahisi na bora zaidi za kufikia watu na kupata ujuzi wa kutoa ushuhuda nyumba kwa nyumba. Kila toleo linatoa mambo mapya ya kuzungumza. Pamoja na hayo, ukirudia wote wanaokubali gazeti, karibuni utakuwa na orodha ya watu ambao unaweza kurudia kwa ukawaida ukiwa na matoleo ya karibuni zaidi. Polepole utawajua watu hao. Makala kama mfululizo wa “Umetaka Kujua . . . ?” (katika Amkeni!) zitakusaidia kuanzisha mazungumzo na hata kuanzisha funzo la Biblia. Somea mwenye nyumba fungu la kwanza, uliza swali la kwanza lililoandikwa (kichwa kidogo)—mruhusu ajibu—kabla ya kusoma fungu linalofuata na maandiko yo yote yaliyoandikwa. Kisha nenda kwenye swali lifuatalo (kichwa kidogo), uendelee hivyo kwa wakati alio nao mwenye nyumba. Sababu gani usijaribu hivyo? Utashangazwa na furaha na uradhi wa kimungu utakaopata kwa kumtolea Yehova huo “utumishi mtakatifu.”—-Ufu. 7:15, NW.
VIJANA WAKRISTO, ENDESHENI “FARASI” HAO!
16. Ni maandiko gani yanayoonyesha kwamba hata Wakristo vijana wanatiwa ndani pia?
16 Daraka la kuwa “mashahidi . . . kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia” linachukuliwa na Wakristo wote, vijana kwa wazee. Zaburi ya kiunabii ya 110 inasema hivi kumhusu Kristo:
“Fimbo ya nguvu yako Yehova ataituma toka Sayuni, akisema hivi: ‘Nenda uwe ukitiisha katikati ya adui zako.’ Watu wako watajitoa wenyewe kwa moyo wa kupenda siku ya jeshi lako la vita. Katika fahari za utakatifu, kutoka tumbo la uzazi la mapambazuko, unalo shirika la wanaume vijana kama matone ya umande.” (Zab. 110:2, 3, NW)
Zaburi nyingine ya Kimasihi inasema juu ya “wanawali” ambao wangekuwa “wenzi” wa bibi-arusi wa Kristo. (Zab. 45:13, 14, NW) Vifungu hivyo vyote vinahusu mabaki waliotiwa mafuta na “mkutano mkubwa” ambao kwa njia halisi unatia ndani “vijana” na “wanawali.” Basi, ninyi, pia, mwapaswa ‘kujitoa wenyewe kwa moyo’ na kuwa “wenzi” washikamanifu wa waliobaki wa jamii ya bibi-arusi aliyetiwa mafuta walioko duniani, ambao pia wanafananishwa na wale “malaika wanne” wanaoongoza “majeshi ya wapanda farasi” juu ya milki ya ulimwengu ya kidini ya Shetani.—Ufu. 9:15-19; 21:2, 9.
17. Vijana wengi wazuri wa kiume na wa kike wanatoaje “utumishi mtakatifu”?
17 Vijana wengi wa kiume na wa kike wanatoa “utumishi mtakatifu” katika Brooklyn na katika yale matawi 97 yaliyopo duniani pote. Wakiwa hapo, wanafanya kwa moyo wa kupenda kazi mbalimbali zinazohusiana moja kwa moja na kutayarisha na kutuma “farasi” wa mfano—vitabu vyenye ujumbe wa hukumu unaohusu “siku ya kisasi upande wa Mungu wetu” na vilevile vyenye kutoa kweli zenye kufariji juu ya “mwaka wa nia njema upande wa Yehova.” (Isa. 61:1, 2, NW) Wote hao wenye moyo wa kupenda wanashiriki kutayarisha “farasi” hao watumiwe shambani, na pia wanashiriki katika utumishi wa shambani wenyewe, wakitumia sana “farasi” hao, sana-sana magazeti.
18. (a) Wakristo wengine vijana wanajionyeshaje kuwa wenzi wenye juhudi wa mabaki? (b) Mfalme na “ndugu” zake wanaionaje juhudi yao?
18 Wakristo wengine vijana ‘wanajitoa kwa moyo wa kupenda’ na kujionyesha kuwa wenzi wenye juhudi wa mabaki waliotiwa mafuta wakiwa “mapainia,” yaani, kwa kutoa saa zisizopungua 1,000 kwa mwaka katika kazi ya kutoa ushuhuda waziwazi. Juhudi ya hao Wakristo inamvutia sana Mfalme Yesu Kristo na “ndugu” zake waliotiwa mafuta ambao wangali duniani.—Linganisha Mathayo 25:34-40.
19. Ni kitia-moyo gani wanachopewa vijana wengineo Wakristo?
19 Lakini kuna maelfu mengi ya “vijana” na “wanawali” wengine ndani ya makundi ya watu wa Yehova. Je! ‘unajitoa mwenyewe kwa moyo wa kupenda siku ya jeshi la Kristo’? Au unaacha “farasi” hao wa mfano walundamane chumbani mwako au wakae bila kutumiwa katika mfuko wako wa kutolea ushuhuda? Endesha “farasi” hao! Nenda shambani baada ya saa za shule kwisha, mwishoni mwa juma na vipindi mbalimbali vya likizo ulivyo navyo katika mwaka wote. Utumishi wa painia-msaidizi unakupa nafasi nzuri sana ya ‘kujitoa kwa moyo wa kupenda’ kwa “utumishi mtakatifu.” Nayo kazi ya kugawa magazeti ni njia ya kutoa ushuhuda wa Kikristo ambayo inafaa sana-sana kwa vijana. Unaweza kuifanya nayo inaweza kutokeza mambo mema.
MASHAHIDI WENYE KUTENDA MPAKA MWISHO
20, 21. (a) Kristo aliwapa Wakristo wa karne ya kwanza na wale wenye kuishi katika “siku za mwisho” mgawo gani? (b) Ushahidi wa profesa wa historia unaonyesha nini? (c) Mashahidi wa Yehova wametumiaje magazeti hayo kwa kusudi hilo?
20 Kwa Wakristo wa kwanza Yesu alisema hivi: “Mtakuwa mashahidi wangu mimi . . . kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” (Matendo 1:8, NW) Kwa Wakristo wenye kuishi katika “siku za mwisho,” au “wakati wa mwisho,” alisema hivi kwa njia ya kiunabii: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.”—Mt. 24:14, NW; Dan. 12:4; 2 Tim. 3:1.
21 Kuhani mkuu wa Kiyahudi, adui mkuu wa Wakristo wa kwanza, alikubali hivi kwa masikitiko: “Tazameni! mmeujaza Yerusalemu mafundisho yenu.” (Matendo 5:28, NW) Katika kitabu chake These Also Believe, profesa wa historia’ Charles Braden aliandika hivi: “Kwa njia halisi Mashahidi wa Yehova wameieneza dunia yote kwa ushuhuda wao. . . . Inaweza kusemwa kwa kweli kwamba hakuna kikundi kimoja cha kidini katika ulimwengu kilichoonyesha juhudi na uendelevu mwingi katika kujaribu kueneza habari njema za Ufalme zaidi ya Mashahidi wa Yehova.” Ingawa katika mwaka 1919 walikuwa maelfu chache, mabaki waliotiwa mafuta walikubali mwaliko huo. Kupitia kwa “nguvu” za roho takatifu na kwa msaada wenye kuongezeka kutoka kwa “mkutano mkubwa” wa wenzi wao wenye kuongezeka, ‘kwa njia halisi wameieneza dunia yote kwa ushuhuda wao.’ Tangu 1919 mpaka 1980, Wakristo hao wamegawa nakala zaidi ya 4,750,000,000 (bilioni nne na robo tatu) za Mnara wa Mlinzi na gazeti mwenzi wake (The Golden Age; Consolation; sasa ni Awake!).
22. Mambo ya hakika yanaonyesha nini, na kwa hiyo sote tunatiwa moyo tufanye nini?
22 Magazeti hayo mazuri ya Kikristo yamekuwa njia ya maana ya kutolea ushuhuda kwenye miisho ya dunia na kufanya “wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,” nayo yangali yanafanya hivyo. (Mt. 28:19, 20, NW) Mambo ya hakika yanaonyesha kwamba kungali kwatakiwa ushuhuda mwingine utolewe. Basi nendeni kwenye “farasi” wenu enyi mashahidi Wakristo waaminifu! Wachukueni na kuwaendesha “shambani,” naye Yehova aendelee kubariki matumizi makubwa ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! katika siku zijazo.
[Maelezo ya Chini]
a Tazama vitabu Jehovah’s Witnesses in the Divine Purpose na Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi cha Yehova 1975, ambavyo vimechapwa na Watch Tower Society.
b Katikati ya 1919 na 1980, magazeti 4,767,784,340 yalienezwa ulimwenguni pote na Mashahidi wa Yehova, bila kutia ndani milioni za nakala zilizotumwa kwa waandikishaji wa Mnara wa Mlinzi na Amkeni. Hiyo ni zaidi ya maradufu ya hesabu ya trakti na vijitabu vilivyoenezwa wakati wa kipindi icho hicho.
c Kwa maelezo kamili ya unabii huo, tazama kitabu “Then Is Finished the Mystery of God,” kurasa 238-247.
[Chati katika ukurasa wa 15]
Orodha ya Uenezaji wa Utendaji wa Ulimwenguni Pote
Miaka Trakti na Vijitabu Magazeti Vitabu Jumla
1879 —
1917 419,078,170 (Pamoja na magazeti) 9,894,056 428,972,226
1918 102,775 13,140 256,609 372,524
1919 —
1980 2,322,888,592 4,767,784,340 450,642,739 7,541,315,671
Jumla Kuu
Jumla 2,742,069,537 4,767,797,480 460,793,404 7,970,660,421