Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/93 uku. 1
  • Je! Waweza Kumtumikia Yehova Ukiwa Painia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Waweza Kumtumikia Yehova Ukiwa Painia?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Utumishi wa Painia—Je, Wakufaa Wewe?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Mapainia Hutoa na Kupokea Baraka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Kutembea kwa Nafsi Yote katika Njia ya Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Ndugu Zaidi Wanahitajiwa Katika Utumishi wa Painia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 1/93 uku. 1

Je! Waweza Kumtumikia Yehova Ukiwa Painia?

1 Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya, msemaji mmoja aliuliza hivi: “Je! wewe waweza kupainia? Je! utapainia?” Alionyesha kwamba maswali hayo yanafaa kwa sababu Har–Magedoni iko karibu sana, na hilo lafanya kazi ya kuhubiri iwe ya haraka zaidi ya wakati mwingine wowote.—1 Kor. 7:29a.

2 Hakuna shaka kwamba kufanya upainia ni kazi ngumu. Kunahitaji kujidhabihu na kupanga mambo vizuri. Hata hivyo, kazi yetu ngumu hudumani “siyo bure.” (1 Kor 15:58) Je! lilo hilo laweza kusemwa kuhusu utendaji mwingine ambao huenda tukachagua kufuatia na unaotumia wakati na nishati yetu? Kumpenda Yehova kunawasukuma Wakristo wawe wenye bidii katika utumishi wake, na bidii kwa ajili ya utumishi wa Yehova imeongoza wengi wachukue kazi ya upainia.—1 Yoh. 5:3; Ufu. 4:11.

3 Wengi kati ya watumishi wa Yehova wachanga wanaomaliza shule ya upili hivi karibuni wanafikiri kwa uzito juu ya kufanya upainia. Hilo lafaa kabisa. Ni kazi-maisha gani iwezayo kuwa yenye umaana zaidi ya huduma ya wakati wote? (Mt. 6:33) Ni lazima habari njema za Ufalme wa Mungu zihubiriwe: hiyo ni kazi ya Yehova, na ni pendeleo lililoje kujishughulisha sana nayo kutoka ujana wa mtu na kuendelea!—Mt. 24:14.

4 Je! nyinyi wazazi huwatia moyo watoto wenu wachukue utumishi wa wakati wote? Je! watoto wenu huelewa kwa wazi kwamba mnawataka watumie mioyo, nafsi, akili, na nguvu zao zote katika kazi hiyo inayostahili? (Mk. 12:30) Wahubiri wengi wachanga hujitayarisha wenyewe kwa ajili ya kazi ya upaina wa kawaida kwa kushiriki wakiwa mapainia wasaidizi kwa kila fursa wakati wa miaka yao wakiwa shuleni. Kwa hakika ujitoaji huo kwa Yehova huuchangamsha moyo wake!—Mit. 27:11.

5 Bila shaka, si kila mtu aliye na hali zinazoruhusu utumishi wa upainia. Hata hivyo, iwe umefunga ndoa au ni mseja, iwe wewe ni kijana au mzee katika miaka, je, umefikiria kwa uzito na kwa sala kumtumikia Yehova ukiwa mhudumu painia wa habari njema? (Kol. 3:23) Wenzi wa ndoa wengi wachanga wanajitahidi kupanua huduma yao ili mmoja wao au wote wawili waweze kufanya upainia.

6 Ikiwa huwezi kufanya upainia wa kawaida kwa sasa, je, waweza kutumikia ukiwa painia msaidizi? Yaelekea wahubiri wengi kunduni mwako wanapanga kufanya hivyo katika Aprili. Je! waweza kujiunga nao? Ingawa watumishi wote wa Yehova waaminifu-washikamanifu hupokea baraka nyingi, baraza za ziada zawangojea wale wanaoweza kutumia wakati zaidi katika utumishi wa Ufalme wakiwatafuta wale wenye mfano wa kondoo.—Mdo. 20:35.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki